Skip to main content

MAZOEZI NA KISUKARI


MAKALA  HII  NI  MAALUMU  KWA  WANAO  SUMBULIWA  NA   TATIZO  LA  KISUKARI.

Kwa vyovyote vile utakuwa umewahi kuusikia au hata kupata uzoefu kuhusu ugonjwa wa kisukari. Eidha
kwa kuwa na ndugu, rafiki wa karibu au wewe mwenyewe kuwa mwathirika wa tatizo hili. Tatizo la
kisukari linaongezeka siku hadi siku, hususani kutokana na kuongezeka kwa tatizo la unene. Sababu
kubwa si ngumu kuifahamu, ni ulaji wa chakula unaozidi mahitaji ya miili yetu. Kwa lugha rahisi
tunaweza kusema, kula chakula bila kufanya mazoezi.
Ziko aina kuu mbili za ugonjwa wa kisukari. Ule unaotokea kwa sababu ya upungufu wa homoni ya
insulin mwilini( Type 1 diabetes), na ule unaotokana na homoni ya insulin kutokufanya kazi, japo kuwa
inatengenezwa kwa kiwango hata zaidi ya kawaida, (Type 2 diabetes). Asilimia 90 ya wagonjwa wa
kisukari wana kisukari cha aina ya pili(type 2 diabetes). Hivyo basi maelezo mengi yatakayoandikwa hapa
yatahusiana na kisukari cha aina ya pili.
Kisukari aina ya pili(Type 2 diabetes) ni nini haswa?
Ugonjwa huu huathiri uwezo wa mwili kutumia sukari, protini, mafuta na wanga. Miili yetu inahitaji
vichocheo mbali mbali ili kutengeneza nguvu na chembe hai na kutufanya tuendelee kuishi. Ugonjwa wa
kisukari huaribu uwezo wa mwili kufanya kazi wakati wa kawaida na hata wakati wa mazoezi.
Katika hali ya kawaida miili yetu hubadilisha sukari na wanga na kuwa glukozi au sukari kwa lugha ya
kawaida, ambayo hutumika mwilini kutengeneza nguvu zinazotuwezesha kuishi na kufanya shughuli za
kila siku. Glukozi husafirishwa katika damu na kupelekwa katika misuli, sehemu ambako kiasi kikubwa
cha glukozi hutumika kutengeneza nguvu na joto. Insulin, homoni itengenezwayo na kongosho,
inahitajika kuwezesha glukozi kuchukuliwa na misuli. Kwa maana hiyo basi, ili glukozi iweze kutumika
kutengeneza nguvu na joto, homoni inayoitwa insulini inatakiwa kuwepo. Glukozi ikishaingia kwenye
misuli, inatumika kutengeneza nguvu na joto au kutunzwa kwa matumizi ya baadaye.
Katika aina hii ya kisukari, ukikumbuka hapo awali tuligusia kwamba, homoni ya insulin inatengenezwa
lakini kutokana na sababu fulani(ambazo tutakuja kuziongelea siku nyingine) inashindwa kufanya
kazi.(Kumbuka ktk kisukari cha aina ya kwanza, uwezo wa kongosho kutengeneza insulin unakuwa
mdogo, hivyo kuathiri kiwango cha insulin inayotengenezwa). Kitendo cha insulini kutokufanya kazi licha
ya kutengenezwa kwa kiwango cha kawaida na wakati mwingine kiwango cha juu, kinatokana na misuli
kuwa sugu kwa insulin.Tatizo la mwili kuwa sugu kwa insulin linajulikana kitaalamu kama insulin
resistance. Kinachotokea ni kushindikana kwa sukari kuingia katika misuli hivyo kubaki katika damu. Hii
husababisha sukari kuwa nyingi zaidi ya kawaida katika damu.
Sukari kuwa nyingi katika damu kwa muda mrefu, kunaweza kusababisha magonjwa ya moyo, kufeli kwa
figo , upofu na matatizo ya mishipa ya fahamu.
Tofauti na aina ya kwanza ya kisukari, ambacho husababishwa na matatizo yanayouwa chembehai
zinazotengeneza insulin kwenye kongosho, ugonjwa wa kisukari cha aina ya pili unauhusiano mkubwa na
mifumo ya maisha hususani lishe na mazoezi. Watu wenye uwezekano mkubwa wa kupata tatizo hili
wana historia ya ugonjwa huu katika familia zao, na pia mara nyingi wanakuwa na magonjwa ya shinikizo
la damu na moyo. Mara nyingi ugonjwa huu huwapata watu wenye maisha ya kibwanyenye, ambayo
huwafanya kula chakula kingi zaidi ya mazoezi. Wengi wao wanakuwa ni wanene na wenye mafuta
mengi mwilini.
Kinachotumika kuzuia ugonjwa huu wa kisukari aina pili, ndicho kinchotumika kuzuia usilete madhara
makubwa kama magonjwa ya moyo na figo. Na si kitu kingine bali mazoezi na lishe bora.
Mazoezi yanaweza saidia
Matokeo ya tafiti chungu nzima yameyapa mazoezi kipau mbele katika kuzuia, na kutibu ugonjwa wa
kisukari aina pili, kwa sababu mazoezi yanauwezo wa kupunguza usugu wa insulin unaosababisha
homoni hii isifanye kazi. Kufuatia mazoezi ya mara kwa mara, chembe hai za mwili zinaweza kutumia
insulin kuchukua sukari kutoka kwenye damu, kuitumia na hivyo kuipunguza.
Mazoezi pia yanaweza kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo kwa kupunguza kiasi cha
mafuta mwilini na shinikizo la damu. Kwa kila kilo tano mtu mwenye kisukari anazopoteza, anapunguza
usugu wa insulin kwa asilimia ishirini.
Ushauri wa mazoezi
Kama unakisukari aina ya pili, unashauriwa kufanya mazoezi yafuatayo
1. Mazoezi yanayoufanyisha kazi mfumo wa damu na moyo(cardiovascular exercise):
Weka lengo la kufanya mazoezi ya wastani, kama vile kutembea, na mazoezi mengine
yasiyotumia nguvu nyingi kama vile kuendesha baiskeli na kuogelea, angalau mara tatu mpaka
nne kwa wiki. Kumbuka, kufanya mazoezi ya namna hii kila siku kunaleta matokeo mazuri zaidi.
2. Mazoezi ya kunyanyua au kusukuma vitu vizito(Resistance exercise):
Watu wengi hukosa kufanya mazoezi haya, kwa kudhani kwamba ni kwa ajili ya wabeba vyuma
na wapiganaji tu. Mazoezi haya ni muhimu sana, na siku zijazo nitaelezea kwa undani umuhimu
wa mazoezi haya. Weka lengo la kufanya mazoezi ya kunyanyua au kusukuma vitu vyenye uzito
wa wastani angalau mara mbili kwa wiki. Akikisha unafanyisha kazi misuli yote muhimu ya mwili
wako. Fanya walau marudio kumi mpaka kumi na tano kwa kila aina ya msuli.
3. Mazoezi ya kulainisha viungo(flexibility exercises):
Angalau mara mbili au tatu kwa wiki fanya mazoezi ya kunyoosha viungo muhimu vya mwili ili
kulainisha viungo na misuli. Fanya kwa angalau dakika kumi na tano mpaka thelathini, mara
mbili mpaka nne kwa kipindi.
Undani zaidi kuhusu mazoezi haya, utaelezewa katika makala zifuatazo. Makala hii inagusia aina
ya mazoezi tunayotakiwa kufanya ili kupunguza uzio na sukari mwilini.
Niandikie kwa maoni na maswali,

MAKALA  HAYA  YANATOKA :  WWW.AFYAANDFITNESSTV.COM 

Comments

  1. This comment has been removed by a blog administrator.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA