Skip to main content

NIMEKAA KWENYE NDOA KWA MIAKA KUMI BILA KUPATA MTOTO NDIO MAANA NIMEIBA MTOTO WA MWANAMKE MWENZANGU.



Jeshi  la  polisi  nchini  Nigeria, katika  jimbo  la  Akwa  Ibom, linamshikilia mwanamama  Peace  Chukwuemeka  kwa  kosa  la  kumuiba  mtoto  mwenye  umri  wa  mwezi  mmoja  kutoka  kwa  mama  yake  mzazi.


Akihojiwa  na  polisi, mwanamama  huyo  alinukuliwa  akisema “  Nimekuwa  katika ndoa  kwa  muda  wa  miaka  kumi  bila  kupata mtoto. Nilichukua  uamuzi  wa  kumuiba  mtoto  huyo  ili  na  mimi  niwe  na  mtoto  wangu mwenyewe  na hivyo  kuepuka  manyanyaso  kutoka  kwa  mama  yangu  na  mume wangu.”

Akielezea  jinsi  alivyo fanikiwa  kumuiba  mtoto  huyo  kutoka  kwa  mama  yake, Peace  alisema :

“ Sikumewekea  dawa  wala  kitu  chochote, nilimkuta  mama  wa  mtoto  akiwa amesinzia  hivyo  nikatumia  fursa  hiyo  kumuiba  mtoto  na  kumpeleka  kijijini  kwa  mama  yangu lakini  mama  angu  alikataa  kumpokea, hivyo  nikaamua  kurudi  hapa  mjini, ambapo  mama  wa  mtoto  aliposikia  uwepo wangu  akaanza  kuniuliza  kuhusu  mtoto  na  kwenda  kutoa  taarifa  polisi na  mwishowe  nikakamatwa.


CHANZO : VYOMBO  MBALIMBALI  VYA  HABARI  NCHINI  NIGERIA.

Comments