Skip to main content

FAIDA ZA KIAFYA ZA MAFUTA YA NYONYO


Habari yako msomaji,
Natumaini uko vema, unaendelea na kusaka mahela hapa duniani lakini usimsahau MUNGU katika kusaka na kutumia mahela.
Leo tuyakumbuke haya mafuta mazuri mno, ya nyonyo. Wengi tunaoyafahamu haya mafuta tunayajua kwa kazi yake kwenye kutatua tatizo la kutopata choo; yanafanya kazi vizuri tu nyanja hiyo.

Mafuta ya Nyonyo katika Kukuza Nywele


Mafuta ya nyonyo yanakuza nywele haraka, ukiyapasha joto kidogo kabla ya kupaka, kisha unapaka kwenye ngozi ya kichwa na kuyatawanya vizuri katika ngozi taratibu kama una massage kichwa chako pia bila kupasha kule kumassage kunayongezea joto linayoyapa uwezo wa kupenya vizuri. Unapopaka na kutawanya vizuri unasaidia kuongeza mzunguko wa damu kichwani hivyo virutubisho vinavyoletwa na damu kukuza nywele zako vinafika kwa utoshelevu.  Mafuta haya yana virutubisho mbali mbali ikiwemo Omega 6 fatty acids ambazo huongeza virutubisho vinavyoleta afya katika nywele zako.

Iwapo unataka utumie kama conditioner basi ukimaliza kupaka  kwenye ngozi paka katika ncha zako pia kisha vaa kikofia cha plastiki kisha baadae uzioshe nywele zako vizuri kuondoa mafuta kwa kuwa ulipaka mengi kama conditioner.
Mafuta ya nyonyo ni mazito sana, iwapo utaona una nywele nyepesi na hutaki ziligee kwa uzito wa mafuta pale unapopaka basi changanya na mafuta mengine hasa mafuta ya nazi kwa uwiano wa 1:1.


Mafuta ya nyonyo yanatibu mba na matatizo mengine ya ngozi ya kichwa.


Mafuta haya huwa na sifa ya kuwa na uwezo wa kuua bacteria na fangasi ambao huweza kuleta matatizo yanayosababishwa na vimelea hivi ikiwemo mba.
Iwapo una nywele kavu na una mba basi changanya mafuta ya nyonyo na ya mzaituni kidogo kisha paka kichwani pako kwa mfululizo mpaka shida yako ipungue au iishe.
Iwapo una mba na nywele zina mafuta mengi basi changanya hivi: kijiko kimoja kimoja cha mafuta ya nyonyo, asali na ute ute wa aloevera na maji ya nusu limao. Paka kwenye mizizi ya nywele yani kwenye ngozi kaa nayo dakika 30 kisha osha mchanganiko utoke kwenye nywele yako.
Pamoja na kutibu mba michanganyiko hii hurutubisha nywele na kufanya zing'ae.

Yanajaza nywele Zako

Mafuta ya nyonyo yana omega 6 na omega 9 acids ambazo ni virutubisho vinavyosaidia katika afya ya nywele yako. Ukitumia mara kwa mara mafuta ya nyonyo yanasaidia kuotesha nywele na kuzipa nguvu(kuzinenepesha) nywele zako ambazo tayari ni ndefu.


Unaweza kutumia kama conditioner 

Unapaka na kuvaa plastiki kisha unaosha, unaweza kulala nayo kichwani mpaka asubuhi. Pia unaweza kuchanganya na conditioner au steaming yako unayotumia.


Yanarudisha mng'ao wa nywele zako

Iwapo utayachanganyana mafuta mengine au utayatumia yenyewe yana virutubisho vinavyoiacha nywele yako iking'aa.

Iwapo unasumbuliwa na ncha za nywele zako hii ni dawa

paka mafuta ya nyonyo kabla ya kuosha nywele zako na shampoo, shampoo inamaliza baadhi ya mafuta ya asili kwenye nywele na kukupa ncha kavu zinazosababisha kuchomoka nywele zako unapochana.

Yanasadia kutibu chunusi

Haya mafuta yana kiungo chenye uwezo wa kuua bacteria wanaosababisha chunusi.


Pishana na uzee kwa mafuta ya nyonyo

Yanasaidia kuondoa vikunyanzi vidogo vidogo usoni vinavyotokea kwenye ngozi ya watu wenye umri mkubwa. Imeonekana mafuta haya ya kirutubisho kinachosadia kubalance collagen katika ngozi yako, collagen ndio kirutubisho kinachotunza ngozi ya ujana.

Kuza kope na nyusi kwa mafuta ya nyonyo

Inasemekana yamekuwa na mafanikio pia katika kukuza/kujaza kope na nyusi.

kupaka machoni


Upatikanaji wake

Mafuta ya nyonyo yapo yanayochujwa kwa njia ya kawaida kama ya nazi, mbegu za nyonyo hupondwa na kupikwa. Kuna haya maarufu kama 'Jamaican Castor Oil' haya huandaliwa kwa kukaanga kwanza zile mbegu kisha yanachujwa hivyo hutoka meusi. ni vema upate yaliyoandaliwa kiasili yasiwe super refined au yameongezewa kemikali.
mmea wake( mti wa nyonyo)




mbegu za nyonyo(castor beans/seeds)

our black Castor Oil
Jamaican Version

Tahadhali

Mafuta ya nyonyo yana harufu kali hivyo unaweza kuchanganya na kitu kingine kama mdalasini au mafuta mengine kupunguza harufu.

                                Jaribu uone haya mafuta yanavyofanya kazi.

                                     CREDIT : www.centilicious.blogspot.com 

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA