Skip to main content

Kila vifo 33 kati 100 vinavyotokea nchini vinatokana na Magonjwa yasiyoambukiza



 

Imeelezwa kuwa kila vifo 33 kati ya 100 vinavyotokea nchini vinasababishwa na magonjwa hayo na robo 3 ya wananchi hawajitambui kuwa wana tatizo hilo.

Mkurugenzi Msaidizi wa Magonjwa Yasiyoambukiza Dkt. James Kiologwe amesema Mjamzito mwenye Magonjwa hayo yupo hatarini kujifungua watoto wenye uzito pungufu na kurithisha vizazi 4.

Takwimu za WHO zinaonesha Magonjwa yasiyoambukiza yanachangia 74% ya vifo vyote duniani huku 86% ya vifo vikitokea katika nchi za kipato cha chini na kati.

Magonjwa yasiyo ya kuambukiza yanasababisha vifo 33 kati ya vifo 100 ambavyo ni takriban vifo vinne katika kila vifo kumi vinavyotokea Tanzania.

Hayo yamesemwa leo Novemba 9,2022 na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kasper Mmuya katika maadhimisho ya kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza (NCD) katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Amesema magonjwa yasiyo ya kuambukizwa nchini yanachochewa na tabia bwete ya watu wengi wakiwamo vijana kutoshughulisha miili huku wengi wakiwa hawafanyi mazoezi.

"Kuna tabia imejengeka miongoni mwa vijana, wakitoka kazini badala wajishughulishe na mazoezi au kujadili mambo ya maendeleo, wanaenda baa kunywa pombe kali na wengine wanatengeneza mchanganyiko wa pombe kali wanakunywa, wanajitengenezea bomu mwilini bila kujijua,” amesema Mmuya.

Aidha, amewataka wananchi kujenga tabia ya kupima afya mara kwa mara ili kujua hali ya afya zako ikiwa ni pamoja na kuzingatia ulaji unaofaa wa vyakula.

Naye, Mkurugenzi Msaidizi wa Magonjwa Yasiyoambukiza kutoka Wizara ya Afya, Dk James Kiologwe amesema zaidi ya robo tatu ya wananchi hawajitambui kuwa wana magonjwa yasiyoyakuambukiza na kutaka elimu zaidi itolewe.

Amesema mwanamke mwenye magonjwa yasiyoambukiza yupo katika hatari zaidi ya kujifungua watoto wenye uzito pungufu na pia wapo kwenye hatari zaidi ya kurithisha vizazi vinne, cha kwanza, cha pili, cha tatu na cha nne.

Katika maadhimisho hayo yenye kaulimbiu: ‘Badili Mtindo wa Maisha Boresha Afya.’ Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ambaye ni Mratibu Wadau Sekta ya Afya, Leticia Rweyemamu, amesema asilimia 74 ya vifo vinavyotokea duniani vinasabishwa na magonjwa yasiyoambukiza.

Kwa mujibu wa Rweyemamu, mwaka 2012 kulikuwa na vifo milioni 157 kati ya hivyo, milioni 41 vilichangiwa na magonjwa yasiyoambukiza. Tangu mwaka 2016 takwimu hizo zimekuwa zikiongezeka na kufikia asilimia 74.

“Kila mwananchi akijitambua, tutafika lengo la kupunguza vifo vitokanavyo na magonjwa hayo ambayo ni mzigo mkubwa kwa familia na taifa kwa kuwa licha ya kuwaathiri wagonjwa, huchangia ongezeko la umaskini,”amesema.

Amesema mtindo usiofaa wa masiaha ukiwamo ulaji mbovu ni miongoni mwa mambo yanayoongeza kasi ya magonjwa hayo ambayo ni pamoja na kisukari, presha na moyo.

Credit : HABARI LEO


 

Kitambi, unene na uzito kupita kiasi ni miongoni mwa mambo yanayo tajwa kuwaweka watu katika hatari ya kupatwa na magonjwa ya moyo. Kufahamu  jinsi  kitambi, unene, uzito ulio zidi kinavyo tokea na jinsi kinavyo weza kudhibitiwa  kwa  kutumia dawa za mimea ya  asili, tembelea link hii  hapa  chini :
https://neemaherbalist.blogspot.com/2016/12/fahamu-jinsi-kitambi-kinavyo-patikana.html


Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA