Skip to main content

Tiba Asilia ya Maradhi Ya Saratani & Magonjwa Mbalimbali.





Pakaa mafuta ya HABBA SOUDA (Nigella oil seed ) mara tatu kila siku pamoja na kula kijiko kimoja cha unga wa HABBA SOUDA uchanganye katika juisi ya karoti (carrot) na ule kila unapomaliza kula. Endele kwa muda wa miezi mitatu.

Katika KITUNGUU THOUM (Garlic) muna kiinia kinachozuia Saratani (Cancer), kwa kila mgonjwa wa saratani anashauriwa ale kwa wingi kitunguu thoum na karoti (Carrot) kwa kuendelea.  Bila  shaka  atapata  matokeo  mazuri.

Chukua mkate wa nyuki kutoka mzingani moja kwa moja kiasi cha miligramu 100 kwa wiki mara moja, na kula asali pamoja na nnta yake kila siku kiasi cha kikombe kimoja, na sugua mwili wako kwa mafuta ya Habba souda, kisha oga kwa maji yenye uvuguvugu (warm water) na baadae kula asali iliyochanganywa na unga wa habba souda katika juisi ya karoti kila siku.

Dawa ya kizunguzungu na hata kuumwa na kichwa
Chukua Haba Sawda kisha kaanga na utie kwenye kitamba cheupe na uwe unanusa kila mara. Pia inasaidia kwa kuumwa na kichwa.

Kizunguzungu husababishwa na mambo mengi mfano:
1-Upungufu wa damu mwilini
2-kukosa kulala kwa uzuri
3-Mafikra yakizidi
4-Kukosa kula vizuri

Dawa ya Kuondosha weusi wa vipele vya uso
Kijiko cha chai kimoja -- Juice ya mbatata
nusu kijiko cha chai -- Unga wa Lozi
robo kijiko cha chai -- Manjano

Changanya vitu vyote pamoja kisha pakaa kwenye vipele vyeusi (usipake uso mzima kwenye vipele tu). Iwache kwa muda wa nusu saa au hata unaweza kulala nayo. Pakaa kila siku kwa muda wa wiki mbili. Baadae utapaka kwa wiki mara mbili mpaka uone umeondoka weusi utastop.

Wacha kula vitu vya gas kama masoda pia vyakula vyenye pilipili na vitu vya sukari.

Dawa ya chunusi za usoni

Chukuwa limau bichi halafu suguwa yaani jitiye katika sehemu za muasho. au chukuwa mafuta ya halzetu changanya kijiko kimoja kisha jipake sehemu yenye muwasho na kupasuguwana halafu iwache kwa muda kama wa saa moja kisha ukoshe kwa sabuni na maji, fanya hivyo mara moja kwa siku mpaka utapoana muwasho unaondoka

Au hi Dawa ya kutibu chunusi Usoni Chukua asali uchanganye na mdalasini ujipake usoni na shingoni uweke kwa muda wa nusu saa na baadae ukoshe kwa maji ya dafidafi (warm water). Pia unaweza kutumia maziwa yaliyochemshwa na uyatie ndimu/limau na uyaache kwa dakika kumi, kabla ya kulala ujipake usoni shingoni na hata mikononi.

Jisugue usoni na shingoni kwa kutumia kipande cha ndimu/limau na baadae changanya maji ya ndimu katika maji ya kawaida unawe uso.

Dawa ya Kusafisha uso

Kijiko kimoja kidogo unga wa mchele
Kijiko kimoja rob
Asali kijiko
nusu kijiko lozi ya unga.

chukua vitu vyote changanya pamoja pakaa kwenye uso wacha mpaka ikauke iwe kavu, baadae tia kidogo maji anza kusugua kidogo kidogo kama ukitia ( scrub) sugua baadae utakosha utaona uso wako laini fanya mara mbili kwa wiki

Dawa ya ugonjwa kwenye fizi ya meno

atafune chembe moja ya kitunguu saumu pale penye jaraha halafu akimaliza atie asali juu yake bila kuchelewa.Lakini ahakikishe hio asali iwe asali safi isiwe asali ya kutengeneza(feki).Na anapotia iwe anajaribu kuhakikisha kwa ulimi kama imefika pahala penye hilo jeraha.

Manufaa Za Kucheka

Manufaa za kucheka.
Wanasayansi wamekadiria kwamba kucheka kwa furaha kwa nusu dakika ni sawa na kupumzika kabisa kwa dakika 45. Kuangua kicheko kunalingana na kufanya mazoezi ya viungo kwa dakika tatu, hali kutabasanu kwa uchangamfu mara kumi ni sawa na kufanya mazoezi makali kama ya kuiga makasia kwa kutumia mashini kwa dakika kumi.

Manufaa mengine ya kucheka yanatia ndani kuongezeka mara tatu kwa kiasi cha hewa kinachovutwa ndani ya mapafu na vilevile kuborashwa kwa mzunguko wa damu, umeng'enyaji, kuyeyushwa kwa chakula, utendaji wa ubongo, na kuondolewa kwa vitu vyenye kudhuru.
"Napendekeza kwamba ili uwe mwenye furaha, jambo la kwanza unalopaswa kufanya kila asubuhi ni kutabasamu na kumwonyesha mwenzi wako na watoto wako tabasamu, kama huna hata jamaa zako.

" Jifunze kicheka unapokosea, na jaribu kuona mambo kwa njia nzuri hata wakati hali inapokuwa ngumu."
Makala  haya  yameandaliwa  na  Neema  Herbalist, tunapatikana  jijini  Dar  Es  salaam  kwa  simu  0766538384.

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA