Jina langu naitwa Mwanaidi Juma, umri wangu ni miaka 33, kabila langu ni Mmanyema wa Ujiji, Kigoma na makazi yangu kwa hapa jijini Dar Es Salaam, yapo Chanika. Ninatafuta nafasi ya kazi ya ndani ya kwenda na kurudi ( Silali kwa mwajiri). Kazi iwe ndani ya Chanika au kama nje ya Chanika basi iwe sehemu ambayo nitakuwa napanda gari tu kufika. Nina uzoefu wa miaka mitano katika kazi hii. Nimepata mafunzo maalumu kutoka NEEMA HERBALIST kuhusu jinsi ya kuandaa na kutayarisha lishe maalumu kwa watu wenye maalumu ya kiafya kama vile: Presha na Sukari, Vidonda vya Tumbo, Tatizo la ukosefu na upungufu wa nguvu za kiume, tatizo la kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake, tatizo la kitambi, tatizo la unene na uzito ulizo zidi, tatizo la kupungua mwili. Kw hivyo, ninaweza kupika mapishi na vyakula naalumu kwa watu wenye mahitaji mbalimbali ya kiafya kama vile: 1. Lishe maalumu kwa watu wenye tatizo la presha na sukari. 2. Lishe maalumu kwa watu wenye tatizo la ...