Skip to main content

UHUSIANO KATI YA KITAMBI NA UKOSEFU WA NGUVU ZA KIUME

 

 

 

 

 

 

UHUSIANO  KATI  YA  KITAMBI  NA  TATIZO  LA  UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME 

Kuna andiko  linasema   “  ASIYE  FANYA  KAZI  NA  ASILE “   Msingi  wa  andiko  hili  ni  kupromote  spirit  ya  kujishughulisha  na  ku discourage  spirit  ya uvivu “iddleness”  katika  jamii.  

Hata  hivyo  andiko  hilo  linaweza  kuwa  na  maana  nyingine  ya  ziada.  Maana  hii  ya  ziada  ni  tafsiri  yangu  binafsi  kulingana  na  muktadha  wa  makala hii  ya leo. Maana  hii  ya ziada   ndio  msingi  wa  mada yetu  hii  ya  leo.

Kama  nilivyo  dokeza  hapo  juu,  andiko  asiye  fanya  kazi  na  asile  linaweza  kuwa  na  maana  nyingine  ya  ziada  ambayo  kimsingi  haitofautiani  sana  na  maana ya  msingi  ya  andiko  lenyewe.

 

 Maana  hii  inaweza  kuwa  “  ASIYE  USHUGHULISHA  MWILI  WAKE  NA  ASILE CHAKULA “  kwa  sababu  mtu  akila  chakula  bila  kuushughulisha  mwili  wake  chakula  hicho  kitaenda  kubadilika  na  kuwa  sumu  ambayo  itaenda  kumdhuru  mtu  huyo, madhara  yanayo weza kuyaweka  maisha  ya  mtu  huyo  hatarini. 

 Ni  nani  asie  jua  kwamba   kutofanya  mazoezi  ya  mwili  ni  moja  kati  ya  vyanzo  vikuu  vya  matatizo  mbalimbali  ya  kiafya  kama  vile   kuwa  na  kiasi  kikubwa  cha  mafuta  yasiyo  faa  kwenye  damu “ kolestrol ”  au  kuwa  na  kiwango  kikubwa  cha  sukari  kwenye  damu.

 Ni  nani  asie  fahamu  kwamba  kutofanya  mazoezi ya  mwili  ni  moja  kati  ya  vyanzo  vikuu  vya  tatizo  la  kitambi, tatizo  la  kuwa  na  unene  ulio pitiliza  ama  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mkubwa  kupita  kiasi ?

Ni nani asie  jua  kuwa  moja  kati  ya  mambo  yanayo  weza  kumuweka  mtu  katika  hatari  ya  kupatwa  na  magonjwa  ya  moyo  ni  tabia  ya  kutofanya  mazoezi  ya  mwili  “ physical  exercises “?

Ndio  maanatukaambiwa  asiye  fanya  kazi  na  asile.  Kazi  inayo  zungumziwa  hapa  kwa  tafsiri  yangu (BINAFSI )  ya  pili,  ni  shughuli  yoyote  ambayo  inaushughulisha  mwili  kiasi  cha  kuufanya  mwili  utokwe  na  jasho  jingi. 

 

Ndio  maana  wataalamu  wa  afya  duniani  kote  wanashauri  kwamba  binadamu  anatakiwa  kufanya  mazoezi  ya  mwili  wake “ physical  exercises “ angalau  mara  mbili  au  tatu  kwa  wiki.  

 

Kama  ilivyo  kula  chakula, kufanya  mazoezi  ya  mwili  ni  jambo la  lazima.  Kila  mtu  anatakiwa  kufanya  mazoezi  ya  mwili  wake.    Hivyo  ndivyo  Mwenyezi  Mungu  alivyo  u  design  mwili  wa  mwanadamu. 

 

Kwa  jinsi  Mwenyezi  Mungu  alivyo  u  design  mwili  wa  mwanadamu  ni  lazima  mwanadamu  awe  ana  ushughulisha  mwili  wake  kila  siku  ili  mwanadamu  huyo  awe  na  uhakika  wa  kuwa  na  afya  njema  na  kuendelea  kuwa na  afya  njema. 

 

Tatizo  ni  kwamba  watu  wengi  wanapo  kuwa wakisikia  kuhusu  ishu ya  kufanya  mazoezi, mawazo  yao  huwapeleka  kwenye  kitu  kama   mazoezi  ya  kwenda  gym  kila  siku,  au  kucheza  mpira  au  kukimbia  umbali  mrefu  au  kuruka  kamba , au  kupiga  push  up  nyingi  na  mazoezi  yanayo  fanana  na  hayo.

 

Mwisho  wa  siku  watu  hawa  hukata  tama  hata  kabla  ya  kuanza  mazoezi  hayo  pengine  kutokana  na  ugumu  wa  ratiba  ya  mazoezi  (  Mtu  anashindwa  kubalance  muda  wa  kwenda  kazini  na  muda  wa  kwenda  gym )   

Mfano mtu  anaishi  Tegeta  anafanya  kazi  Posta, gym  ipo  Mlimani  City  au  Upanga  au  Masaki.  Ofisini  anaingia  saa  mbili  anatoka  saa  kumi,   muda  wa  gym  ni  kuanzia  saa  kumi  kamili jioni.

Mwisho  wa  siku  mhusika  hata  kama  ana  nia  ya  kwenda  gym  anajikuta  anashindwa  kutokana  na  muingiliano  kati  ya  muda  wa  kuingia  ofisini, muda  wa  kwenda  gym  na  issue  ya  geographical  location.

Aliwahi  kusema  Mchekeshaji  kutoka  Uganda  aitwane  Kansiime  kwamba  “   Three  days  after  I started  going  to  the  gym, instead  of  losing  weight, I lost  morale “  akimaanisha  kwamba “  Siku  tatu  baada  ya  kuanza  kwenda  gym, badala  ya  kupoteza/kupunguza  uzito, nikapoteza  ari  ya  kufanya  mazoezi.   A lot  of  people  can relate  with  what  Kansiime  has  just joked.

Sasa  basi  ninapo sema  kwamba  Mwenyezi  Mungu  alivyo  u design  mwili  wa  mwanadamu  ali  udesign  katika  jinsi na  namna  ya  kwamba  ili  mwanadamu  awe  na  uhakika  wa  kuwa  na  afya  njema  na  kuendelea  kuwa  na  afya  njema  ni  lazima  mwanadamu  huyo  awe  anafanya  mazoezi,  simaanishi   kwamba  mazoezi  hayo  ni  mazoezi  ya  gym, kukimbia, kucheza  mpira, kuogelea, kupiga  push  up, nakadhalika .

Isipokuwa Mazoezi  ninayo  yazungumzia  hapa ni    ni  MAZOEZI  YA  KUTEMBEA.  Tafiti  za  kisayansi  duniani  kote  zime  thibitisha   kwamba  mazoezi  ya  kutembea  ndio  mazoezi  bora  kuliko  mazoezi yoyote  yale  duniani. 

Ndio  mazoezi  yenye  faida  nyingi  katika  afya  ya  mwanadamu  pengine  kuliko  mazoezi  mengine  yoyote  duniani. 

 Ninapo  andika  maneno  haya  simaanishi  kwamba   kwenda  gym, kukimbia, kucheza  mpira , kupiga  push  up  nakadhalika  ni  kitu  kibaya  la  hasha, wewe  unae  weza  kwenda  gym  endelea  kwenda  gym, wewe  unae weza  kufanya  mazoezi  ya  kukimbia, kuruka  kamba, kupiga  push  up, kuogelea  nakadhalika  endelea  kufanya  mazoezi  yako  kwa  kadri  utakavyo  ona  inafaa. 

 

Hapa  ninazungumza  na wewe  ambae  hauwezi  kwenda  gym,  hauwezi  kuogelea , hauwezi  kupiga  push  up, hauwezi  kufanya  mazoezi  ya  kukimbia  umbali  mrefu  nakadhalika   kwamba  usiwe  na  wasi  wasi  kabisa  kwa  sababu  unaweza  kupata  faida  nyingi  na  kubwa  sana  kwa  kufanya  mazoezi  ya  kutembea.

Bila  shaka  mazoezi  ya  kutembea  ndio  mazoezi  yaliyo  kusudiwa  na  Mwenyezi  Mungu  kwa  sababu  ni  mazoezi  yanayo  weza  kufanywa  na  kila  mwanadamu  na  ni  mazoezi  ya  lazima  kwa  sababu  Mwenyezi  Mungu  kabla  hajamuumba  mwanadamu  alijua  kwamba  mwanadamu  atahitaji  kutembea  kila  siku  ndio  maana  akayafanya  mazoezi ya  kutembea  kuwa  yenye  faida  nyingi kwenye  afya  ya  mwanadamu.

 

RIPOTI  ZA  KITAALAMU  DUNIANI  ZIMETHIBITISHA  KWAMBA, KWENYE  NYAYO  ZA  MIGUU  YA  MWANADAMU  KUNA  POINTS  AMBAZO  ZINA  CONNECT  NYAYO  NA  OGANI  MUHIMU  KWENYE  MWILI WA  BINADAMU  KAMA  VILE  MOYO.  NAAM  KWENYE  NYAYO  ZAKO  KUNA  POINT  AMBAZO  ZINA  CONNECTION   YA MOJA  KWA  MOJA  NA  MOYO.  MOYO  NDIO OGANI  MUHIMU  KULIKO  ZOTE  KATIKA  MWILI  WA  BINADAMU.  UNAPOKUWA  UNATEMBEA,  KUPITIA  FRICTION  AMA  MSUGUANO  AMA  MGUSANO  KATI  YA  MIGUU  YAKO NA ARDHI,  FRICTION  HIYO  AU  MSUGUANO  HUO  UNA IMARISHA MISHIPA  NA  MISULI  YA  MOYO  NA  KUUFANYA  MOYO  WAKO  KUWA  IMARA  ZAIDI. 

Yaani  unapokuwa  unatembea  kwa  sababu  kwenye   nyayo  za  miguu  yako  kuna  points  ambazo  zina  connection  na  moyo  wako,  ile  friction  kati  ya  point  hizo  kwenye  miguu  yako  na ardhi  inasaidia  kustrengthen  ama  kuimarisha  misuli  ya  moyo.  Ndio  maana  wanasayansi  duniani  wanayataja mazoezi  ya  kutembea  kama  moja  kati  mambo  muhimu  sana  katika  afya  ya  moyo wa  mwanadamu.

Kadri  unafanya  mazoezi  ya  kutembea kwa  muda  mrefu  ndivyo  una  vyo  uimarisha  hata  moyo  wako.  Mbali  na  kuwa  na  point  kwenye  nyayo  za  miguu  yako  ambazo  zina  connection  ya  moja  kwa  moja  na  moyo, mazoezi  ya  kutembea  husaidia  pia  kuunguza  mafuta  yasiyo faa   pamoja  na  sumu  mbalimbali  kwenye  mishipa  ya  damu.  Mafuta  yasiyo  faa  yaliyopo  kwenye  mishipa  ya  damu  yasipo shughuliwa  yanaweza kuleta  madhara  makubwa  ya  kiafya  kama  vile  shinikizo  la  juu  la  damu  ambalo  mwisho wa  siku  hu uathiri  moyo pia.

Hivyo  mbali  na  uwepo  w  connection  kati  ya  nyayo za  miguu  ya  mishipa  ya  moyo, mazoezi  ya  kutembea  husaidia  kuunguza  mafuta  yasiyo  kwenye  damu  ambayo  automatically  jambo  hili  huenda  kuunufaisha  moyo.

Hiyo  connection  kwenye nyayo  za  miguu  kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu  haipo  kati  ya  nyayo  za  miguu  na  moyo  bali  ipo pia  baina  ya  nyayo  za  miguu  na  ogani  nyinginezo  muhimu  kwenye  mwili wa  binadamu .Nitaziandikia  makala  siku  za  mbeleni  panapo  uzima.

So  ninaposema  kwamba  Mwenyezi  Mungu  alivyo  udesign  mwili  wa  mwanadamu  ame udesign  katika   namna  ambayo  ili  mwanadamu  huyo  aendelee  ku survive  akiwa  na  afya  njema  ni  lazima  awe  anafanya  mazoezi  hicho  hapo  ndicho  ninacho  kimaanisha, na  mazoezi  ninayo  yanzungumzia  hapa  ni  mazoezi  ya  asili  kabisa  ambayo  ni  kutembea kwa miguu  yako miwili.

 

JE! MAZOEZI  YA  KUTEMBEA  YAFINYIKE  KWA  KIWANGO GANI  NA  KWA  MUDA  GANI ?

Kwanza  kabisa  hutakiwi  hata  kuyaita  mazoezi  ya  kutembea, kwa  sababu  kutembea  ni  hitaji  la  msingi  kabisa  kwa  mwanadamu  yoyote  Yule  kama  ilivyo  kwa  mahitaji  mengineyo  kama  vile  kunywa  maji  nakadhalika.

So  unacho  takiwa  kufanya  ni  kulichukulia  suala  la  kutembea  umbali mrefu kama  jambo  la  lazima  katika  maisha  yako.  Ulifanye  kuwa sehemu  ya  maisha  yako  na  wala usi  chukulie  kama  unafanya  mazoezi.  Nasema  hivi  kwa  sababu  uzoefu  unaonyesha  kwamba  watu  wengi wanao  jiwekea  malengo  ya  kufanya  mazoezi  huwa  hawatimizi  malengo  yao  na sababu  ni  kwamba  watu  wengi  huwa  hawapendezwi  na  idea  kwamba wanacho kifanya  ni  mazoezi. Kwa  mfano  tuchukulie  kusimama  kwa  muda  mrefu  ingekuwa ni mazoezi, ukimwambia  mtu  asimame  juani  kwa  muda  wa dakika  ishirini  mfululilo linaweza  kuwa  zoezi  gumu  sana  kwake, lakini  mtu  huyo  huyo anaweza  kutazama  mechi  ya  Simba  na  Yanga  akiwa  amesimama  kwa muda  wa  dakika  tisini  bila  wasiwasi  wowote.  Kilicho kwenye  akili  ya  mtu  huyu  ni kwamba  anatazama  mpira na  sio  kwamba  amesimama  juani  kwa  muda  wa dakika  tisini. 

Vivyo  hivyo  kwako  wewe  unaetaka  kuanza  kufanya  zoezi  hili  la  kutembea  kwa  miguu.  Chukulia  kwamba  umebadilisha  ama  una  badilisha  mfumo  wa  maisha  yako.  Badala  ya  kuwa  unatumia  muda  wako  mwingi  kutumia  usafiri  wa  gari  kutoka  point  moja  kwenda  nyingine  basi  wewe  uwe  unatumia  miguu  yako  mwenyewe.  Gari  upande  tu  pale unapokuwa  na  dharula.

 

Ama  kwa kiwango  cha  kutembea  na  jinsi  ya  kutembea, wataalamu  wanashauri  uwe  unatembea  kwa  umbali  mrefu  na  uwe  unatembea  haraka  haraka.

Kwa  wewe  ambae  hujatembea  umbali mrefu  kwa muda  mrefu  (  kwa  sababu  muda  mwingi  unatumia  usafiri wa  gari )  mwanzoni  inaweza  kukuwia  vigumu kidogo  kwa  sababu  hujazoea, lakini  amini  ninacho  kuambia  jambo  hilo  litakuwa  la  muda  mfupi sana  kwani  baada  ya  kama wiki  moja  hivi  utazoea  kabisa  na  usafiri  wako  mkuu  utakuwa  miguu.  Gari  utakuwa  unatumia  pale  unapo  kuwa  una  dharula  au  unapo  kuwa  unawahi  mahali  kama  vile  kwenda  kazini  nakadhalika.  Tofauti  na  hapo  usafiri  wako utakuwa  ni  miguu.  Ni mazoezi  ambayo  uyatapenda  sana  kwa  sababu  utaona  mabadiliko  makubwa  sana  kwenye  mwili  wako  na  hutopenda  urudi  tena  kule  ulipo  kuwa  kabla ya  kuanza  kufanya  mazoezi  haya.  Kuna  watu  wamekuwa  addicted  na  mazoezi  ya  kutembea  kiasi  kwamba  safari  zote  wanazo  zifanya  katika  mizunguko  yao  ya  kila  siku  wao  hutembea  tu. 

Kuna  watu  wanaishi   Makumbusho  wanafanya  shughuli  zao  posta  na  kila  siku  wanaenda  kwa  kutembea  na  kurudi  wanarudi  kwa  kutembea.  Shuhuda  ninazo  nyingi  sana, katika  makala  zangu  zinazo  kuja  nitakuwa  nina  andika  kuhusu  shuhuda  za  watu  mbalimbali  ambao   wamechagua  mazoezi ya  kutembea  kuwa  sehemu  ya  maisha  yao  pamoja  na  faida  kubwa  katika  afya  zao  ambazo  wamezipata  kwa  mazoezi  ya  kutembea.

 

UHUSIANO  KATI  YA  TATIZO  LA  KITAMBI, UNENE &  UZITO  ULIO ZIDI  NA  TATIZO  LA  UKOSEFU  NA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

·          Kuna  uhusiano  mkubwa  sana  kati  ya  tatizo  la  kiriba  tumbo (  kitambi )  na  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume

·         Kuna  uhusiano  mkubwa  sana  kati  ya  tatizo  la  kuwa  na  unene  ulio pitiliza na  tatizo  la ukosefu  wa  nguvu  za  kiume

·         Kuna  uhusiano  mkubwa  sana kati  ya  tatizo  la  kuwa  na  uzito mkubwa  kupita  kawaida  na  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume

·         Kuwa  na  kitambi, unene  ulio pitiliza  na  uzito  mkubwa  kupita  kiasi   tafsiri  yake ni  kwamba  mwili  mwako  unakupa  taarifa  kwamba  kuna  kitu  hakipo  sawa  ndani  yako.   

·         Mwili  wako  unakupa  taarifa  kwamba  una  kiwango  kikubwa  cha  mafuta  yasiyo faa ( lehemu/kolestrol)  kwenye  damu  yako.

·         Mwili  wako  unakupa  taarifa  kwamba  una  kiwango  kikubwa  cha sukari  kwenye  damu  yako.

·         Mwili  wako  unakupa  taarifa  kwamba  baadhi  ya  ogani  muhimu  ndani  ya  mwili  wako  zinaogelea  kwenye  mafuta yasiyo  faa.

·         Mwili  wako  unakupa  taarifa  kwamba  moyo  wako  umelemewa  na  kazi  ya  kusukuma  damu, kwa  sababu  una  kiwango  kikubwa  sana  cha  mafuta  kwenye  damu, ambacho  kimeifanya  damu yako  kuwa  nzito kupita  kawaida, uzito  ambao  misuli  ya  moyo  wako  haiwezi kuustahimili, kwa  sababu    moyo  umekuwa  desgined  kusukuma  damu  ambayo  haina  kiwango  kikubwa  cha  mafuta , sasa  kwa  sababu  una  kiwango kikubwa cha  mafuta  kwenye  damu  basi  maana yake ni  kwamba  moyo  unafanya  kazi  isivyo  kawaida,  unatumia nguvu  nyingi  kusukuma  damu, jambo  ambalo  ni  hatari  sana  kwa  afya  yako  kwa  sababu  huathiri  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  moyo  wako na  kukuweka  katika  hatari  ya  kupatwa  na  magonjwa  ya  moyo.   Ndio  maana  wewe  mwenye  tatizo  la  kitambi, unene  ulio pitiliza  kiasi  au  uzito  mkubwa  kupita  kiasi  ukijaribu  kukimbia  kwa  nguvu  unachoka  haraka  na  mapigo  ya  moyo  yanaenda  kasi sana  na endapo  utajilazimisha sana  unaweza  kupatwa na  shambulio  la  moyo, kwa  sababu  moyo  wako  hauna  uwezo wa  kusukuma damu  kwa  kasi kwa  sababu  damu  yako  ina  mafuta  mengi sasa  unapo kimbia  una  ulazimisha  moyo  wako  kusukuma  damu yenye mafuta  mengi  kwa  haraka kinyume  na  uwezo  wa  mishipa ya moyo  wako katika  kusukuma  damu.

·         Mwili  wako  una  kutahadharisha  kuhusu  hatari  inayo  weza  kutokea  mbele  yako  endapo hauta  chukua  hatua  za  haraka  kukabiliana  ama  kudhibiti  tatizo  hilo.

·         Mwili  wako  unakupa  taarifa  kwamba  upo  katika  hatari  ya  kukabiliwa  na  magonjwa  hatarishi  kama  vile  presha, kiharusi, na  magonjwa  mengineyo  ya  moyo.

·         Kwa  hiyo  mwili  wako  unakutaka  kuchukua  hatua  za  haraka  kukabiliana  na  hatari  hiyo  kabla  haijawa  kubwa  zaidi

JINSI  KITAMBI  KINAVYO  PATIKANA

Kitambi  ni  ile  hali  ya  tumbo  kuwa kubwa  na  kuchomoza  kwa  mbele  na  wakati mwingine  kufikia  hatua  ya  kunin’ginia.

 

JINSI  KITAMBI  KINAVYO  PATIKANA

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, mwili wa binadamu una seli kati  ya bilioni 50  hadi 200 za mafuta zilizogawanyika katika  sehemu  mbalimbali  za  mwili wa binadamu.

 Kwa wanawake  seli hizo  zipo sana katika maeneo ya matiti, kwenye  nyonga, kiunoni na kwenye makalio.

 

Kwa upande  wa  wanaume seli  hizo zinapatikana  sana kwenye kifua, tumboni na kwenye makalio pia.

Mafuta ya tumbo yanayofanya kitambi hukusanywa kwa njia kuu mbili:

i.                    Njia  ya kwanza ni mafuta kutoka kwenye tishu zilizo chini ya ngozi

ii.                  Na  njia  ya pili ni kutoka kwenye ogani za ndani kama moyo, kongosho n.k

 

SABABU ZA KUPATA KITAMBI

 

Sababu kubwa ya kitambi ni kukosekana ulingano wa nguvu(kalori) katika  mwili  wa  mwanadamu, hali  inayo  sababishwa  na  mtu  kula vyakula vinavyotia nguvu sana kuliko jinsi anavyoweza kutumia na kutoa kama taka mwili.

 

VYAKULA  VINAVYO  CHANGIA KULETA  KITAMBI

 

Vyakula vinavyochangia  kuleta  kitambi ni  pamoja  na :

i.                    Vyakula  vyenye  mafuta  mengi  kama  vile  nyama nyekundu  (iwe ni ya kuchemsha, kukaanga au kuchoma), nyama  ya  kuku  wa  kizungu  ( iwe  ya  kuchemsha, kukaanga  ama  kuchoma ), mafuta ya kupikia, (hasa yale yatokanayo na bidhaa za wanyama, kama siagi, na jibini), viazi vya kukaanga kwa  mafuta  (chips) pamoja  na  pizza.

ii.                   Vyakula vyenye wanga mwingi kama  vile ugali wa mahindi, mihogo, wali, mkate  mweupe.

iii.                 Vyakula  na  vinywaji  vyenye  sukari  nyingi  iliyo  ongezwa 

( added  sugar ), kama  vile  soda  na  keki.

 

iv.                Vyakula  vilivyo  tengenezwa  kwa  ngano  na  sukari kama  vile  keki, skonzi, chapatti, maandazi, mkate  mweupe  nakadhalika

v.                  Pamoja  na  vinywaji  vilivyo  tengenezwa  kwa  kutumia  ngano  kama  vile  bia  za  aina  mbalimbali  na  kadhalika.

Vyakula  vilivyo  tajwa  hapo  juu, vikitumiwa  bila  kuzingatia  kanuni  za  mlo  kamili, huchangia  kuleta  tatizo  la  kitambi.

vi.                Sababu nyingine ni  kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na  viungo

(  physical  exercises  )  kwa  muda  mrefu.

 

JINSI YA KUJUA KAMA UNA KITAMBI

Kitambi kinaweza kuonekana kirahisi kwa macho. Ila kujua ni kwa kiwango gani kitambi chako kipo inabidi kufanya vipimo vya kiuno(waist) na nyonga (hips).

Mzingo wa kiuno ukiwa >102 cm au 40  kwa wanaume na >88 cm au 35  kwa wanawake, na uwiano wa kiuno na hips(Waist-Hip Ratio) ikiwa >0.9 kwa wanaume na >0.85 kwa wanawake.

BMI ya 30 au zaidi inaashiria 'Obese' uzito kuzidi kiasi. Kuwa na mzingo uliozidi kawaida ni kiashiria hatari cha matatizo ya kimetaboliki, kuliko hata cha BMI.

Kipimo kingine cha kitambi ambacho kimeonyesha uwezo zaidi kuliko BMI katika kutabiri uwezekano mkubwa wa magonjwa ya moyo ni Index Of Central Obesity(Waist-To-Height Ratio-WHtR) ambapo uwiano ukiwa sawa na 0.5 au zaidi, hii ikimaanisha mzingo wa kiuno angalau ni nusu ya kimo cha mtu.

Kipimo kingine ni Body Volume Index, kinachopima kitambi kwa kupima umbo la mtu na mgawanyo wa uzito wake.

 

MAMBO  YANAYO  MUWEKA  MTU  KATIKA  HATARI  YA  KUPATWA  NA  KITAMBI

 

Tumekwisha  ona  hapo  juu jinsi  kitambi  kinavyo  patikana  na  vyakula  pamoja  na  sababu  nyinginezo  zinazo  sababisha  kutokea  kwa  kitambi, sasa  tutazame  mambo  yatakayo  kufanya  uwe  katika  hatari  ya  kupatwa  na  kitambi.

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za kitaalamu, mambo  yafuatayo  huwaweka  watu  katika  hatari  kubwa   ya  kupatwa  na  kitambi :

1.          Ulaji  mbovu  wa  chakula; Ulaji  mbovu  wa  chakula  ni  ulaji  usio  zingatia  kanuni  za  mlo  kamili. Hapa  mtu  hufululiza  kutumia  chakula  cha  aina  fulani  pekee  bila  kuzingatia  aina  nyinginezo  za  chakula.  Mfano; mtu  anaweza  kuwa  anakula  mlo  ufuatao :

Asubuhi :  Mchemsho  ama    supu  ya  ng’ombe , chapatti  tatu  na  soda  moja.  Mchana :   Ugali  nyama  choma anashushia  kwa  maji  na  soda.

Jioni :  Mchemsho  wa  kuku  na  bia  mbili  nakuendelea.

Usiku  :  Chips  mayai  au  chips  kuku  au  chips  mishikaki  na  bia.

Mtu  huyu  akiendelea  na  utaratibu  huu  kwa  muda  mrefu, ni  lazima  atapatwa  na  kitambi.

 

2.           Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  mafuta  mengi 

3.          Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye wanga  mwingi  .

4.          Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vyenye  sukari  iliyo  ongezwa ( added  sugar  ).

5.          Ulaji  mfululizo  wa  vyakula  vya  ngano.

6.          Ulaji  mfululizo  wa   vinywaji  vyenye ngano  na  sukari.

7.          Kutofanya  mazoezi  ya  mwili  na viungo  ( physical  exercises  ).

Mhusika  anapokuwa  katika  makundi  yote  yali yotajwa  hapo  juu, hali  huwa  mbaya  zaidi.  

 

NJIA ZA KUONDOA KITAMBI

 

Kuwa  na  kitambi  ni  lugha  ya  mwili  ( body-language )  inayo  leta  ujumbe  kwako  kwamba  “ Mwili    wako  haupo  salama  tena “

 

Kama  una  kitambi   maana  yake  una  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini, mwili  wako  unatumika  kuhifadhi  mafuta  usiyo  yahitaji.

 

Hali  hii  kitabibu  imaanisha  kwamba, ogani  nyinginezo  zilizomo  ndani  ya  mwili  wako  zinao gelea  kwenye  mafuta( fats  )  yasiyo  hitajika   yaliyomo ndani  ya  mwili  wako,  jambo  linalo  kuweka  katika  hatari  kubwa  sana  ya  kushambuliwa  na  magonjwa  hatari  kama  vile  shinikizo  kubwa  la  damu, kiharusi  na kisukari  na  kwa kutaja  machache.

Hivyo  basi  ili  kuondokana  na  hatari  hiyo, yakupasa   kupambana  kuondoa  hayo  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini  mwako.

 

NJIA   ZA  KUONDOA  KITAMBI.

 

Unaweza  kuondokana  na  kitambi  kwa  kufanya  diet  pamoja  na  mazoezi ya  mwili  na  viungo.

Vilevile  unaweza  kuondoa  kitambi  na  kupunguza  mafuta  mwilini  kwa  kutumia  dawa  asilia  ya  kuondoa  kitambi  na  kuondoa  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

 

 

JINSI  TIBA  YA  KUONDOA  KITAMBI  INAVYO  FANYA  KAZI

 

1.          Kuyeyusha  mafuta  yasiyo  hitajika  mwilini.

2.          Kusaidia  kupunguza  hamu  ya  chakula.

3.          Kuzuia  kutengenezwa  kwa  seli  za  mafuta  ( fat cells  ) katika  mwili  wa  mwanadamu. Unapokula  chakula  chenye  mafuta  mengi, dawa  hufanya  kazi  ya   kupambana  kuyafanya  mafuta  hayo  yasitengeneze  seli  za  mafuta  mwilini  mwako. Hali  hii  huuepusha  mwili  wako  kuhifadhi  mafuta   yasiyo  hitajika  mwilini.

4.          Kusaidia  kupunguza  uzito wa mwili  kwa  haraka 

 

 

 

UHUSIANO  KATI  YA  KITAMBI  NA   TATIZO  LA  NGUVU  ZA  KIUME

Ili  uume  wa  mwanaume  uweze  kusimama  barabara kitu  cha  kwanza  kabisa  mwanaume  huyo  lazima  apate  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, wazo  hili  huweza  kuchagizwa  na  vichocheo  mbalimbali  kama  vile  kuyaona  maumbile  ya  mwanamke  ampendae,  wazo  hili  hunaswa  kama sumaku  kwenye  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  kwenye  ubongo.  Mishipa  ya  fahamu ikisha  pata  picha  hii  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  kwenye  ubongo  ambayo  nayo  hupeleka  taarifa  kwenye  mishipa  ya  ateri, mishipa  ya  ateri  ikipokea  taarifa  hii  hufunguka   na  inapofunguka  damu  hutiririka  kuelekea  kwenye  misuli  ya  uume na  mwisho  wa  siku  uume  usimama.

Jambo  hili  ni  gumu  sana  kwa  mwanaume  mwenye tatizo  la  kitambi, au  tatizo  la  unene  ulizo  zidi  au  tatizo la  uzito  ulio  pita  kiasi  kwa  sababu  zifuatazo:

 

1.      Kwanza  mwanaume  mwenye  kitambi, unene  ulio  zidi  au  uzito  ulio  zidi  ana  kiwango  kikubwa sana  cha  mafuta  yasiyo  faa  kwenye  damu.    Mafuta  hayo  kwanza  huathiri  utendaji  kazi  wa  moyo  katika  kusukuma  damu  lakini  pili  huathiri  utiririkaji wa  damu  kutoka  kwenye  moyo  kuelekea  katika  maeneo  mengine  ya  mwili  ikiwamo  misuli  ya  uume..  Kwa  hiyo  mwanaume  huyu  hata  mishipa  ya  ubongo  wake  ikipata w azo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, damu  hushindwa  kutiririka  vizuri  kwa  sababu  inapata  upinzani  kutoka  kwenye  mafuta  yaliyo  ganda  kwenye  mishipa  ya  damu, mwisho  wa  siku  mwanaume  huyu  anakuwa  na  weak  erection  na  hata inapotokea  mwanaume  huyu akapata  erection  hufika  kileleni  kwa  muda  mfupi  na  hukosa  uwezo wa  kurudia  tendo  la  ndoa.

2.      Pili  mwanaume mwenye  kitambi, unene  ulio  zidi  au  uzito  ulio zidi huweza  kuwa  na  kiwango  kikubwa  cha  sukari  kwenye  damu.  Kiwango kikubwa  cha  sukari  kwenye  damu  huweza  kuathiri  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  fahamu  katika  ubongo. Na  kama  nilivyo sema  hapo  awali  kwamba  ili uume  wa  mwanaume  uweze  kusimama  ni  lazima  kwanza  mwanaume  huyo  apate  wazo  la  kufanya  tendo la  ndoa.  Sasa  basi  kwa  kuwa  ufanisi  wa  mishipa  yake  ya fahamu  katika  ubongo  umekuwa  dhaifu , mwanaume  huyu  hata anapo  pata  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, mishipa  yake  katika  ubongo  hufanya  kazi  katika  hali dhaifu  na  matokeo  yake  hata  erection yake  huwa  dhaifu.  Kama  hiyo haitoshi  kiwango kikubwa  cha  sukari  kwenye  damu  pia  huathiri  utiririkaji  wa  damu.

3.       Mwanaume   mwenye  kitambi, unene  na/au  uzito  ulio zidi anaweza  kuwa  na  kiwango  kikubwa  cha  sumu  kwenye  damu, sumu ambayo  huathiri  suala zima  la  utiririkaji  wa  damu .

 

 

 

 

SULUHISHO   KWA  MWANAUME  MWENYE  KITAMBI  AMBAE  ANASUMBULIWA  NA  TATIZO  LA  UKOSEFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.

Mwanaume  mwenye  tatizo  la  kitambi  au  unene  ulio  zidi  au  uzito  ulio  zidi  anatakiwa  apate  tiba  ya  asili  ambayo  kwanza  itaondoa  mafuta  yote  yasiyo faa  kwenye  mishipa  ya  damu,   tiba  itakayo  rekebisha  kiwango  cha  sukari  kweny e  damu  yake, tiba  ya  asili  itakayo  ondoa  sumu  yote  kwenye  damu  yake.  Tiba  zote  hizi  kwanza  zitaondoa  kabisa  kitambi  alicho  nacho, pili  zitapunguza  unene alionao , tatu  zitapunguza  uzito  wake  kwa  kiasi  kikubwa  sana  na  mwisho  zita  mtibu  na  kumponyesha  kabisa  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume linalo  mkabili.

 

MAKALA  HAYA  YAMEANDALIWA  NA  DUKA  LA  KUUZA  DAWA  LA  NEEMA  HERBALIST.  TUNAUZA  DAWA  MBALIMBALI ZA  ASILI  AMBAZO  ZINATIBU  NA  KUPONYESHAMATATIZIO  TUNAPATIKANA  UBUNGO  JIJINI  DAR  ES  SALAAM, NYUMA  YA  JENGO LA   UBUNGO  PLAZA  JIRANI  NA  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

 

WASILIANA  NASI  KUPITIA  SIMU  NAMBA :  0766   53  83  84.

TUTEMBELEE  KUPITIA  BLOGU  YETU :  www.neemaherbalist.blogspot.com

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA