Katika miaka ya hivi karibuni idadi ya vijana wadogo wenye vipara imekuwa kubwa kuliko ilivyo kuwa hapo zamani. Miaka ya 90 kurudi nyuma ilikuwa ukimuoa mtu ana upara kichwani basi pasi na shaka yoyote mtu huyo alikuwa ni mtu mzima at least kuanzia miaka hamsini na kuendelea. Kama angekuwa kijana sana basi at least angekuwa kwenye miaka arobaini mwishoni yani anaitafuta miaka hamsini. Ilikuwa ni nadra sana kumuona kijana ana upara. Miaka hiyo ya zamani dhana ya mtu kuwa na upara ilihusishwa na uzee ndio maana kipindi hicho ulisikia watu wakiitwa Mzee Kipara nakadhalika. Ilikuwa ni nadra sana kumkuta kijana mdogo akiwa na upara. Lakini hali imekuwa tofauti sana katika miaka ya hivi karibuni. Siku hizi kumekuwa na vijana wadogo sana amb