Skip to main content

NIMEKAA KWENYE NDOA KWA MIAKA KUMI BILA KUPATA MTOTO NDIO MAANA NIMEIBA MTOTO WA MWANAMKE MWENZANGU.



Jeshi  la  polisi  nchini  Nigeria, katika  jimbo  la  Akwa  Ibom, linamshikilia mwanamama  Peace  Chukwuemeka  kwa  kosa  la  kumuiba  mtoto  mwenye  umri  wa  mwezi  mmoja  kutoka  kwa  mama  yake  mzazi.


Akihojiwa  na  polisi, mwanamama  huyo  alinukuliwa  akisema “  Nimekuwa  katika ndoa  kwa  muda  wa  miaka  kumi  bila  kupata mtoto. Nilichukua  uamuzi  wa  kumuiba  mtoto  huyo  ili  na  mimi  niwe  na  mtoto  wangu mwenyewe  na hivyo  kuepuka  manyanyaso  kutoka  kwa  mama  yangu  na  mume wangu.”

Akielezea  jinsi  alivyo fanikiwa  kumuiba  mtoto  huyo  kutoka  kwa  mama  yake, Peace  alisema :

“ Sikumewekea  dawa  wala  kitu  chochote, nilimkuta  mama  wa  mtoto  akiwa amesinzia  hivyo  nikatumia  fursa  hiyo  kumuiba  mtoto  na  kumpeleka  kijijini  kwa  mama  yangu lakini  mama  angu  alikataa  kumpokea, hivyo  nikaamua  kurudi  hapa  mjini, ambapo  mama  wa  mtoto  aliposikia  uwepo wangu  akaanza  kuniuliza  kuhusu  mtoto  na  kwenda  kutoa  taarifa  polisi na  mwishowe  nikakamatwa.


CHANZO : VYOMBO  MBALIMBALI  VYA  HABARI  NCHINI  NIGERIA.

Comments

Popular posts from this blog

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na...

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ...

FAIDA KUMI ZA MTI WA MKOMAMANGA

Mti   wa   Mkomamanga   ni   mti   wenye   faida   nyingi   sana   katika   afya   ya   mwanadamu. Mti   huu   una   virutubisho –afya     mbalimbali   ambavyo   ni   muhimu   katika   afya   ya   mwanadamu.   Virutubisho   hivyo   vinapatikana   kwenye   magome, majani, mbegu, maganda   ya   matunda, juisi   ya   matunda   pamoja   na kwenye   maua   ya   mti   wa   mkomamanga. Zifuatazo   ni   faida   muhimu   za   mti   wa   mkomamanga : 1.           Maganda   ya   tunda   la   mkomamanga   yakichemshwa    hutoa   juisi    ambayo   hutumika   kama   dawa   ya   kufunga   kuhara. 2.   ...