Baadhi ya madaktari nchini Marekani, wamemuonya mwanamuziki Mariah Carey kuwa endapo hatofanya jitihada za kupunguza uzito wake, basi atakuwa katika hatari kubwa ya kupatwa na shambulio la moyo. ( Heart Attack ) Onyo hili limekuja baada ya mwimbaji huyo nguli kuripotiwa kuwa na uzito wa Pounds 263 ambazo ni sawa sawa na Kilogram 119 point 295 Kwa mujibu wa mtandao mmoja wa habari nchini Marekani, uzito wa Mariah Carey umesababishwa na ulaji mbaya wa vyakula. Iliripotiwa pia, kwenye tamasha la Caesars Palace, Mariah Carey alilazimika kubebwa kila alipokuwa akitaka kupanda au kushuka stejini na kama hiyo haitoshi alipumzika kwa muda mrefu kuliko kawaida wakati anajiandaa kuimba wimbo wake namba 19. SOURCE : MITANDAO MBALIMBALI YA HABARI NCHINI MAREKANI.