Skip to main content

ATOA USHUHUDA JINSI URAIBU WA KUVUTA SIGARA NA POMBE KALI ULIVYO SABABISHA RAFIKI YAKE KUPATA SARATANI YA MAPAFU ( Je Kuna Tiba ya kumsaidia mraibu wa sigara na pombe kuacha kutumia tena vitu hivyo?)

 

 



Rafiki yangu amebakiza mwezi mmoja kuishi kutokana na uraibu wa sigara na pombe kali iliyosababisha saratani ya mapafu

 

 

Habar za muda huu wana Jf.

Usiku huu nimepokea taarifa zilizonishtua sana kutoka Kwa rafiki yangu (Mdogo wangu) kuhusu Afya yake.

Alichoniambia mpaka sasa sijaelewa kinawezaje kumuathiri haraka hivyo kutokana na mimi nilivyokuwa nafahamu.

Iko hivi, huyu dogo ni mraibu wa sigara na pombe kali. Sasa anachoniambia kutokana na matumizi yake ya vilevi hivyo kuwa makubwa amepatikana na tatizo la Saratani ya mapafu na ipo katika stage mbaya Sana, naweza kusema ya mwisho kabisa.

Sikupata Nafasi ya kumuhoji mambo mengi kutokana na hali aliyokuwa nayo (Alikuwa amelewa sana leo, pia alikuwa analia Kwa uchungu sana) Hivyo muda mwingi niliutumia kumbembeleza kumfanya asijisikie vibaya zaidi.

Kwa maelezo Aliyonipa anasema tatizo limeanza muda kidogo lakini wakati anakwenda Hospital lilikuwa limeshamla zaidi ya 75% hivyo Madaktari, Wamemweleza ukweli hapo alipofikia haiwezekani tena too late, hivyo kwa kipindi chote hicho Amekuwa mtu Wa kutumia sindano ili kupunguza makali Ya tatizo kumpelekea kwenye kifo.

Ameendelea kunieleza sindano anazochoma ni gharama Sana na ni kila wiki hivyo imempelekea Kuuza baadhi ya vitu vyake kwa ajili ya kuendelea na matibabu. Sasa kitu Walichomueleza hospital hizi siku za hivi karibuni ni kwamba Stage aliofikia now hata hizo sindano haziwezi msaidia. Uwezekano wa kuishi zaidi ya siku 30 kuanzia sasa labda itokee muujiza na neema za Mungu. Kutokana na nature ya tatizo.

Kumbe dogo Aliambiwa apunguze matumizi ya hivyo vitu hususani sigara ikiwezekana aache kabisa itamsaidia kwa kiasi fulani lakini yeye akawa anapiga kama kawa.

Kilichonifanya nije jukwaani Hapa, Kwanza nafahamu kama sigara zina madhara lakini chalii ni mdogo under 30, imewezekanaje zimalize mapema hivyo?

Kama jibu ni ndio, basi kuna vifo vya wetu wengi sana kutokana na matumizi ya sigara.

Kingine wataalamu wanieleze hii issue imekaaje kuhusu upande wa matibabu, pia naamini kuna watu wamewahi experience hii issue yaweza kuwa imempata rafiki, ndugu, jirani whatever..je ilikuwaje?

Dogo ndio amezidi kuchanganyikiwa anakunywa mapombe hovyo anauza mali Zake hovyo amejikatia taamaa haoni tena thamani ya haya maisha. Kilichoniuma Ananiambia ameniita kuniaga siku 😭 😭 😭 siku nikisikia amekufa basi sababu ni hiyo.

Hivyo kwa sasa Anahesabu siku na masaa kiukweli roho imeniuma. Aisee wale wa vitaji wa sigara na mapombe makali, jifunzeni kutokana na kisa hicho.

Nimepitia google kwenye chanzo fulani cha habari kinasema Watumiaji wa tumbaku kuanzia Miaka ya 2005+ imeonekana kuwa na adhari kubwa zaidi kuliko hizo za miaka ya nyuma.

Hivyo vifo vimeongezeka tena zaidi ni vijana na jinsi ya kiume. Serikali iangalie kwa makini sana hili jambo tutapoteza nguvu kazi ya taifa, wasiangalie tu kwenye kodi waangalie na maisha ya watu.

Karibu kwa mawazo, hoja ushauri. Nawasilisha🙏

 

CREDIT:  Jamii Forums.

 

KUTOKA NEEMA HERBALIST : Je zipo dawa ambazo zinaweza kumsaidia mraibu wa sigara na pombe kurejea katika hali yake ya kawaida? Yani kuacha kabisa kuvuta sigara na/au kunywa pombe ? Jibu ni NDIO zipo dawa  mbalimbali za asili zitokanazo na mimea ambazo zina uwezo wa kumfanya mraibu pombe na/au  sigara kuacha kabisa. Kazi kubwa ya dawa hizo ni ku reverse addiction . Kufahamu zaidi  kuhusu tiba hii, wasiliana na duka la Neema Herbalist kupitia simu namba 0766 53 83 84. Tunapatikana Dar Es Salaam, Ubungo nyuma ya UBUNGO PLAZA jirani na shule ya Msingi UBUNGO NATIONAL HOUSING.

Comments

Popular posts from this blog

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na...

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ...

FAIDA KUMI ZA MTI WA MKOMAMANGA

Mti   wa   Mkomamanga   ni   mti   wenye   faida   nyingi   sana   katika   afya   ya   mwanadamu. Mti   huu   una   virutubisho –afya     mbalimbali   ambavyo   ni   muhimu   katika   afya   ya   mwanadamu.   Virutubisho   hivyo   vinapatikana   kwenye   magome, majani, mbegu, maganda   ya   matunda, juisi   ya   matunda   pamoja   na kwenye   maua   ya   mti   wa   mkomamanga. Zifuatazo   ni   faida   muhimu   za   mti   wa   mkomamanga : 1.           Maganda   ya   tunda   la   mkomamanga   yakichemshwa    hutoa   juisi    ambayo   hutumika   kama   dawa   ya   kufunga   kuhara. 2.   ...