Skip to main content

TAHADHARI KWA WAGONJWA WA KISUKARI





Papai
KAMA UNA KISUKARI CHUKUA TAHADHARI: NI MUHIMU KUJUA KWAMBA UNAKABILIWA NA HATARI MARA 3 ZAIDI YA KUKUMBWA NA SARATANI KULIKO MTU AMBAYE HANA KISUKARI.

Tafiti zinaonyesha kwamba kuna wakati saratani ni matokeo ya mchakato wa ukarabati wa seli zilizoharibika ndani ya mwili.
Tafiti hizi zinaonyesha kwamba mimba inapotungwa seli katika mimba hiyo changa hugawanyika haraka sana na kutengeneza makundi mawili ya seli zenye maumbile na kazi tofauti. 

Nanasi

Kundi la kwanza la seli hizo (Kiini tete, au embryo kwa lugha ya kitaalamu) huendelea kugawanyika na kubadilika likiwa safari kutengeneza kiumbe ambacho hatimaye kitazaliwa kama mtoto.
Hali kadhalika kundi la pili nalo hundelea kugawanyika na kubadilika na hatimaye kutengeneza kondo la uzazi (placenta) ambalo kazi yake ni kulizingira lile kundi la kwanza. 


Kila moja ya seli katika kundi hili la seli ambalo sasa limetengeneza kondo la uzazi ina gamba ambalo limebeba umeme hasi.
Seli hizi kitaalamu huitwa Trophoblasts. Kazi ya hizi Trophoblasts ni kutoa ulinzi kwa kiini tete kisiweze kushambuliwa na mfumo wa kinga za mwili za mama!
 Bila seli hizi chembechembe nyeupe za damu katika mwili wa mama ambazo huunda sehemu kubwa ya jeshi la kinga katika mwili wa mwanadamu zingeshambulia kiini tete hicho na kukiharibu kwa dhana kwamba ni adui ailiyeingia mwilini! Kinachotokea ni kwamba kwa kuwa chembechembe hizi nyeupe za damu nazo zimebeba umeme hasi kama zilivyo Trophoblasts, zinapokaribia eneo kiliko kiini tete umeme hasi wa Trophoblasts na ule wa chembechembe cheupe husukumana (repels each other) na hivyo kusababisha chembechembe hizo nyeupe kusogezwa mbali na kiini tete.
 Tafiti zinaonyesha kuwa ulinzi huu wa Trophoblasts hukoma ghafla katika juma la nane la ujauzito.

Tafiti zinaonyesha kuwa sababu ya hatua hii ni kwamba katika kipindi hiki kiumbe kinachoendelea kukua na kubadilika tayari kina ngongosho linalofanya kazi na kongosho hili huzalisha kiasi kikubwa cha vimeng’anyo (pancreatic enzymes) ambavyo haviruhusu trphoblasts au chembechembe nyeupe za damu kutoka kwa mama kusogea katika eneo hilo. 

Vimeng’enya hivi vina uwezo wa kuchakatua na kuyeyusha protini (digest) hivyo basi chembechembe yoyote nyeupe katika eneo hilo, au seli ya trophoblast itaharibiwa kwa protini yake kuchakatuliwa na kuyeyushwa na vimeng’enya hivyo.

Tafiti zinaonyesha kuwa mwili unapositisha uzalishaji wa trophoblasts, chache ya hizi seli hubakia zikiogelea kwenye damu katika kipindi chote cha maisha ya kiumbe. Kazi ya hizi trphoblasts ni kusaidia katika ukarabati wa seli za mwili zinazoharibika kwa sababu mbalimbali.

 Katika eneo ambalo seli zimeharibika na zinahitaji kukarabatiwa seli chache za trophoblasts huenda katika eneo hilo na kuanza kugawanyika kwa kasi inayozifanya kuongezeka kwa wingi ndani ya muda mfupi, huku zikifanya kazi ya kusadia ukarabati. 
Tatizo linakuja pale ambapo uharibifu wa seli husika ni kitendo endelevu na pengine cha kudumu. Kwa mfano, kwa wavutaji wa sigara wa muda mrefu ambapo uharibifu wa seli za mapafu yao ni endelevu.
 Hii ina maana kwamba katika eneo husika trophoblasts zitakuwa zinajigawanya kwa kasi na zitaongezeka kupindukia mipaka (out of control growth).

Uchunguzi wa kimaabara unaonyesha kuwa seli za trophoblasts zinazojikuta katika mazingira ya aina hii hufanana kwa kila hali na seli za saratani! 

Hii imepelekea baadhi ya wanasayansi kuamini kuwa saratani chanzo chake ni nia nzuri na jitihada ya mwili kutaka kurekebisho kasoro zinazojitokeza katika seli za mwili. 
Jitihada zinapokwenda mrama kutokana na uharibifu katika seli husika kuwa endelevu basi saratani hujitokeza. 

Imethibitika kuwa vimeng’enyo vinavyozalishwa na kongosho (pancreatic enzymes) ni msaada mkubwa wa kuzuia trophoblasts kutengeneza saratani mwilini.

Ugunduzi huu ulifuatia jitihada kubwa za Dr. William D. Kelly wa kule nchini Marekani ambaye aliamini kuwa saratani ni zao la mwili kushindwa kuchakatua vizuri vyakula vya jamii ya protini kutokana na upungufu wa vimeng’enya vinavyozalishwa na kongosho, hususan vile ambavyo kazi yake ni kuchakatua na kuyeyusha protini (proteolitic enzymes).

Ili kuusadia mwili kufanya kazi hiyo kwa ufanisi Dr. Kelly alipendekeza mfumo wa tiba kwa wagonjwa wake ambao ulijumuisha marekebisho katika lishe, matumizi ya tiba-lishe (nutritional suppliments), na uondoshaji wa sumu mwilini. Dr. Kelly ambaye alipingwa sana na madaktari wa mfumo (conventional cancer doctors) alisafishwa na Dr. Nicholas Gonzales wa Newyork ambaye alifanya kazi kubwa ya kutafiti kesi moja moja ya wagonjwa wa Dr. Kelly kwa udhamini wa taasisi ya Memorial Sloan - Kettering Cancer Center. Ripoti ya kazi ya Dr. Gonzales, iliyokuwa na kurasa 500, ilithibitisha kuwa tiba ya Dr. Kelly ilikuwa kweli inafanya kazi katika saratani za aina nyingi mwilini.

Utafiti wa ziada uliofanywa katika kazi ya Dr. Kelly na wengine waliomfuata umethibitisha bila shaka kuwa uchache wa vimeng’enya vya kongosho ni sababu ya msingi ya kuibuka kwa saratani mwilini; na kuwa wagonjwa wa ugonjwa wa kisukari ambao kimsingi kongosho zao zinazalisha kiwango kidogo cha hivi vimeng’enya, wako katika hatari mara tatu zaidi ya kupata ugonjwa wa saratani.

Hii ina maana kuwa mgonjwa wa kisukari anatakiwa achukue tahadhari mara tatu zaidi kuliko mtu wa kawaida katika kulinda seli zake za mwili zisiharibike na kujenga mazingira ya trophoblasts kuzaliana kwa wingi. Uharibifu huu ni ule unaoweza kufanywa na uvutaji wa sigara, ulaji wa vyakula vilivyotunzwa kwa kemikali, matumizi ya vipodozi bandia (synthetic cosmetics), matumizi ya nyama zilizochakatuliwa na kuhifadhiwa kwa kemikali, matumizi ya nyama za kuchoma zilizoungulia na kufanya mkaa, nakadhalika. 

Aidha mgonjwa wa sukari anahitaji kutumia nyongeza/tiba- lishe (nutritional supplements) za vimeng’enya, hususan vile ambavyo kazi yake kubwa ni kuchakatua na kuyeyusha protini.

Vimeng'enywa vilivyotengenezwa viwandani wakati mwingine ni ghali kuliko uwezo wa walio wengi. Kama hali ni hii basi ni vema kula vyakula vinavyoweza kukupatia vimeng'enya hivi. 

Tunda kama papai ni chanzo kizuri sana ya kimeng'enya kinachoitwa papain. Kigogo kilichoko katikati ya tunda la nanasi ni chanzo kizuri sana cha kimeng'enya kinachoitwa bromelain.
 Kongosho bichi lililotoka kwenye mnyama mchanga ni chanzo kikubwa mno kwa vimeng'enya vya aina tofauti tofauti vya protini.

                     CREDIT :  HERBAL IMPACT

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA