Skip to main content

Posts

Showing posts from October, 2016

Mwanamitindo wetu leo

Jina  :   Leah  Rajab  Umri :  Miaka  22 Anaishi  : Dar  Es  Salaam. Fani : Mitindo

MWANAMITINDO WETU LEO

Jina : Grace  W. Masatu. Umri : Miaka  21 Anaishi : Dar Es Salaam. Fani : Mitindo. Elimu : Chuo  Kikuu.

Mimea Inayo Tibu Tatizo La Homa Ya Mapafu ( Pneumonia ) Kwa Watoto.

Mbefu; unaotumika  katika  tiba  dhidi  ya  ugonjwa  wa  Homa  ya  Mapafu Mbefu Chimtemte: Majani  ya  mmea  huu  hutumika  katika  tiba  dhidi  ya  ugonjwa  wa  Homa  ya  Mapafu Vigengegenge Msada Msada Homa ya mapafu ni aina ya maambukizi yanayoathiri mapafu. Ni ugonjwa ambao unaua watoto wengi hasa katika nchi zinazoendelea duniani. Inakadiriwa kwamba watoto karibu milioni 1.6 walio chini ya miaka 5 wanakufa kila mwaka kutokana na ugonjwa huu. Kutokana na vifo vingi vinavyotokana na homa ya mapafu tarehe 12 ya mwezi wa Novemba kila mwaka imefanywa kuwa siku rasmi ya homa ya mapafu duniani, ambapo nembo ya siku hiyo ni nguo za rangi ya bluu. Muundo wa Mapafu Mapafu yanajumuisha mirija mikubwa ya hewa ( bronchi ) ambayo hugawanyika kufanya mirija midogo zaidi ya hewa ( bronchioles ), ambayo nayo hutengeneza vifuko vidogo vidogo ya hewa ( alveoli ). Vifuko hivi vidogo vya hewa ( alveoli ) vina mishipa ya kupitisha damu ( capillaries ) ambayo husa

Sarah Nkuki : Mwanamitindo Chipukizi mwenye ndoto za kufika mbali katika fani ya mitindo.

Fani  ya  mitindo  inazidi  kukua  kwa  kasi  nchini  Tanzania, huku  wasichana  wengi  wakijitokeza  kuonyesha  vipaji  vyao  katika  fani  ya  mitindo.  Sarah  Nkuki,( 19 )  mkaazi  wa  Iringa, ni miongoni  mwa  mabinti  wa  kitanzania  wanao  jitokeza  kuonyesha  mapenzi  makubwa  katika  fani  ya  mitindo. Akiwa  mtoto  wa  mwisho  kati  ya  watoto  watatu  kwa  upande  wa  baba  na  mama  yake, Sarah  anasema  ameanza  kuhusudu   kuwa  mwanamitindo  tangu  akiwa  anasoma  shule  ya  msingi. Kwa  sasa, Sarah  anachukua  Certificate  ya  Inforamation Technology ( IT)  katika  chuo  kimoja  kilichopo  mjini  Iringa. Katika  tasnia  ya  mitindo, Sarah  anavutiwa  zaidi  na  Hamisa  Mobeto  kwa  hapa  Tanzania, na  nje  ya  nchi  anavutiwa  na  Naomi  Campbell. Sarah  anasema  changamoto kubwa  anayo  ipata ni  kutokuwa  na  management  nzuri  itakayo  weza  kusimamia  kazi  zake  na  kumuendeleza   katika  fani  ya  mitindo.

Hope Lucy Ruhinda; NAPENDA KUWA NA MWANAUME ASIE NIPANGIA AINA YA MAVAZI YA KUVAA

Hope  Lucy  Ruhinda;   NAPENDA   KUWA  NA   MWANAUME  ASIE NIPANGIA  AINA  YA  MAVAZI  YA  KUVAA   Hope  Lucy  Ruhinda  ( 25 ) ni  mwanamitindo  anae  fanya  vizuri sana  katika  tasnia ya  urembo  nchini  Afrika.   Mwanamitindo  huyu ambaye  ni  mtanzania  kwa  mama, na  mnyarwanda  kwa  baba, kupitia  kazi  zake  za  mitindo , ameonyesha  nia  ya  kufika  mbali  katika  tasnia  ya  mitindo., huku  lengo  lake   likiwa  kufikia  level  za  kimataifa  kama   Naomi  Campbell. Akielezea  kuhus  safari  yake  katika tasnia  ya  mitindo,  Hope  anasema  “  Tangu  nikiwa  shule  ya  msingi, siku   zote  nilikuwa  nikitamani  sana  kuwa muimbaji, dancer  au  mwanamitindo. Lakini  kwa  kuwa  sikuwa  na  kipaji  cha  kuimba  wala  kudance,  nikaamua  kujikita  katika  mitindo “ Akaongeza  “ Nilipofika  O-Level  nikaanza  kufanya  modeling  for  fun.  Hapo  nilikuwa  bado  Tanzania. Nilipo maliza  O-Level  huko  Tanzania, nilikuja  kujiunga  na  masomo  ya  A-Level