Skip to main content

TIBA LISHE YA MGONJWA WA PUMU





 
 Katika  makala  iliyopita, tumeufahamu  kwa  undani  ugonjwa  wa  pumu, makala  haya  yanaelezea  tiba  lishe  ya  ugonjwa  wa  pumu.  Zipo  aina  mbalimbali  za  lishe zinazo  weza  kutumika  kama  tiba  ya  ugonjwa  wa  pumu, leo  tutaanza  na  aina  ya  kwanza.


                        TIBA  LISHE  YA  UGONJWA  WA  PUMU
 
Baadhi ya vyakula vinavyoaminika kutoa ahueni na kuwa kama tiba kwa mgonjwa wa pumu ni pamoja na asali, juisi ya limau, mchanganyiko wa vitunguu swaumu na maziwa na mchangayiko wa mdalasini pamoja na asali. Vyakula hivyo vikiwa sehemu ya mlo wa mgonjwa kila siku, atapata ahueni ya ajabu.Pamoja na kuepuka ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, mgonjwa wa pumu anatakiwa pia kula kwa kiasi kidogo mlo wenye matunda, mboga za majani na vyakula vingine vitokanavyo na nafaka ambavyo hutoa ‘alikalaini’.

Aidha, wagonjwa wa pumu wanatakiwa kujiepusha na ulaji wa kiasi kikubwa cha wali, sukari, mtindi (yoghurt), unywaji mwingi wa chai, kahawa, pombe na vyakula vote vya kusindika au kwenye makopo.Mgonjwa anashauriwa pia kufanya mazoezi ya kuvuta hewa safi na kuishi katika hali ya hewa isiyo na baridi, kunywa maji mengi mara kwa mara, kufunga kula (fasting) japo mara moja kwa wiki. Kwa kufuata masharti hayo, mgonjwa anaweza kuishi na pumu bila kusumbuliwa wala kutumia dawa kali kwa maisha yake yote.Pia unatakiwa kuepuka kufanya mazoezi kwenye baridi, epuka moshi wa sigara, dhibiti ugonjwa wa kucheua na kiungulia, epuka kukaa na wanyama na epuka kuishi katika mazingira yenye hewa yenye unyevunyevu.


KWA  MAHITAJI  YA  DAWA  YA  ASILI  INAYO  TIBU  UGONJWA  WA  PUMU, TAFADHALI  FIKA  KATIKA  OFISI  ZETU  ZILIZOPO  KATIKA  ENEO  LA  CHANGANYIKENI  KARIBU  NA  CHUO  CHA  TAKIWMU, AU  PIGA  SIMU  0767010756  AU  0753644583.

Comments