Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2023

Nini tiba ya tatizo sugu la harufu mbaya ya kinywa

  Ipo   idadi kubwa ya watu duniani ambao wana sumbuliwa na tatizo la kutokwa na   harufu mbaya ya kinywa.   Miongoni mwao wapo ambao tatizo hilo limekuwa sugu kwa maana ya kwamba licha kuzingatia kanuni zote za usafi wa kinywa pamoja na kutumia dawa za aina mbalimbali ili waweze kujitibu tatizo lao lakini tatizo linabaki kuwa pale pale.     Hakuna tatizo linalo fedhehesha kama tatizo la kutokwa na harufu mbaya ya kinywa.   Jambo hili humkosesha mtu raha na amani na humfanya akose confidence ya kuingia katika mahusiano ya kimapenzi.   Kuna watu tatizo hili ni kubwa kiasi kwamba hata akiwa amekaa na mtu lets say kwenye meza wanazungumza basi ile harufu mbaya kutoka kinywani kwake huweza kusikika.   Je   tatizo hili husababishwa na kitu gani haswa?    1.Harufu  mbaya  ya  kinywa  husababishwa  na  aina  ya  bacteria  anayeishi  kwenye  tishu  ndogo kwenye sehemu  ya  mgongo  wa  kinywa ( Hususani  kwenye  sehemu  ya  nyuma  ya  ulimi ). Bacteria  huyu  nd

ATOA USHUHUDA JINSI URAIBU WA KUVUTA SIGARA NA POMBE KALI ULIVYO SABABISHA RAFIKI YAKE KUPATA SARATANI YA MAPAFU ( Je Kuna Tiba ya kumsaidia mraibu wa sigara na pombe kuacha kutumia tena vitu hivyo?)

    Rafiki yangu amebakiza mwezi mmoja kuishi kutokana na uraibu wa sigara na pombe kali iliyosababisha saratani ya mapafu     Habar za muda huu wana Jf. Usiku huu nimepokea taarifa zilizonishtua sana kutoka Kwa rafiki yangu (Mdogo wangu) kuhusu Afya yake. Alichoniambia mpaka sasa sijaelewa kinawezaje kumuathiri haraka hivyo kutokana na mimi nilivyokuwa nafahamu. Iko hivi, huyu dogo ni mraibu wa sigara na pombe kali. Sasa anachoniambia kutokana na matumizi yake ya vilevi hivyo kuwa makubwa amepatikana na tatizo la Saratani ya mapafu na ipo katika stage mbaya Sana, naweza kusema ya mwisho kabisa. Sikupata Nafasi ya kumuhoji mambo mengi kutokana na hali aliyokuwa nayo (Alikuwa amelewa sana leo, pia alikuwa analia Kwa uchungu sana) Hivyo muda mwingi niliutumia kumbembeleza kumfanya asijisikie vibaya zaidi. Kwa maelezo Aliyonipa anasema tatizo limeanza muda kidogo lakini wakati anakwenda Hospital lilikuwa limeshamla zaidi ya 75% hivyo Madaktari, Wamemweleza ukweli hapo al

Testimony : Nilianza kwa majaribio nikaishia kuwa teja, Story ya ukweli jinsi nilivyokuwa mtumwa wa kujichua kwa miaka 10

      Ilikuwa ni kipindi nipo darasa la sita nikiwa na miaka 12 kwenye kipindi cha sayansi mwalimu alikuja kufundisha topic ya mitindo ya maisha kama sikosei ilikuwa ni reproduction. Ni topic ambayo wengi iliwafanya wawe wasikivu kama mjuavyo hata watoro walikuwa hawaikosi, sasa katika maswali ya hapa na pale kuna jamaa akauliza swali kwamba uume ukipakwa sabuni kinatokea nini, nadhani huyo jamaa alikuwa tayari ashaanza kujichua na hilo swali kauliza kimafumbo ila kwa akili ya mwalimu mtu mzima alishajua nia ya lile swali. Mwalimu ndio akaanza kugusia mambo ya nyeto kwamba kuna wavulana huwa wanajifungia ndani wanaanza kujichezea uume kwa kuuvuta vuta, hizo sabuni ni vilainishi, wanavuta mbele na nyuma ili wasikie raha hatimae wanamwaga. Maswali yakaendelea hapo wakulungwa tukaanza kuuliza maswali hio raha inafikia utamu wa chai ya maziwa yenye sukari ? hizo sperms zinavyotoka ni hadi uamue au ni kwa hiari?, kiasi gani cha nguvu kinatumika?, n.k. mwalimu alikuwa ni mchangamfu

Kijana wa kiume alie fanya punyeto kwa muda wa miaka kumi aelezea jinsi uraibu wa kujichua uume ( punyeto ) unavyo mtesa katika maisha yake ya mahusiano

  Hakuna kitu kinawatesa   vijana   wa kiume   kwenye mahusiano kama athari zitokanazo na kufanya punyeto kwa muda mrefu.   Moja kati ya   athari kubwa kabisa   wapitazo wanaume ambao wamefanya punyeto kwa muda mrefu ni pamoja na maumbile yao ya kiume kulegea na kusinyaa kabisa na kutokuwa na uwezo wa kusimama vizuri, kutokuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa kwa muda mrefu( yani kumaliza mchezo ndani ya dakika chache sana ) uume kusimama ukiwa katika hali ya ulegevu, kutokuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa nakadhalika. Huyu hapa chini   ni   kijana   ambae   alijihusisha na   punyeto kwa muda wa miaka kumi na haya hapa ndio   masahibu   yaliyo mkuta kijana huyo. Kijana huyo ameyaelezea masahibu hayo kupitia mtandao wa kijamii wa jamii forums. Haya hapa maneno ya kijana huyu : “ Uraibu wa punyeto/kujichua kwa zaidi ya miaka kumi suluhisho lake nini na uchukua muda gani tiba”   Samahani wadau nahitaji msaada nashida ya kuwa na uume mdogo na kuwai kumwaga na kila aina ya ma

Dar, Mwanza, Kilimanjaro na Unguja Kusini yaongoza kwa wanawake wenye vitambi

  Wakati Watanzania na wadau wa masuala ya afya na lishe wakisubiri ripoti ya Utafi ti wa Afya ya Uzazi na Mtoto (THDS) na Utafi ti wa Kitaifa wa Lishe (TNNS) zote za mwaka 2022, yapo mambo makubwa matatu yanayoikabili sekta ya lishe ikiwemo uzito uliokithiri, viribatumbo au vitambi na udumavu. Kwa upande wake, Ofisa Utafiti wa Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC), Walbert Mgeni anasema kuwa katika utafiti walioufanya mwaka 2018, kulingana na kipimo cha Body Mass Index (BMI) kinacholinganisha kati ya urefu na uzito ulibaini kwamba asilimia 7.3 ya wanawake wenye umri kati ya miaka 15 hadi 49 ni wembamba au wana uzito pungufu kiwango ambacho ni cha juu ukilinganisha na mwaka 2014. Anasema asilimia 10 ya wanawake waliobainika kuwa na uzito pungufu ni kutoka Unguja Kaskazini, Pemba, Manyara, Kagera na Singida. Kwa mujibu wa TNNS 2018, asilimia 31.9 ya wanawake wana uzito uliokithiri ambayo inaonesha ongezeko kutoka asilimia 29.7 mwaka 2014. Kiribatumbo kimeongezeka kwa asilimia 20. Mg