Skip to main content

FAIDA ZA KIAFYA ZA MAFUTA YA NYONYO


Habari yako msomaji,
Natumaini uko vema, unaendelea na kusaka mahela hapa duniani lakini usimsahau MUNGU katika kusaka na kutumia mahela.
Leo tuyakumbuke haya mafuta mazuri mno, ya nyonyo. Wengi tunaoyafahamu haya mafuta tunayajua kwa kazi yake kwenye kutatua tatizo la kutopata choo; yanafanya kazi vizuri tu nyanja hiyo.

Mafuta ya Nyonyo katika Kukuza Nywele


Mafuta ya nyonyo yanakuza nywele haraka, ukiyapasha joto kidogo kabla ya kupaka, kisha unapaka kwenye ngozi ya kichwa na kuyatawanya vizuri katika ngozi taratibu kama una massage kichwa chako pia bila kupasha kule kumassage kunayongezea joto linayoyapa uwezo wa kupenya vizuri. Unapopaka na kutawanya vizuri unasaidia kuongeza mzunguko wa damu kichwani hivyo virutubisho vinavyoletwa na damu kukuza nywele zako vinafika kwa utoshelevu.  Mafuta haya yana virutubisho mbali mbali ikiwemo Omega 6 fatty acids ambazo huongeza virutubisho vinavyoleta afya katika nywele zako.

Iwapo unataka utumie kama conditioner basi ukimaliza kupaka  kwenye ngozi paka katika ncha zako pia kisha vaa kikofia cha plastiki kisha baadae uzioshe nywele zako vizuri kuondoa mafuta kwa kuwa ulipaka mengi kama conditioner.
Mafuta ya nyonyo ni mazito sana, iwapo utaona una nywele nyepesi na hutaki ziligee kwa uzito wa mafuta pale unapopaka basi changanya na mafuta mengine hasa mafuta ya nazi kwa uwiano wa 1:1.


Mafuta ya nyonyo yanatibu mba na matatizo mengine ya ngozi ya kichwa.


Mafuta haya huwa na sifa ya kuwa na uwezo wa kuua bacteria na fangasi ambao huweza kuleta matatizo yanayosababishwa na vimelea hivi ikiwemo mba.
Iwapo una nywele kavu na una mba basi changanya mafuta ya nyonyo na ya mzaituni kidogo kisha paka kichwani pako kwa mfululizo mpaka shida yako ipungue au iishe.
Iwapo una mba na nywele zina mafuta mengi basi changanya hivi: kijiko kimoja kimoja cha mafuta ya nyonyo, asali na ute ute wa aloevera na maji ya nusu limao. Paka kwenye mizizi ya nywele yani kwenye ngozi kaa nayo dakika 30 kisha osha mchanganiko utoke kwenye nywele yako.
Pamoja na kutibu mba michanganyiko hii hurutubisha nywele na kufanya zing'ae.

Yanajaza nywele Zako

Mafuta ya nyonyo yana omega 6 na omega 9 acids ambazo ni virutubisho vinavyosaidia katika afya ya nywele yako. Ukitumia mara kwa mara mafuta ya nyonyo yanasaidia kuotesha nywele na kuzipa nguvu(kuzinenepesha) nywele zako ambazo tayari ni ndefu.


Unaweza kutumia kama conditioner 

Unapaka na kuvaa plastiki kisha unaosha, unaweza kulala nayo kichwani mpaka asubuhi. Pia unaweza kuchanganya na conditioner au steaming yako unayotumia.


Yanarudisha mng'ao wa nywele zako

Iwapo utayachanganyana mafuta mengine au utayatumia yenyewe yana virutubisho vinavyoiacha nywele yako iking'aa.

Iwapo unasumbuliwa na ncha za nywele zako hii ni dawa

paka mafuta ya nyonyo kabla ya kuosha nywele zako na shampoo, shampoo inamaliza baadhi ya mafuta ya asili kwenye nywele na kukupa ncha kavu zinazosababisha kuchomoka nywele zako unapochana.

Yanasadia kutibu chunusi

Haya mafuta yana kiungo chenye uwezo wa kuua bacteria wanaosababisha chunusi.


Pishana na uzee kwa mafuta ya nyonyo

Yanasaidia kuondoa vikunyanzi vidogo vidogo usoni vinavyotokea kwenye ngozi ya watu wenye umri mkubwa. Imeonekana mafuta haya ya kirutubisho kinachosadia kubalance collagen katika ngozi yako, collagen ndio kirutubisho kinachotunza ngozi ya ujana.

Kuza kope na nyusi kwa mafuta ya nyonyo

Inasemekana yamekuwa na mafanikio pia katika kukuza/kujaza kope na nyusi.

kupaka machoni


Upatikanaji wake

Mafuta ya nyonyo yapo yanayochujwa kwa njia ya kawaida kama ya nazi, mbegu za nyonyo hupondwa na kupikwa. Kuna haya maarufu kama 'Jamaican Castor Oil' haya huandaliwa kwa kukaanga kwanza zile mbegu kisha yanachujwa hivyo hutoka meusi. ni vema upate yaliyoandaliwa kiasili yasiwe super refined au yameongezewa kemikali.
mmea wake( mti wa nyonyo)




mbegu za nyonyo(castor beans/seeds)

our black Castor Oil
Jamaican Version

Tahadhali

Mafuta ya nyonyo yana harufu kali hivyo unaweza kuchanganya na kitu kingine kama mdalasini au mafuta mengine kupunguza harufu.

                                Jaribu uone haya mafuta yanavyofanya kazi.

                                     CREDIT : www.centilicious.blogspot.com 

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na...

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ...

FAIDA KUMI ZA MTI WA MKOMAMANGA

Mti   wa   Mkomamanga   ni   mti   wenye   faida   nyingi   sana   katika   afya   ya   mwanadamu. Mti   huu   una   virutubisho –afya     mbalimbali   ambavyo   ni   muhimu   katika   afya   ya   mwanadamu.   Virutubisho   hivyo   vinapatikana   kwenye   magome, majani, mbegu, maganda   ya   matunda, juisi   ya   matunda   pamoja   na kwenye   maua   ya   mti   wa   mkomamanga. Zifuatazo   ni   faida   muhimu   za   mti   wa   mkomamanga : 1.           Maganda   ya   tunda   la   mkomamanga   yakichemshwa    hutoa   juisi    ambayo   hutumika   kama   dawa   ya   kufunga   kuhara. 2.   ...