Skip to main content

JITIBU KISUKARI, PRESHA, SHINIKIZO LA DAMU, FIGO NA MOYO KWA TIBA ASILIA

Unaweza  kujitibu  tatizo  la  moyo,figo,shinikizo  la  damu  ama  kisukari  kwa  kutumia  dawa  asilia.  Ifuatayo  ni  namna  ya  kujitibu  matatizo  tajwa  hapo  juu  kwa  tiba  asilia. Tunaanza  na  tatizo  la  kisukari.

 

JINSI  YA  KUJITIBU  KISUKARI  KWA  TIBA  ASILIA


1. UWATU

Dawa mbadala 10 zinazotibu Kisukari

Uwatu
Tafiti nyingi zimeonyesha kuwa uwatu unao uwezo mkubwa katika kutibu kisukari. Uwatu huzisisimua seli katika kongosho kitendo kinachofanya uzalishwaji wa insulini kuongezeka. Maajabu haya ya uwatu yanasemekana kufanyika kutokana na uwatu kuwa na asidi amino mhimu sana ijulikanayo kama ‘4-hydroxyisoleucine’. Miaka mingi kabla hata ya huu utafiti kufanyika, uwatu umekuwa ukitumika kama moja ya dawa bora kabisa za asili katika kutibu kisukari.
Namna ya kuutumia Uwatu kujitibu kisukari
• Chota mbegu za uwatu vijiko 4 na uziloweke katika maji robo lita kwa usiku mmoja. Asubuhi ponda ponda hizo mbegu za uwatu ndani ya maji kisha zichuje na upate maji yake. Kunywa maji haya kila siku asubuhi kwa muda wa miezi 2.
• Chukuwa uwatu ya unga vijiko vikubwa 2 na uweke ndani ya maziwa au maji ya uvugu uvugu robo lita, koroga vizuri na unywe kila siku kutwa mara 2 kwa miezi 2.
• Chukuwa gramu 100 za mbegu za uwatu na gramu 50 za binzari manjano. Unaweza kuongeza kiasi kidogo cha pilipili manga nyeupe kwenye mchanganyiko huu. Ongeza kijiko 1 cha mchanganyiko huu wote katika maziwa robo lita na unywe kutwa mara 2 kila siku.
• Unaweza pia kuongeza uwatu ya unga katika unga wako unaotumia kutengenezea mkate au hata chapati.

2. MDALASINI


Dawa mbadala 10 zinazotibu Kisukari
Mdalasini
Utafiti uliofanywa kwa watu wenye kisukari aina ya pili umeonyesha kuwa utumiaji wa gramu 1 hadi 6 za mdalasini kwa siku unaweza siyo tu kupunguza kaisi cha damu sukari mwilini, bali pia unaweza kupunguza kiasi cha mafuta mazito katika damu (triglyceride) na hata kudhibiti kolesto!
Waathirika wa kisukari pia hutokewa kuwa na matatizo katika mfumo wao wa upumuwaji, hivyo utumiaji wa mdalasini kwao unaleta maana zaidi kwakuwa mdalasini unao uwezo mkubwa katika kuzuia magonjwa katika mfumo wa upumuwaji pia. Mdalasini ya unga hushusha kiwango cha damu sukari kwa kuziamsha shughuli za insulini. Mdalasini pia ina faida kwa watu waliogunduliwa kuwa na kisukari cha mwanzo (pre-diabetes status) na hivyo matumizi ya mdalasini kwao yatasaidia kuzuia wasipatwe na kisukari katika siku za usoni.
Hata hivyo aina ya mdalasini unaotumia pia inahusika katika kutibu kisukari au maradhi mengine. Nashindwa kupata maneno haya kwa Kiswahili lakini kuna aina kama mbili hivi za mdalasini ambazo ni ‘Cassia cinnamon’ ambao wenyewe huwa na kitu kingine ndani yake kiitwacho ‘coumarin’ ambayo ni sumu na husababisha matatizo katika ini. Mdalasini nzuri kwa kutibu kisukari na ambayo bei yake ipo juu kidogo ni ile iitwayo kwa kiingereza kama ‘Ceylon cinnamon’.

Namna ya kutumia mdalasini kutibu kisukari
• Chukuwa lita 1 ya maji na uyachemshe. Mara yatakapoanza kuchemka, ongeza vijiko 3 vikubwa vya mdalasini ya unga na uache kwa dakika kama 15 hivi kisha ipuwa chuja na unywe ikiwa bado ya uvugu uvugu kutwa mara moja kila siku kwa mwezi 1.
• Ongeza mdalasini kijiko kidogo kimoja cha chai katika kikombe kimoja (robo lita) cha maji ya uvugu uvugu, koroga na unywe kila siku.
• Unaweza pia kuongeza mdalasini ya unga ndani ya kachumbari kila unapokula.

3. MAJANI YA MANJANO


Dawa mbadala zinazotibu Kisukari
Majano ya Manjano
Utafiti unaonyesha kuwa, kutokana na kuwa na kiasi kingi cha madini kama vile madini ya chuma, Zinki, na shaba; majani ya manjano ni mhimu sana katika kuutunza usawa wa glukozi katika damu. Madini haya huziamsha seli za kongosho zinazohusika na uzarishwaji wa homoni ya insulini. Majani ya manjano pia husaidia umeng’enywaji wa wanga mwilini. Yanao uwezo wa kuviamsha upya vimeng’enya katika figo na ini ambazo zinahusika katika kumeng’enya wanga na kuurudisha katika hali yake ya kawaida na hivyo kusaidia kutibu kisukari.
Wagonjwa wa kisukari huwa wana tatizo la kuwa na uwezo mdogo kudhibiti sumu mwilini jambo ambalo hupelekea seli zao za mwili kufa katika kiwango kingi. Utafiti unaonyesha kuwa majani ya manjano yana uwezo wa kupunguza kiasi cha seli kufa, seli ambazo ni mhimu katika uzarishwaji wa insulini.
Majani ya manjano yanaweza kushusha usawa wa damu sukari na ni mhimu sana kwa watu wanaopata kisukari kama matokeo ya uzito kuzidi. Ikiwa kisukari kinazunguka katika familia yenu, jitahidini kutumia majani ya manjano kwakuwa yamethibitika kuthibiti pia hata kile kisukari cha kurithi.
Namna ya kutumia majani ya manjano kujitibu kisukari
• Tafuna majani freshi ya manjano 7 mpaka 10 kila siku asubuhi.
• Tumia majani ya manjano kwenye kila chakula unachopika kila siku.


4. MSHUBIRI (Aloe Vera)


Dawa mbadala zinazotibu Kisukari
Mshubiri/Aloe Vera
Wakati mshubiri umekuwa ukitumika kwa miaka mingi katika kutibu kisukari, baadhi ya tafiti za hivi karibuni zimeonyesha kuwa mshubiri unao uwezo pia katika kushusha kiwango cha damu sukari na mafuta katika mzunguko wa damu kwa wagonjwa wanaosumbuliwa na kisukari. Mshubiri umethibitika katika kutibu kisukari cha aina ya kwanza na hata cha aina ya pili.
Jinsi ya kuandaa mshubiri kutibu kisukari
Changanya vifuatavyo:
• Jeli ya mshubiri kijiko cha chai 1
• Unga wa majani ya matunda ya damu ya mzee kijiko cha chai 1
• Unga wa manjano kijiko cha chai 1
Kunywa mchanganyiko huu kila siku kabla ya chakula cha mchana na jioni.


5. MAJANI YA MUEMBE


Dawa mbadala zinazotibu Kisukari
Majani ya Muembe
Wakati tunda la embe halina uwezo wa kutibu kisukari, majani ya mti wa muembe yanao uwezo huo! Waganga wengi wa Nigeria wamekuwa wakitumia sana majani ya muembe katika kutibu kisukari. Yanao uwezo wa kupunguza ufyonzwaji wa glukozi katika utumbo mkubwa hivyo kusaidia kupunguza usawa wa sukari katika damu. Pia yana uwezo mkubwa katika kudhibiti kiwango cha mafuta katika damu.
Namna ya kuandaa
• Loweka majani 10 mpaka 15 ndani ya nusu lita ya maji kwa usiku mmoja. Chuja maji haya asubuhi mapema na uyanywe kabla ya kula chochote. Subiri lisaa limoja lipite ndipo ule chakula cha asubuhi.
• Kausha majani ya muembe kwenye kivuli. Yatakapokuwa yamekauka kabisa, yasage kupata unga wake na hifadhi unga huu katika chombo kisafi na kisha lamba unga huu nusu kijiko kidogo cha chai kila siku kabla ya chakula cha mchana na jioni.


6. MREHANI


Dawa mbadala zinazotibu Kisukari
Mrehani/Basil
Mrehani (basil) una faida nyingi sana kiafya. Nje ya kudhibiti kisukari, Mrehani pia una sifa na uwezo katika kudhibiti asthma, kuondoa mfadhaiko, kudhibiti bakteria, kudhibiti virusi, kudhibiti vivimbe, kuondoa sumu mwilini, kudhibiti asidi tumboni, na kuongeza kinga ya mwili. Mrehani huzisaidia pia seli za kongosho kufanya kazi zake vizuri na kusaidia utolewaji au uzarishwaji mzuri wa insulini.
Jinsi ya kuutumia mrehani kutibu kisukari
• Tafuna majani mawili mpaka manne ya mrehani kila siku asubuhi kabla hujala chochote.
• Ponda majani ya mrehani kupata juisi yake kama kijiko kimoja hivi cha chai na unywe kila siku asubuhi kabla ya kula kitu chochote.


7. BAMIA


Dawa mbadala zinazotibu Kisukari
Bamia
Bamia zina kiasi kingi cha vitamini A, B6, C, K, magnesium, potassium, zinki, na faiba. Bamia ina uwezo mkubwa katika kusawazisha usawa wa sukari mwilini. Mbegu za Bamia zina kidhibiti kiitwacho alpha-glucosidase ambacho huzuia wanga kujibadili kuwa glukozi. Faiba iliyomo kwenye bamia husaidia kurekebisha kiwango ambacho sukari humeng’enywa katika utumbo mkubwa.
Jinsi ya kutumia Bamia katika kujitibu Kisukari
Mahitaji:
• Bamia 2 mpaka 3
• Maji glasi 1
Jinsi ya kuandaa:
• Zisafishe bamia vizuri kabisa.
• Ondoa au ikate sehemu ya kichwa na mkia katika bamia na utupe. Kisha kata kila bamia katikati kwa urefu ili kupata vipande 2, hivyo utapata jumla vipande 4 kwa bamia hizo 2.
• Hivyo vipande 4 viweke ndani ya glasi iliyojaa maji, funika na uache hivyo kwa usiku mmoja.
• Asubuhi na mapema kunywa hayo maji yote yaliyokuwa na bamia kabla ya kula kitu kingine chochote. Ukiweza unaweza kula hata hizo bamia pia. Bamia mbichi zinafaida zaidi mwilini kuliko zilizopikwa.
• Fanya hivi kila siku kwa miezi kadhaa.


8. MBEGU ZA KATANI


Dawa mbadala zinazotibu Kisukari
Mbegu za Katani
Mbegu za katani zina kiasi kingi cha mafuta mhimu sana yajulikanayo kama “essential omega-3 fat alpha-linolenic acid (ALA)’’, pia zina protini, faiba na muunganiko wa mmea uitwao ‘lignans’. Hii lignans hufanya kazi kama kiuaji sumu au kwa maneno mengine hufanya kazi ya kuondoa sumu mwilini. Baadhi ya tafiti zimeonyesha kuwa mbegu za katani zinao uwezo wa kusawazisha usawa wa damu sukari mwilini kwa vile zina kiwango kikubwa cha faiba ndani yake. Mbegu za katani zinasaidia katika kazi za kumeng’enya chakula, pia husaidia katika ufyonzaji mzuri wa mafuta na sukari. Kama unatumia mara kwa mara hizi mbegu za katani, kiasi chako cha sukari chaweza kushuka hadi asilimia 28 kwa wakati mfupi.
Jinsi ya kutumia mbegu za katani katika kutibu kisukari
• Ongeza kijiko kikubwa kimoja cha unga wa mbegu za katani ndani ya glasi ya maji au maziwa na unywe wakati wa chakula chako cha asubuhi.
• Ongeza kijiko kidogo kimoja cha chai cha unga wa mbegu za katani katika nafaka zako unazotumia wakati wa chakula cha asubuhi.
• Ongeza pia unga wa mbegu za katani katika supu.


9. Chai ya Majani ya Mpapai


Dawa mbadala zinazotibu Kisukari
Majani ya Mpapai
Majani ya mpapai ni mazuri katika kuongeza ufanisi wa insulini. Ni mazuri kwa watu wenye kisukari cha aina ya pili. Pia majani ya mpapai husaidia kupunguza matatizo yawezayo kuwatokea watu wenye kisukari, matatizo kama vile mafuta kwenye ini, matatizo katika kibofu cha mkojo na pia husaidia kupunguza mfadhaiko/stress. Kuna faida nyingine kubwa zaidi ya kutumia majani ya mpapai ambayo ni uwezo wake katika kutibu vidonda vitokanavyo na kisukari kwa haraka zaidi. Waganga wengi wa tiba asili kutoka Japani na Australia Na wengine wengi toka mataifa mbalimbali wamekuwa wakitumia majani ya mpapai kutibu kisukari kwa miaka mingi sasa.
Mahitaji:
• Majani 10 ya mpapai
• Maji lita 2

Maandalizi:

• Tumbukiza hayo majani ya mpapai katika maji.
• Chemsha hayo majani katika maji kwenye moto hadi maji yatakapobaki nusu yake (lita 1).
• Ipuwa na uache ipowe
• Kunywa maji haya kidogo kidogo kutwa nzima. Fanya hivi kwa mwezi mmoja mpaka miwili.
Juisi hii ya majani ya mpapai iliyoandaliwa kwa mtindo huu ni nzuri katika kuondoa sumu mwilini na kurekebisha afya yako kwa ujumla huku ikirekebisha matatizo katika mfumo wa umeng’enyaji wa chakula na kuongeza kinga ya mwili wako.

10.Cocktail  ya  asili


Dawa mbadala zinazotibu Kisukari
Juisi ya Asili
Hii ni juisi nzuri sana kwa mtu yeyote anayesumbuliwa na kisukari na hata shinikizo la damu, vitu vingi vinavyoingia katika juisi hii ni tiba nzuri kwa magonjwa mengi mwilini. Hii ni juisi inayotengenezwa kutokana na mchanganyiko wa vitu tofauti vifuatavyo.
  • Vitunguu swaumu 12
  • Vitunguu maji 12
  • Tangawizi 12
  • Asali ya nyuki wadogo lita 1
  • Ndimu 12
  • Chumvi ya mawe kijiko kidogo kimoja
Namna inavyoandaliwa
Saga (blendi) kwa pamoja vitunguu saumu na vitunguu maji pamoja na maji lita 2 na uchemshe kwenye moto kwa dakika kumi. Ikipoa chuja vizuri kupata juisi yake.
Saga tangawizi pamoja na maji lita 1 Ikipoa chuja vizuri kupata juisi yake, weka pembeni kwenye bakuli safi
Chukuwa limau au ndimu kata katikati kila moja na uchemshe kwenye moto na maji lita moja kwa dakika 15. zikishachemka subiri zipowe kisha zikamuwe na uchuje kupata juisi yake.
Changanya hizo juisi zote hapo juu katika chombo kimoja kikubwa na kisha
Ongeza asali ya nyuki wadogo mbichi nzuri lita moja, na mwisho ongeza chumvi ya mawe kijiko kidogo cha chai kimoja, koroga vizuri kwa pamoja.
Ukifuata vizuri maelezo haya mwishoni utapata juisi ya ujazo wa lita 5 au 6.
Kunywa juisi hii kikombe kimoja (robo lita) kutwa mara 3 kwa muda wa mwezi mmoja. Juisi hii inaweza kukaa bila kuwekwa kwenye friji wiki 2 hadi 3 bila kuharibika.
VITU MHIMU VYA KUZINGATIA KWA MTU YEYOTE ANAYESUMBULIWA NA UGONJWA WA KISUKARI:
  1. Acha kabisa soda ya aina yeyote pamoja na juisi za viwandani
  2. Acha chai ya rangi na kahawa
  3. Jishughulishe zaidi na mazoezi
  4. Ongeza unywaji maji na utumiaji wa chumvi hasa ya mawe ile ya baharini
  5. Dhibiti uzito wako, hakikisha una uzito ule unaotakiwa kuwa nao kwa mjibu wa urefu wako
  6. Tumia vyakula ambavyo havijakobolewa, mfano kama ni ugali tumia unga wa dona na siyo wa sembe . ITAENDELEA

Comments

  1. Hello,

    Kwa mawasiliano zaidi nitawapata kwa address au contacts zipi kupata ushauri au tiba muhafaka kwa dawa zenu za asili

    Asante,
    Amani

    ReplyDelete
  2. Nimefurahia na nimeelewa maelezo yenu. Kwa kweli ni maelezo rafiki. Mimi ni mmojawapo ninasumbuliwa na Kisukari aina ya pili na pengine hili la kutokua na uwezo wa kiume kusimama kisawasawa.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA