Skip to main content

Dar, Mwanza, Kilimanjaro na Unguja Kusini yaongoza kwa wanawake wenye vitambi

 





Wakati Watanzania na wadau wa masuala ya afya na lishe wakisubiri ripoti ya Utafi ti wa Afya ya Uzazi na Mtoto (THDS) na Utafi ti wa Kitaifa wa Lishe (TNNS) zote za mwaka 2022, yapo mambo makubwa matatu yanayoikabili sekta ya lishe ikiwemo uzito uliokithiri, viribatumbo au vitambi na udumavu.

Kwa upande wake, Ofisa Utafiti wa Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC), Walbert Mgeni anasema kuwa katika utafiti walioufanya mwaka 2018, kulingana na kipimo cha Body Mass Index (BMI) kinacholinganisha kati ya urefu na uzito ulibaini kwamba asilimia 7.3 ya wanawake wenye umri kati ya miaka 15 hadi 49 ni wembamba au wana uzito pungufu kiwango ambacho ni cha juu ukilinganisha na mwaka 2014.

Anasema asilimia 10 ya wanawake waliobainika kuwa na uzito pungufu ni kutoka Unguja Kaskazini, Pemba, Manyara, Kagera na Singida. Kwa mujibu wa TNNS 2018, asilimia 31.9 ya wanawake wana uzito uliokithiri ambayo inaonesha ongezeko kutoka asilimia 29.7 mwaka 2014.

Kiribatumbo kimeongezeka kwa asilimia 20. Mgeni anasema kuwa mikoa inayoongoza kwa kuwa na wanawake wenye uzito uliokithiri na viribatumbo ni Kilimanjaro, Dar es Salaam, Mwanza na Kusini Unguja (Zanzibar).

Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa lishe wa mwaka 2018 ambao ulibainisha kuwa wanawake ndio wanaoongoza kwa kuwa na viribatumbo kuliko wanaume kwani takwimu za THDS zinaonesha kuwa uzito uliokithiri umeongezeka kutoka asilimia 28 mwaka 2015 hadi asilimia 32 mwaka 2018.

Kwa upande wa kiribatumbo wanawake wanaongoza kwa kiwango cha asilimia 15 na wanaume asilimia 2.5.

Inaelezwa kuwa uzito uliokithiri ni moja ya viashiria vya ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo saratani, magonjwa ya moyo na kisukari.

Kwa upande mwingine, magonjwa hayo ya lishe yamekuwa fursa kwa wafanyabiashara wengi ambao huuza bidhaa zao kwenye mitandao ya kijamii wakieleza namna ya kupunguza tumbo na nyama uzembe hususani kwa wanawake.

Hivi sasa dawa zinazodaiwa kuondoa vitambi zinauzwa kila kona. Kama hiyo haitoshi, ‘diet’ ndio neno pendwa kwa wanawake huku wengi wao wakipata ushauri wa watu wasio wataalamu wa afya na kuwasababishia athari kedekede.

Hata hivyo, mapinduzi ya sayansi na teknolojia, kutofanya mazoezi na kutozingatia lishe bora kwa kula vyakula vyenye madini, vitamini, wanga na protini huchangia kwa kiasi kikubwa matatizo hayo.

Athari za kiuchumi pia hutajwa kusababisha ulaji usiofaa kwani huchangia upatikanaji wa vyakula vilivyoandaliwa kwa haraka, unywaji wa vimiminika vya viwandani na kutozingatia mazoezi.

Maadhimisho ya Siku ya Uzito Uliozidi na Kiribatumbo Duniani hufanyika Novemba 26, kila mwaka. Kwa mujibu wa utafiti wa Shirika la Afya Duniani (WHO) uliochapishwa Juni 2021 kuhusu unene uliopitiliza, umebaini zaidi ya watu bilioni 1.9 wenye umri kuanzia miaka 18 wana uzito uliopitiliza na watu milioni 650 wana vitambi duniani kote.

WHO ilibainisha kuwa wanawake ndio wanaongoza kwa kuwa na vitambi kuliko wanaume kwa sababu ya asili ya miili yao kuwa na uwezo mkubwa wa kuhifadhi mafuta mwilini (excess fat).

Mganga Mfawidhi wa Nsambo Health Care Polyclinic, Dk Boaz Mkumbo anasema kitambi ni sukari ya ziada iliyohifadhiwa na homoni ya insulini katika mfumo wa mafuta kwani kadri hifadhi ya sukari inavyozidi mwilini ndivyo seli za mwili zinavyodumaa kitaalamu inaitwa insulin resistance.

Dalili za usugu wa homoni hiyo ni weusi shingoni na sehemu kwenye mikunjo, kuwa na mikunjo usoni na shingoni, hali ambayo inabadilisha damu na kuonesha kuwa homoni ya insulini ipo juu.

“Kitambi hakitokani na vyakula asili vya mafuta na si sehemu ya mwili. Madhara ya kitambi hutokana na muda ambao umeishi na mafuta ya ziada,” anasema Dk Mkumbo.

Anaeleza kuwa mwili haupendi mazingira ya sukari nyingi hivyo mwili hujiendesha salama kwa wastani wa gramu tano za damu na kwamba sukari yoyote ya ziada, mwili huifadhi.

Dk Mkumbo anasema homoni ya insulini kwenye damu muda wote inatakiwa iwe chini na hupanda pale tu mtu anapokula chakula endapo mtu atakuwa na lishe duni, homoni hiyo huwa juu hali inayosababisha homoni ya Testosterone kushuka na kuongeza uzalishaji wa homoni ya kike ya Estrogen.

Pia anasema kwa kawaida kitambi kinaathiri msukumo wa damu wa moyo ambao husukuma lita 5.6 za damu kila dakika (80mls kwa kila mdundo).

“Ukiwa na kitambi unapunguza uwezo wa moyo kufanya kazi ya ziada unakuwa na mapigo mabaya ya moyo, kupumua haraka haraka, ganzi mwilini, kuvimba miguu inayobonyea na kukosa pumzi unapotembea au kupanda ngazi.

“Hiyo ni dalili mojawapo ya mwili kuzidiwa maji ya ziada kwenye damu. Mtu mwenye uzito mkubwa homoni inayohifadhi na kushikilia mafuta na inayozuia chumvi na maji visitoke, hushindwa kufanya kazi hiyo na badala yake huzidisha kumimina ndani ya damu yako,” anasema Dk Mkumbo.

“Uzito uliokithiri ni moja ya viashiria vya ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo ugonjwa wa moyo, saratani na kisukari. Lazima tuhakikishe lishe bora inazingatiwa kwa kuendelea kutoa elimu ili kupunguza magonjwa yanayoambukiza ambayo yanaligharimu taifa na familia kwa ujumla,” anasisitiza.

Mkazi wa Dar es Salaam, Princess Dominic, anasema hakuna siri kubwa ya kufuata katika maisha kama lishe bora. Anasema kuwa kufanya mazoezi ya kupunguza mwili hususani kitambi bila kuzingatia lishe ni kazi bure hivyo ili mtu aone mafanikio ya mazoezi anayofanya kwa ajili ya kupunguza uzito, anatakiwa kufuata lishe bora.

“Baada ya kujifungua niliongezeka kilo hadi kufikia 110 na hata umbo langu lilibadilika sikuvutiwa nalo, kuna wakati nilikuwa natumia mkanda wa kupunguza tumbo ili ninapokwenda kwenye matukio mbalimbali ya sherehe nionekane nimependeza. “Sikuwahi kuzingatia masuala ya lishe kwani chakula changu pendwa ni chipsi mayai, mishikaki na pepsi baridi, hali ilikuwa mbaya baada ya muda nilianza kutafuta watu wanaotangaza dawa za kupunguza mafuta na uzito kwa haraka ingawa gharama zake ni ghali lakini nilinunua ili kutimiza azma yangu ya kupunguza mwili, anaeleza Princess.

Anasema alitumia dawa nyingi ambazo nyingine zilimsababishia kuharisha kama ambavyo wataalamu hao walimuelekeza, alianza ‘diet’ lakini alishindwa kuendelea ndipo daktari alimwelekeza kufuata lishe bora ndipo alipata matokeo.

Jesika Sauli anasema kuwa tangu alipoacha kutumia vyakula vyenye wanga, mafuta mengi na sukari ame- punguza mwili wake kwa hara- ka na kwamba ataendelea kuzingatia ulaji unaofaa sambamba na kuelekeza familia yake ili kuepuka magonjwa.


Credit: Mitandao mbalimbali ya kijamii


Kitambi, unene na uzito kupita kiasi ni miongoni mwa mambo yanayo tajwa kuwaweka watu katika hatari ya kupatwa na magonjwa ya moyo. Kufahamu  jinsi  kitambi, unene, uzito ulio zidi kinavyo tokea na jinsi kinavyo weza kudhibitiwa  kwa  kutumia dawa za mimea ya  asili, tembelea link hii  hapa  chini :
https://neemaherbalist.blogspot.com/2016/12/fahamu-jinsi-kitambi-kinavyo-patikana.html

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA