Skip to main content

Ripoti: Zaidi ya Nusu ya Wanawake wa Dar es Salaam wana uzito uliopitiliza

 

 


Licha ya jitihada zinazofanywa na wanawake waishio mjini ikiwamo jijini Dar es Salaam, ripoti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inaonyesha idadi ya wanaoelemewa na uzito inaongezeka.

Ripoti hiyo ya utafiti wa Ufuatiliaji wa Kaya (NPS) ya mwaka 2020/21 inaonyesha asilimia 47 ya wanawake wenye umri kati ya miaka 15 hadi 49 wasio na mimba, wana uzito uliopitiliza likiwa ni ongezeko la asilimia 8.2 kutoka mwaka 2014/15.

Ripoti hiyo iliyotumia kipimo cha ulingano wa uzito na urefu (BMI) inaonyesha vigezo vya mtu kuwa na uzito uliopitiliza ni kuwa na BMI kuanzia 25 na zaidi ya 30.

Takwimu hizo zinaonyesha katika kila wanawake wawili nchini, mmoja ana uzito uliopitiliza kutokana na kutumia vyakula vyenye mafuta mengi.

Kwa wanawake wanaoishi Dar es Salaam, ripoti imewaweka katika hali ya hatari zaidi kupata magonjwa ya shinikizo la damu, kisukari na saratani kutokana na uzito uliopitiliza kwani saba katika kila 10 wana hali hiyo.

“Wanawake wenye uzito uliopitiliza mwaka 2014/15 jijini Dar es Salaam walikuwa asilimia 52.7 lakini wameongezeka hadi asilimia 64.5 mwaka 2020/21,” inasema ripoti hiyo.

Asilimia 40.3 ya wanawake wanaoishi vijijini, ripoti inasema wana uzito uliopitiliza wakilinganishwa na asilimia 60.5 ya wanawake wa mjini.

Matokeo ya utafiti huu yanalingana na ule uliofanyika India mwaka 2013 na kuchapishwa katika Journal of Family Medicine and Primary Care ulioitwa ‘lishe na shughuli za kimwili miongoni mwa wanawake katika maeneo ya mjini na vijijini kusini mwa India’ ambao ulionyesha wanawake wa vijijini hawana uzito uliozidi kutokana na kufanya shughuli za kimwili mara tatu zaidi ya wanawake wa mjini.

Anastazia Mwelu (27), mkazi wa Sinza jijini Dar es Salaam mwenye uzito wa kilo 96 anasema ameshauriwa na daktari kuacha kula vyakula vyenye mafuta na wanga kwa wingi ili kupunguza uzito.

“Nilienda hospitali daktari alinishauri vyakula ambavyo sitakiwi kutumia kwa sasa zikiwamo chipsi ambazo nahisi zimenisababishia huu mwili. Pia, nimeambiwa niache kula vyakula vya wanga na nifanye mazoezi sana,” anasema Anastazia.

Katika hali ya mashaka na kutojiamini, Christina Joseph, mkazi wa Mbezi Beach jijini humo ana wasiwasi wa kuongezeka uzito kutokana na kukaa nyumbani muda mwingi baada ya kumaliza masomo yake ya chuo kikuu.

“Naona kabisa uzito wangu unaongezeka na nakuwa mvivu kwa sababu sina shughuli za kufanya baada ya kumaliza chuo, nikiamka asubuhi ni kula, kufanya shughuli za nyumbani na kulala. Naogopa kupima uzito, nahofu nitakuwa nimeongezeka uzito,” anasema Christina.

Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake katika Hospitali ya Salaaman, Abdul Mkeyenge anasema sababu ya wanawake kuwa na uzito mkubwa ni kutokula mlo kamili kama inavyoshauriwa.



Kwa kawaida, anasema kila binadamu anatakiwa kuwa na uwiano kati ya urefu na uzito wa mwili wake yaani BMI.

“Kwa kawaida, BMI inatakiwa kuanzia 18 mpaka 29.5 kwani zaidi ya 30 inamaanisha uzito uliopitiliza. Kuna sababu nyingi za mtu kuwa na uzito uliopitiliza lakini kubwa ni kutofuatilia mlo kamili,” anasema daktari huyo.”

Kitu cha msingi kuzingatia anasema ni kuepuka vyakula vyenye mafuta na sukari kwa wingi ambavyo wanawake wengi wanavipenda zaidi.

“Mji kama Dar es Salaam unakua kwa kasi na watu hawapangi ratiba ya kula vizuri, wanapenda kula vyakula vyenye mafuta na sukari na wanakunywa pombe kupitiliza,” anasema.

Vyakula vinavyoliwa mjini, daktari huyo anasema ni vya kusindika na huwekwa kwenye friji kwa muda mrefu hivyo kupoteza ubora.

Changamoto iliyopo, Dk Mkeyenge anasema ni mafuta kwenda kurundikana kwenye mishipa ya damu hali inayochochea uzito na kuzalisha shinikizo la damu kwa wanawake na wanaume.

Anasema kuzaa hakuna uhusiano wowote na uzito uliopitiliza kwani mtoto anapotengenezwa tumboni mwili huhitaji chakula kingi lakini wengi hawali mlo kamili ila wanajaza vyenye sukari na mafuta hivyo kujikuta wananenepa kupita kiasi baada ya kujifungua.

Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake, Isaya Mhando anasema wanawake wengi huongezeka uzito baada ya kujifungua.

“Kuna sababu nyingi, mama anaweza kuongezeka uzito pindi kipato kinapoongezeka au kupungua kwa kazi alizonazo lakini wengi wanaingia kwenye tabia bwete kwa kutokufanya kazi, anatembelea gari akifika nyumbani anakaa tu kwenye kochi,” anasema.

Wanawake wengi, Dk Mhando anasema hawali vyakula vya asili na hawana elimu ya lishe bora.

“Kuna utafiti ulifanyika Kilimanjaro ulioonyesha kuna ongezeko la wanawake wenye vitambi huku kipato nacho kikiongezeka na maeneo yanayozalisha chakula ilionekana kuna watoto wana utapiamlo,” anasema Dk Mhando.

Utapiamlo, anasema huweza kujidhihirisha kwa kuwa na uzito kidogo au uliopindukia hivyo ni lazima watu wakafahamu wanapaswa kula vyakula gani na kufanya mazoezi na au kazi zinazoushughulisha mwili ikiwamo kulima.

Lishe bora

Ofisa Lishe Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC), Walbart Mgeni anasema ni muhimu kila mtu kula mlo kamili ili kusaidia umeng’enywaji na ufyonzwaji wa chakula.

Kila mlo kamili, anasema unatakiwa kuwa na makundi yote matano ya vyakula vikiwamo vya nafaka, mizizi na matunda, mbogamboga, jamii za kunde na vyenye asili ya wanyama, mafuta na sukari bila kusahau kunywa maji safi.

“Tunachosisitiza mlo utokane na makundi hayo kwani unapokula zaidi sukari na mafuta unasababisha mwili kuongezeka. Wanawake wengi wanapenda vyakula hivyo kuliko wanaume,” anasema.

Mtaalamu wa Lishe wa Hospitali ya Taaluma na Tiba Mloganzila, Theresia Thomas anasema mlo kamili unatakiwa kuwa na mchanganyiko wa mbogamboga na matunda ambavyo huongeza kinga za mwili.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Saratani wa Hospitali ya Aga Khan, Dk Harrison Chuwa anasema ulaji usiofaa husababisha saratani ya mfumo wa chakula.

Dk Chuwa anasema miaka ya hivi karibuni wanapokea wagonjwa wengi wa saratani ikilinganishwa na miaka ya nyuma kutokana na mfumo mbaya wa maisha.

“Saratani hizi nyingi zimetokana na kula vyakula vya mafuta, kunywa pombe kali na kutofanya mazoezi,” anasema Dk Chuwa.

Credit :   NBS TANZANIA/ MWANANCHI

 

Tatizo  la  kitambi  linaweza kuthibitiwa  kwa  kutumia  dawa  mbalimbali za  asili. Kufahamu  namna  tatizo la  kitambi  linavyo weza  kudhibitiwa  kwa  kutumia dawa  za  mimea  ya  asili, bonyeza  link hii  hapa chini :

 https://neemaherbalist.blogspot.com/2015/11/fahamu-jinsi-kitambi-kinavyo-patikana.html

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA