Skip to main content

KWANINI LEVINA MUKASA ALIJIUA UDSM?







 Tarehe kama ya leo mwaka 1990 wakati mwanafunzi wa kike wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alipojiua, watu wengi walifikiri kuwa alifanya hivyo kwa sababu alikuwa na matatizo kwao na kuwa masomo yalikuwa yanamshinda. Hata hivyo, waliposikia kwamba alifanya hivyo kutokana na unyanyawaji wa kijinsia uliofanywa na wanafunzi wawili wa Kitivo cha Uhandisi pamoja na kikundi kilichojukana kama “Punch”, baadhi walikasirika wakati wengine walicheka tu.

Marehemu Levina Mukasa, alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza aliyekuwa akisomea shahada ya ualimu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kulingana na maelezo ya waliokuwa wakimfahamu wanasema alikuwa mkimya mwenye msaada na ambaye wakati wote alikuwa tayari kutumia vitu vyake na wenzake. Kila aliposoma wakati wote alishika nafasi ya juu darasani.

Mnamo tarehe 7 Februari 1990, Levina alikatisha maisha yake kwa kumeza vidonge vingi vya klorokwini (vinavyotumika kutibu Malaria). Swali linabaki, “kwa nini alifanya hivyo?” Karibu kila mwanafunzi wa kike aliyesoma katika kampasi kuu ya Chuo Kikuu (inayojulikana sana kama Mlimani) atakuwa amenyanyaswa kijinsia katika kipindi cha Miongo miwili iliyopita. Wamekuwa wakidhihakiwa, kutishiwa kijinsia au kuvamiwa papo kwa hapo na kubakwa.

PUNCH

Pamoja na hayo lipo kundi la kisirisiri hapo mlimani linajukana sana kama PUNCH, linafikia hata kiwango cha kuchapisha maandishi na michoro michafu kuhusu habari za kimapenzi za sasa au za zamani za Mhasirika wao. Madhumuni hasa ya PUNCH ni kuwaweka wanawake chini ya wanaume, kuwafanya wanafunzi bora wa kike washindwe masomo yao na hata kulazimika kukatisha masomo. Inatumiwa pia kuwatishia wasichana wakubali kufanya mapenzi na watu wanaowataka ambao wako katika kundi la PUNCH. Kumkataa mtu aliyeko kwenye kundi la PUNCH kunamfanya mhusika“apanchiwe”.

Bahati mbaya, wanawake walio katika kampasi wanaiogopa PUNCH. Wanafungwa na sheria zake kama vile kutokunywa chai ya saa 10.00 katika mgahawa, kutokukaa kwenye high table, kutokuvaa khanga Mgahawani n.k. Wengine wanafurahia hata kumwona mwanamke mwenzao akipanchiwa. Kutokana na maelezo ya shangazi wa marehemu, Dkt. V.K. Masanja, ambaye ni mhadhiri wa hapo Mlimani, matatizo ya Levina yalianza wakati wa dansi ya kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka wa kwanza iliyofanyika kwenye hoteli ya Silversands ambapo alikataa kwenda na mwanafunzi wa mwaka wa nne wa Kitivo cha Uhandisi aitwaye Mark Victor.

FUJO

Levina alienda dansi hiyo na rafiki zake. Victor alipomuona alimtaka warejee pamoja na akalalamika kwa nini alidhubutu kwenda kwenye dansi na watu wengine wakati alikataa kwenda naye. Levina alikataa kuondoka naye na Victor akamvuta gauni, rafiki zake walijaribu kumtetea na papo hapo ugomvi ukaanza. Baadhi ya marafiki wa Victor wanaojita “Engineers” [Wahandisi] [kundi linalofahamika sana kati ya wanafunzi] walimsaidia Victor. Kundi jingine lijulikanalokama “insiders” walimsaidia Levina. Hatimae, baada ya kushindwa Wahandisi waliondoka kwenye dansi, lakini huo haukuwa mwisho wa matatizo ya Levina.

Waliporejea kwenye dansi mgogoro mwingine ulizuka kati ya Victor na kundi lake na Levina na rafiki zake. Walipofika kwenye mabweni yao, Victor alikuwa akimsubiri ndipo ikawa usiku mzima kutupiana matusi. Asubuhi na mapema Levina alipeleka malalamiko MUWATA [Serikali ya wanafunzi] uongozi ambao ulisulihisha tatizo hilo. Victor aliomba radhi na akadai kuwa alikuwa amelewa.

Siku iliyofuatia, tukio la Silversands lilipanchiwa. Michoro ya Punch haikumwonyesha jina lake lakini kwa kutoa namba yake yakusajiliwa ilidhihirisha kuwa michoro inayofuatia angekuwemo. Baadhi ya wanafunzi wa kiume walimwendea Levina na kumwambia kuwa walikuwa kwenye kundi la PUNCH. Walimtishia kumpanchi iwapo angekataa kufanya nao mapenzi. Aliwakatalia na akakosa raha sana. Mmojawapo wa wanafunzi hawa alikuwa Omari Saloti, mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Uhandisi.

Dkt. Masanja alisema kuwa yeye (Levina) ndiye alimweleza yaliyotokea. Dkt. Masanja alisema kuwa alimweleza Levina kuhusu uzoefu wake na mambo ya PUNCH alipokuwa mwanafunzi na jinsi alivyoweza kuyapuuza. Alisema kuwa Levina alionyesha kupata ujasiri na akafikiria kuwa mambo yamekwisha. Marafiki wa Levina waliambiwa kuwa wangepanchiwa iwapo wangeonekana wakiandamana naye. Alitengwa. Maelezo machafu yalitolewa na maandishi yaliandikwa dhidi ya jina lake katika kila orodha ya majina ambamo majina yake yalikuwemo.

Usiku wa tarehe 3 Februari mwaka huu kiasi cha saa 7.30 wakati Levina alipokuwa kitandani akijisomea alisikia mlango ukigongwa. Kabla hajajibu, mlango ulifunguliwa na Omari Saloti aliingia kwa nguvu chumbani. Walipigana. Levina alimng’ata mkono naye alimpiga ngumi za mashavuni na kwenye matiti. Levina alikimbia akiwa amevaa gauni ya kulalia tu na akajificha kwenye kichaka kilichoko nje ya bweni wakati Saloti akiwa bado anamnyemelea. Aligonga nyumbani kwa mlinzi, ambaye alimsindikiza hadi chumbani kwake na akasubiri kwa muda nje.

Madhumuni hasa ya PUNCH ni kuwadhalilisha wanawake

Inasemekana kuwa Saloti alitaka kumbaka, wakati wengine wanasema alimbaka. Wanasema Levina alikataa tu kusema. Hata hivyo Saloti alikuwa amemtishia Levina kuwa angembaka na kumwibia vitu vyake. Asubuhi iliyofuatia, mlinzi alisema kuwa alizungumza na saloti na akasema alikuwa “Amelewa” wakati huo. Levina pia aliwona meneja wa bweni, ambaye alizungumza na Saloti. Alisema kuwa Saloti alimwambia kuwa alifunguliwa mlango na Modesta mwenzake Levina ambaye walikuwa wakiishi naye chumba kimoja. Modesta, alikanusha madai hayo kwani yeye ameoloewa na kila mwisho wa juma huwa nyumbani na familia yake.

Dkt. Masanja alisema alimpa barua Levina na kumwelekeza kwa Mshauri wa wanafunzi, Dkt. Biswalo ambaye alikuwa akienda kwenye Mkutano wa Baraza hivyo naye alimelekeza kwa Mama Rajabu. Waliitisha jalada la Meneja wa bweni/Mlinzi lakini halikuwa na chochote. Levina alifariki jioni ya tarehe 7, Februari 1990. Inaonekana kuwa kundi la Punch ni mabingwa wa vita vya kisaikolojia na wamefanikiwa lengo lao kinyume cha matarajio yao kwa kumkatisha tamaa Levina mpaka akaona kuwa maisha yake hayana maana tena. Zaidi ya hayo utu wake ulikuwa umedhalilishwa na jitihada za Saloti za kutaka kumbaka [Maana katika jamii ya Kitanzania inaaminika kuwa mwanamke akibakwa amependa mwenyewe].

Kutokana na Punch kuwalazimisha marafiki wa Levina wamtenge, kumdhihaki mbele ya kadamnasi, kumdhalilisha na kumuonea, kutokana na malalamiko yake kutoshughulikiwa na MUWATA kwa kumwambia kuwa hakuna awezaye kushindana na Punch, wakati wengine walikuwa wakimcheka tuu anavyolalamika na rafiki zake wakimuepuka, yote haya yamemfanya alazimike kukata maisha yake kwani aliamini jamii nzima ilikuwa dhidi yake.

Punch ilifanikiwa kuondoa umoja kati ya wanawake. Saloti alifanikiwa kumkosanisha Levina na Modesta, mtu pekee ambaye ndiye alikuwa akimwamini, kwa kudai kuwa yeye ndiye alimpa ufunguo. Ukweli ni kwamba funguo zote za Hall 7 [alimokuwa akiishi Levina] ziliweza kufungua angalau milango mitano, wakati katika Hall 3 bweni lingine la wanawake ufunguo mmoja unafungua milango yote ya gorofa hiyo. Walimfuatafuata na kumgongea mlango usiku wa manane, walimtupia maneno machafu na kumtishia mlangoni pake, walifanya aonekane kama ‘mwenda wazimu’ na asiyefaa.

Mkutano wa dharura wa wanafunzi wa kike wa Chuo Kikuu, wahadhiri, wafanyakazi na wakazi wengine kwenye kampasi uliotishwa tarehe 9 Februari ulikubaliana kuwa wanawake walilaumu uongozi kwa kukataa kuchukua hatua za kinidhamu wakati mambo kama hayo yalipotokea. Wanasema iliendelea hivyo hadi kufikia hatua ya kuwakatisha tamaa wahasirika wasichukue hatua za kisherina kushindwa kutoa ushauri unaofaa kwa wanafunzi.

Levina Shujaa

Walisema kuwa Serikali ya wanafunzi [MUWATA] imekuwa kimya ikiangalia tu na mara nyingine ilishirikiana na waovu hao. Walisema kuwa wanafunzi wa kike ambao walijaribu kupata msaada kutoka MUWATA walijikuta katika matatizo makubwa zaidi, maana walihubiriwa kuhusu ukubwa na uwezo wa Punch.

Zaidi ya hayo wakina mama walisema kuwa jumuiya ya wanafunzi wanaichukulia Michoro ya matusi ya Punch kama burudani muhimu na wanafunzi wanaonewa wametumbukia kutokana na mgawanyo na mbinu za utawala za Punch, wakati wasomi na uongozi wamekaa kimya wakihofia visasi kutoka kwa Punch ambayo ilikuwa, inatikisa jamii nzima. Wakina mama walikubiana kuwa, Levina “asipotee hivi hivi, sisi tumtangaze shujaa ambaye hatimae ameikomesha Punch”.

Hata hivyo wanaume wanaposikia haya wanacheka. Wanauliza, “kwa nini mmuite Levina shujaa? Alikuwa malaya! Alikula pesa za watu! Mlitaka ale tu halafu asilipe? Kwani yeye ni wa kwanza kujiua! Ni m.p.u.m.b.a.v.u. Alikuwa mdhaifu. Alikuwa mjamzito! Unyanyaswaji wa kijinsia ni jambo la kawaida, wanawake pia wanayanyasa kijinsia. Mwanafunzi mmoja alirukwa na akili kwa sababu alikataliwa na msichana.” hayo ni baadhi ya maelezo yanayotolewa na wanaume wetu ndani na je ya kampasi.

Hati zenye kuonyesha uso wa levina zilikuwa zimebandikwa fuvu la Punch. Aliyekuwa Waziri wa nchi asiye na Wizara Maalum, Mheshimiwa Getrude Mongella, alipozungumza kwenye mgahawa baada ya kunywa chai katika ‘high table’ alilaani unyanywasaji wa kijinsia huko Mlimani na kusema ni sawa na kitu kilichokuwa kinachemka na sasa kimepasuka baada yua kufikia kikomo. Mapambano ndiyo kwanza yameanza. Walakini mapambano hayo lazima yaenezwe katika asasi kwanza yameanza. Walakini mapambano hayo lazima yaenezwe katika asasi zote za elimu ya juu na sehemu za kazi. Lazima kuwepo na mapambano ya kitaifa dhidi ya uovu huu!

Makala hii iliandikwa na Chemi Che-Mponda.

Chanzo:http://african.lss.wisc.edu/swahili/...8_makala_1.htm

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA