Skip to main content

KWANINI BAADHI YA WATU WANA UZITO MDOGO KUPITA KIASI ? ( Kukonda na kudhoofu mwili )






Kuna  idadi  kubwa  ya  watu  ambao wana  kabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  uzito  mdogo kupita  kiasi. 
Kwa  mujibu  wa   tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  ni  jambo  linalo weza  kuhatarisha  afya  ya  mhusika.




Kama  ilivyo  kwa  suala  la  kuwa  na  uzito  mkubwa  kupita  kiasi,  suala  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  pia  lina  madhara  mengi  katika  afya  ya  binadamu.

MADHARA   YA KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI  (  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, yafuatayo  ni  madhara  ya  kiafya  yanayo  weza  kumpata  mtu  mwenye  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi.

1.    Kupungua  na  kudhoofika  kwa  kinga  ya  mwili
2.    Kuwa  katika hatari  ya  kushambuliwa  na  magonjwa  ya  mifupa  kwa  sababu  mwili hushindwa  kupokea  na  kutengeneza  virutubisho  muhimu  vinavyo hitajika  katika  kuimarisha  afya  ya  mifupa
3.    Kuwa na  nywele  zisizo  na  afya  (  Kinyonyoki)
4.    Kuwa  na ngozi  isiyo  na  afya
5.    Kuugua  mara  kwa  mara  kutokana  na kuwa  na  kinga  dhoofu  ya  mwili.
6.    Watu  wenye  uzito  mdogo  kupita  kiasi  huwachukua  muda  mrefu  kupona  hata  magonjwa  ya  kawaida  ambayo  hupona  ndani ya  muda  mfupi, kwa  mfano  anaweza  akaugua  mafua  ya  kawaida  kwa  muda  wa wiki  nzima  au  Zaidi.
7.    Kujisikia  uchovu  muda  mwingi
8.    Kupungukiwa  damu  ambako  huweza  kusababisha hali   kama  vile  kizungu  zungu na  maumivu  ya  kichwa  ya  mara  kwa  mara.
9.    Kwa  wanawake , tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi  linaweza  kuathiri  mpangilio  wa  hedhi  ambao  unaweza  kupelekea  matatizo  katika  uzazi.
10.                        Na  kwa  mwanamke  mjamzito  mwenye  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi, anaweza  kupatwa  na  tatizo la  kujifungua  kabla  ya wakati  yani  kabla  ya  wiki  37.
11.                       Tatizo  la  uzito mdogo  kupita  kiasi  huathiri  ukuaji  wa  watoto.  Watoto  wadogo  wanahitaji  kuwa  na  virutubisho  vya  kutosha  ili  waweze  kukua  na  kuongezeka  na kuwa  na  mifupa  yenye  afya.  Ukosefu  wa  vitu  hivyo  maana  yake  ni  kwamba  mtoto  husika  hatoweza  kukua  na  kuongezeka  vizuri .  Vilevile  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi  linaweza  kusababisha  tatizo  la  mifupa  kwa watoto  jambo  ambalo  ni  hatari kwa  mustakabali  wa  afya  za  watoto  husika.
12.                       Tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi huathiri  mchakato  wa  uponyaji  kwa  mtu  mwenye  tatizo  hilo  ambae  anatumia  dawa  kwa  ajili  ya  kutibu  magonjwa  na  matatizo  mbalimbali  ya  kiafya.  Kwa  mfano  mtu mwenye  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi  akipata  tatizo  la  kiafya  kama  vile vidonda  vya tumbo, halafu  akaanza  kutumia  dawa  kwa  ajili  ya  kutibu  tatizo  la  vidonda , itamchukua  muda  mrefu  kupata  nafuu  ya  tatizo  lake  kuliko  mtu  asie  na  tatizo  la  uzito mdogo  kupita  kiasi  na  hii  ni  kwa  sababu  tatizo  la  uzito mdogo kupita  kiasi  huathiri kinga  na ufanisi  wa   mwili.


CHANZO   CHA   TATIZO   LA   KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI
( KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, zifuatazo  ni  baadhi  ya  sababu  kuu  za  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi ( Kukonda  na  kudhoofu  mwili )

1.    Kuugua  magonjwa  na  matatizo  mbalimbali  ya  kiafya  kama  vile  vidonda  vya  tumbo,presha   na kisukari.
2.    Msongo  wa  mawazo.
3.    Kujinyima  kula  ( Kufanya  diet  ngumu )  au  kukosa  hamu  ya  kula  kwa  muda  mrefu.  Kukosa  hamu ya  kula  kunaweza  kuwa  kumesababishwa  na  eidha  kuugua  magonjwa  na matatizo  mbali  mbali  ya  kiafya  au  kupatwa  na  tatizo  la  msongo wa  mawazo.



SULUHISHO   LA  TATIZO  LA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI
( KUKONDA NA  KUDHOOFU  MWILI )
Unaweza  kumaliza  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  kwa  kuzingatia  kula  mlo  kamili  (  Balanced  Diet ) au  kwa  kutumia  DAWA  ZA  ASILI  ambazo  ni  maalumu  kwa  ajili  ya  kumaliza  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi (  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )
DAWA  YA  ASILI INAYO  MALIZA  TATIZO  LA  KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI
( TATIZO  LA  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )

Ipo  DAWA –LISHE  YA ASILI  ambayo  INATIBU  na  KUMALIZA  kabisa  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  ambalo  linaenda  sambamba  na  kukonda  na  kudhoofu  mwili.  Dawa  hii  ni  ya asili  kabisa  isiyo  na  kemikali  yoyote  ya  viwandani  na  inayo  saidia  kutibu  na kumaliza tatizo  hili  na  kuurudisha  mwili  katika  afya  yake  ya  awali  ndani  ya  siku  thelathini.

JINSI  YA  KUPATA DAWA  HII:  Jinsi  ya  kupata dawa  hii, fika  katika duka  la  kuuza  dawa  za  asili  la  NEEMA  HERBALIST.  Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM   nyuma  ya  JENGO  LA  UBUNGO  PLAZA  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Wasiliana  nasi  kupitia  simu  namba  0693  -  005  189.
Na  kwa  taarifa  Zaidi  kuhusu  huduma  zetu  nyingine, tutembelee  kupitia  tovuti  yetu :


Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA