Skip to main content

Prof. Janabi: Matumizi makubwa ya chumvi ni hatari kwa afya ya moyo






Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Prof. Mohamed Janabi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) kwa ajili ya maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani tarehe 29/09/2022. Katika kuadhimisha siku hiyo wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa ALMC wanafanya kambi maalum ya siku tano ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wakazi wa mkoa wa Arusha na mikoa jirani.



Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi amewataka wananchi hususani wa mkoa wa Arusha kuacha matumizi makubwa ya chumvi inayosababisha shinikizo la juu la damu ambalo moja ya madhara yake ni kutanuka kwa moyo.

Prof. Janabi ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo ametoa wito huo leo tarehe 29/09/2022 wakati wa maadhimisho ya siku ya moyo duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Arusha Lutheran Medica Centre.

Alisema watu wengi wanapenda kutumia chumvi nyingi katika chakula hasa chumvi mbichi ambayo inaongezwa baada ya chakula kuiva, unywaji wa juisi za kusindika au kuongeza sukari pindi wanapotengeneza juice pamoja na kula kwa wingi vyakula vyenye wanga vitu ambavyo ni hatari kwa afya ya moyo.

Mkurugenzi huyo mtendaji alisema ukanda wa Arusha unawafugaji wengi na nyama inapatikana kirahisi kutokana na hali hii watu wengi wanapenda kula nyama choma ambayo asilimia kubwa ya chumvi inayotumika ni mbichi kitu ambacho kitasababisha changamoto ya afya kwa siku za usoni.

“Magonjwa ya kisukari na Shinikizo la damu yanatokana na mtindo wetu wa maisha hivyo tupunguze sana ulaji wa chumvi na matumizi makubwa ya sukari kwani asilimia 32 ya vifo vinatokana na magonjwa yasioambukiza hususani moyo na matibabu yake ni gharama kubwa”,.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) kwa ajili ya maadhimisho ya siku ya moyo duniani leo tarehe 29/09/2022. Katika kuadhimisha siku hiyo wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa ALMC wanafanya kambi maalum ya siku tano ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wakazi wa mkoa wa Arusha na mikoa jirani.


“Ili kukabiliana na magonjwa ya moyo wananchi tujitahidi kufuata mtindo bora wa maisha ikiwa ni pamoja na kuacha uvutaji wa sigara, kuacha unywaji wa pombe uliokithiri, kufanya mazoezi ikiwa ni pamoja na kutembea hatua elfu 10 kwa siku pamoja na kula vyakula bora”, alisema Prof. Janabi.

Aidha Prof. Janabi aliwataka wananchi kukata bima za Afya kwani gharama za matibabu zimekuwa zikiongezeka kadri siku zinavyokwenda lakini kama mtu atakuwa na bima ya afya itamsaidia kulipia gharama za matibabu pindi atakapoumwa.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) Elisha Twisa aliwashukuru wataalamu ya JKCI ambao wako katika hospitali hiyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi wa mkoa wa Arusha na mikoa jirani.

“Tunawashukuru wenzetu wa JKCI ambao wametuletea huduma za kibingwa za matibabu ya magonjwa ya moyo katika mkoa wetu wa Arusha, tutazidi kushirikiana nao ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma hii mara kwa mara”, alisema Twisa.

Mkurugenzi huyo mtendaji wa ALMC alisema hospital hiyo ipo mbioni kuanzisha kitengo cha matibabu ya moyo ili kuwasaidia wananchi waweze kupata huduma hiyo karibu zaidi.

Mmoja wa wananchi aliyepata huduma za upimaji na matibabu Kulwa Mayombi alisema yeye pamoja na wenzake wamefurahia kupata huduma hiyo sanjari na elimu ya afya itakayowasaidia kuondokana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza yakiwemo magonjwa ya moyo.

Katika kuadhimisha siku ya moyo dunia ambayo kauli mbiu yake ni “fanya uamuzi sahihi kuhusu moyo wako” wataalamu wa JKCI kwa kushirikiana na wenzao wa ALMC wanafanya kambi maalum ya siku tano iliyoanza tarehe 26 hadi 30 mwezi huu ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wakazi wa mkoa wa Arusha na mikoa jirani.

Credit : Mitandao  mbalimbali  ya  kijamii.

 

Kitambi, unene na uzito kupita kiasi ni miongoni mwa mambo yanayo tajwa kuwaweka watu katika hatari ya kupatwa na magonjwa ya moyo. Kufahamu  jinsi  kitambi, unene, uzito ulio zidi kinavyo tokea na jinsi kinavyo weza kudhibitiwa  kwa  kutumia dawa za mimea ya  asili, tembelea link hii  hapa  chini :
https://neemaherbalist.blogspot.com/2016/12/fahamu-jinsi-kitambi-kinavyo-patikana.html


Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA