Skip to main content

PUNYETO ILISABABISHA NINUSURIKE KWENDA JELA




·        PUNYETO   ILISABABISHA   NINUSURIKE   KWENDA  JELA
·        Mimi ni kijana  mwenye  umri  wa  miaka  32

·       Tabia ya  kujichua  ilisababisha  nisurike  kwenda  jela.


·       Ni  hivi, nilianza  kujihusisha  na tabia  ya kujichua mwaka  2004  nikiwa  na umri  wa  miaka  19.

·       Tofauti  na  vijana  wenzangu, mimi  niliingia  kwenye  tabia  ya  kujichua  sio  kwa  sababu  ya  kukosa  msichana, la  hasha  ila  kwa  sababu, nilikuwa  naogopa  sana  ukimwi


·       Niliamini  kujichua  ndio  njia  pekee  na  ya  uhakika  ambayo  ingeniepusha  na hatari  ya  kupata  maambukizi  ya  virusi

·       Kabla  ya  kuanza  kujichua  tayari  nilikuwa katika  mahusiano  ya kimapenzi  na  wasichana  kadhaa.


·       Baada  ya  kujaribu  kujichua, nikawa  addicted.

·       Kujichua  ikawa  ndio  mchezo wangu wa  kila  siku .


·       Ilifikia  kipindi  nikawa  najichua  asubuhi  mara  tatu na  usiku najichua  pia.
·       Kama  ikitokea  mida ya  mchana  nimepata  sababu  ya  kujichua,na  nipo  maeneo ya  karibu  na  nyumbani, basi  nitaenda  chumbani  fasta, na  kama  nikiona  mazingira  hayaruhusu nitazuga  kama  naenda  kuoga  na  nikiwa  bafuni  namaliza  shughuli  huko  huko.

·       Pamoja  na  kwamba  nilikuwa  najichua, lakini  pia  ilikuwa  ikitokea  nikipata  msichana  ninakuwa  nae.


·       Pamoja  na  yote  hayo  cha  ajabu ni kwamba, hata  kama  nimetembea  na  msichana  siku  hiyo, usiku  lazima  nijichue.

·       Ilikuwa  haiwezi kupita  siku    bila  kujichua.


·       Niliendelea  na  tabia  hii  hata  nilipokuwa  chuo.

·       Wakati  nipo  chuo, mara  nyingi  nilikuwa  nachelewa  vipindi  vya  asubuhi, kwa  sababu  ilikuwa  ikifika  asubuhi ilikuwa ni  lazima  nijichue  na  nisingeweza  kufanya  hivyo mbele  ya  room mates  wangu, na  nisingeweza  kwenda  kufanyia bafuni  kwa  sababu  bafuni kulikuwa  na  foleni mida  hiyo  ya  asubuhi plus  mabafu yalikuwa  hayana  milango , so nikawa  nasubiria  roommates  waondoke  kwanza ili nijichue  kwanza, kisha  baada  ya  hapo ndio  niende darasani.


·       Wakati mwingine  nilikuwa  najichua  nikiwa  kwenye  internet  café. Hasa  hasa  zile  internet  café  zenye  vyumba .  Hii  ilikuwa  inatokea  kama  nikiwa  natazama pornography, basi nitafanya  namna  yoyote  ile  hadi  nijichue

·       Nilipomaliza  chuo nilifanikiwa  kupata  kazi  kwenye  taasisi moja.


·       Siku moja  nikiwa  mkoani  kikazi  nilikutana  na  mdada  mmoja, tukapendana.

·       Nilimkubali kwa  sababu  alikuwa  wife  material.


·       Niliporudi  Dar  nilirudi  nae, tukaanza  kuishi  kinyumba.

·       Hiyo  ilikuwa  mwaka  2013.

·       Pamoja  na  kwamba  nilikuwa  naishi kinyumba  na  mwanamke, lakini  bado  nilikuwa  siachi  kupiga  punyeto.


·       Wakati mwingine  nilikuwa  namuacha  amelala  kitandani  naenda  bafuni  kujichua.

·       Wakati mwingine  nilikuwa  nakataa  kushiriki  nae  unyumba,  na  tukiwa  tumelala, usiku  wa  manane  akiwa  amelala, nitajichua  bila  yeye  kustukia.
·       Nilikuwa  nimeshazoea  asubuhi lazima  nijichue, sasa  kuishi  kinyumba  na  mwanamke  kukawa  kikwazo  kwangu. Nikawa  nashindwa  kujichua  asubuhi.

·       Hivyo basi, ilikuwa  ikifika  weekend, asubuhi  ilikuwa  lazima  nimtume  aende  dukani  au hata  sokoni  mtaa  wa  tatu  au  mjini, lengo  likiwa  kupata  nafasi  ya  kujichua.


·       Ilifika  kipindi  Yule  mwanamke  nilikuwa  naweza  kukaa  nae  hata  miezi  miwili  bila kukutana  nae  kimwili. Na  hata  nikikutana  nae  kimwili  nilikuwa  nafanya  mara  moja  tu halafu nalala  hadi kesho  yake  asubuhi.

·       Kingine  naomba  niseme  ukweli, nilikuwa  mkorofi kidogo  kwa  huyu  dada, kwa  hiyo  wakati  mwingine  nilikuwa  nakuwa  mkali  sana  kwake  bila  sababu.


·       Nilifungua  duka  la  nguo, na  kumpa  dada  huyo  kazi  ya  kulisimamia.

·       Baada  ya  kuwa  mzoefu kidogo, nikawa  namuagiza  yeye  kwenda  kuchukua  marobota  ya  nguo za  kuuza  ofisini.


·       Baada  ya  kukaa na dada  huyu kwa  kama  mwaka  mmoja  hivi, siku  moja, kuna  kitu  aliniudhi  nikampiga.
·       Baada  ya  kumpiga , dada  huyo  alichukua  vitu  vyake, akaita  bajaji  na  kuondoka  zake.

·       Mimi  nilijua  ameondoka  na  atarudi tu mwenyewe  baadae  lakini haikuwa  hivyo.


·       Baada  ya  siku tatu  nikasikia  amepanga  chumba ambako anaishi  na  kijana  wa  kiume  aliyekuwa  anafanya  kazi  ya  bodaboda.

·       Pia  nikaambiwa, dada  huyo  amefungua  duka  la  nguo, na  kwenye  duka  hilo  anafanya  huyo  kijana  wa  kiume.


·       Nguo  hizo  zilikuwa  zinatangazwa  kupitia  instagram

·       Nilipatwa  na  uchungu  na  hasira  sana, kwa  kuona  kumbe  huyo  mwanamke  alikuwa  ananisaliti  na  huyo kijana.


·       Nikaingiwa  na  nia  ovu.

·       Nikatafuta  namba  mpya  na kupiga  simu ya ofisi  ya  duka  la  huyo  mdada, akapokea  kijana  huyo, nikamwambia  alete  nguo  Buguruni, ambapo  akakubali  bila  hiyana.


·       Nikiwa  Buguruni, nikatafuta  nondo. Lengo  langu  lilikuwa  Yule  kijana  atakapo  fika   hapo  Buguruni sokoni, nimpigie  kelele  za  mwizi  halafu  nimpige  na  hiyo nondo.

·       Nilikuwa  na  hasira  kweli  kweli.


·       Sijui  kitu  gani  kilitokea, wakati namsubiria  huyo  kijana  kwa  hasira  na  uchungu, nahisi  malaika  wa Mungu  waliniambia  hebu  ongea  na  hawa  watu.

·       Pale  Buguruni Rozana, siku hiyo  kulikuwa  na  vijana  kama kumi hivi,  wanao husika  na  magari, makonda  na  madereva.


·       Nikawafuata  wale  jamaa  kijiweni  kwao, nakuwaambia, bana, kuna  mtu  anatembea  na  mke  wangu, wanaishi pamoja  na  kufanya  biashara  pamoja, nimempigia  simu  huyo  mwanaume  anaishi na  mke  wangu  alete  nguo  hapa Buguruni, nataka  akifika  hapa  nimpige  na  nondo  kichwani  halafu nimuitie  mwizi.

·       Braza  mmoja  mwenye  hekima  na  busara  akaniambia  mdogo  wangu  usijaribu  kufanya  kitu  kama  hicho. Ukifanya  hivyo, utamuua  halafu utakamatwa  na  kuwekwa  ndani  au  wanachi  wenye  hasira  nao  watakuua. Usijaribu  kabisa mdogo wangu, tena  na  hiyo nondo  yako  ilete hapa.
·       Akaniambia, ni bora  useme   ameshirikiana  na  mkeo  kuiba  hela halafu  umweke  ndani  lakini sio  kumpiga.

·       Kidogo  ushauri wa  Yule  braza  ambao  uliungwa  mkono  na  watu wengine  walio kuwa  pamoja  kijiweni  ukanipa uwoga.


·       Lakini  hata  hivyo bado  nikawa  na  uchungu  na  kijana  Yule.

·       So  nikafanya  maamuzi  mapya, kwamba, sitampiga  na  nyundo, nitampiga  na  ngumi  huku  nikimuita  mwizi.


·       Nikaondoka eneo  walipokuwa  wale  jamaa nilio waomba, na  kusogea hadi maeneo ya  karibu na  Sewa  Bar  pale. Nakumbuka  ilikuwa  siku  ya  Jumamosi.

·       Yule  kijana  alivyo  fika  tu, hata  sikuuliza, nikamuitia  mwizi  huku nikimpiga  ngumi. Nilifanikiwa  kumpiga  ngumi  kama  mbili  hivi  za  kichwani.


·       Bahati nzuri, pale  walikuwepo  “Polisi Jamii”, wakanizuia nisiendelee  kumpiga, wakamkamata  na  kwenda  kituoni  huku  wakinitaka  na  mimi  niende  nao.

·       Kufika  kituoni  baada  ya  maelezo  yetu  kusikilizwa, nikaonekana  mimi  ndio  nina  makosa
·       So nikawekwa  ndani, nikisubiria  kufunguliwa shitaka la  shambulio la  kudhuru  mwili.

·       Bahati nzuri  Yule  kijana  alikuwa  mstaarabu  sana, akasema  hana shida  na  kesi  na  amenisamehe.


·       Kama hiyo haitoshi  akampigia  simu Yule  mwanamke  niliyekuwa  naishi  nae ambae  yeye ndio  aliekuja  kunitoa  polisi.

·       Baada  ya  kuchimba  ukweli nikaja  kugundua  kwamba, kumbe  Yule  kijana  ni mtoto  wa  dada  wa  Yule  mwanamke  niliye kuwa  naishi  nae  na  sio kweli  kwamba  walikuwa  wanaishi  nyumba  moja, ila  kuhusu  kwamba, kijana  alikuwa  anamsaidia  kusupply  nguo  kwa  wateja  wake  ni  kweli kwa  sababu  alikuwa  na  bodaboda  na  kipindi  hicho  bodaboda  zilikuwa  zinaruhusiwa  kuingia  hadi mjini.


·       Nilijaribu  kumbembeleza  Yule  mdada arudi  tusihi lakini  hakukubali bila  kutoa  sababu  yoyote  ile  ila  ninajua sababu  kuu ni mimi  kutokuwa  na  uwezo  wa  kushiriki  nae  tendo  la ndoa

·       Tangu  tukio  hilo  litokee sijafanikiwa  kuonana  tena  na  mdada  huyo, coz  alibadilisha  namba  zake za  simu  na  kurudi  kwao  mkoani…

Kila  ninapo ona  suala  la punyeto huwa  ninaogopa  sana, kwani  nalihusisha  na  mambo  mengi  mabaya. Upigaji  punyeto  unaweza  kumsababishia  mtu madhara  makubwa  kuliko  anavyo weza  kufikiria.
Kwa  mfano  huwa  najiuliza, kama  ningempiga  Yule kijana  na  ile nondo, halafu  akafa  sasa  hivi  si  ningekuwa  naozea  jela?

Upigaji  punyeto  ni  jambo  baya  sana. Kibaya  zaidi  kwa  upande  wangu, mpaka  wakati  huu  bado ninajihusisha  na  upigaji  punyeto, na  sidhani  kama  ninaweza  kuacha.
Nimekata  tama  ya  kuwa  na  mpenzi, kwa sababu  najua  hakuna  mwanamke  anaweza  kuishi  na  mwanaume  kama  mimi.


Kuacha  upigaji  punyeto  ni  changamoto  kubwa  sana. Hata  hivyo, unaweza  kujaribu  njia  ifuatayo. Njia  hii haijathibitishwa  kisayansi kumsaidia  addict  wa  punyeto  kuacha  punyeto, ila inaweza  kukusadia  ama  kukulazimisha  kuacha  punyeto.

Jinsi  njia  hii  inavyo  fanya  kazi, inasaidia  ku incapacitate viungo  vya  mwili vinavyo  husika  na  upigaji  punyeto.
Ni njia  ambayo  inahitaji  ushirikiano  wa  kutosha  wa  mwathirika.
Kufahamu kuhusu njia  hiyo, tafadhali tembelea :

Vile  vile  kama unataka  kufahamu  jinsi  punyeto  iinavyo sababisha  tatizo  la  ukosefu  na  upungufu  wa  nguvu za  kiume  na  jinsi  unavyo weza  kutibiwa  tatizo  la  ukosefu  na  upungufu  wa  nguvu  za  kiume  ambalo  limetokana  na  upigaji  punyeto, tembelea :




Vile vile, kama  na  wewe ni muathirika  wa punyeto, na  unataka kushare  nasi  jinsi  punyeto  ilivyo  athiri  maisha  yako, usisite  kutuandikia : neemaherbalist@gmail.com
Kisa  chako  kinaweza kuwa  na mafundisho  mazuri  na  chaweza  kuwa  msaada  kwa  mamilioni  ya  vijana  ambao  watapata  nafasi  ya  kusoma  story  yako.

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA