Skip to main content

KILIMO CHA MMEA WA ROZELA







Utangulizi



• Rosella ni mmea wenye virutubisho vingi km vitamini, na madini ya chumvichumvi
• Hutumika kutengenezea juisi, jam, jellies, sauces, na mvinyo (pombe)
• Hutumika kuukinga mwili na magonjwa km saratani, ini na ukosefu wa lishe
• Unapunguza rehamu, unatibu presha
• Mmea wa Rosella wenye maua mekundu hujulikana kama choya-Dodoma
• Huitwa mkakaka(pwani) na wengine huutumia kama kiungo cha mboga(ndimu)
• Majani yake yanaweza kuliwa kama mboga vilevile
• Ni zao la biashara na hutumiwa nyumbani Mrosela
• Mmea huu hukua na hufikia urefu wa mita 3.5 kwa msimu
• Mti pamoja na matawi yake vimenyooka • Majani yamepishana kimpangilio na kugawanyika katika sehemu 3 – 7 pembeni yakiwa kama msumeno
• Una rangi ya kijani, nyeusi hadi nyekundu
• Maua ni makubwa yenye rangi nyekundu hadi njano
• Una mzizi mrefu na hutoa maua wakati wa kiangazi.
• Pia unavumilia ardhi yenye tindikali ya juu na ya chini pamoja na magonjwa

Aina  Za  Rozela

• Kuna aina 2  za  Rozela
i.                   : – Hibiscus sabdariffa yenye vikonyo vya rangi nyekundu hadi njano ambavyo vinaliwa
ii.                 Hibiscus altissima Webster ambayo hupandwa zaidi kwa ajili ya kamba kamba (fibres) zake lakini vikonyo haviliwi

Mahitaji ya Mrosela
• Hali ya Hewa:
i.                   Maeneo ya tropiki yenye mvua kati ya 1500 – 2000 mm kwa mwaka
ii.                 Mwinuko wa hadi meta 600 kutoka usawa wa bahari
iii.              Inavumilia joto na hali ya unyevunyevu
iv.              Hupendelea udongo wa mchanga wenye rutuba ambao hupenyeka kwa urahisi
v.                 Hata hivyo unaweza kukua kwenye aina mbalimbali za udongo
vi.              Huhitaji palizi ya mara kwa mara ili kuondoa kivuli na majani
vii.            Huvumilia mafuriko, upepo mkali na maji yaliyotuama

·        Ulimaji  wa  Rozela
Uchaguzi wa eneo, utayarishaji wa eneo, uchaguzi wa mbegu
• Mahitaji ya bustani : vikapu, mbolea, udongo, mchanga
• Tifua ardhi vizuri kwenda chini kama sentimeta 20
• Piga mashimo ya ukubwa wa sm15 X sm 15 na kina cha sm 5
• Panda mbegu kilo 11 – 22 kwa hekta
• Ni vyema kupanda mbegu kwa mistari
• Palizi katika mwezi wa kwanza ni muhimu sana
• Mbolea za asili zinafaa kutumika na husaidia sana
• Mtindo wa kubadilisha mazao (crop rotation) hutumika hasa kwa ajili ya mdudu anayeshambulia mmea huu kwenye mizizi (root knot nematode) Heleredera radicicola
• Unaweza kubadilisha na mazao ya kijani kama kunde, mahindi
• Mashamba madogo nyumbani: – Panda mistari halafu ikisha ota punguza iwe katika mistari ya meta 1 x meta 1.
• Mashamba makubwa: – Mbegu zioteshwe kwenye kitalu halafu zipandwe shambani kwa upana wa meta1.3 hadi 2.6 na mistari ya upana wa meta 2-3.3 Magonjwa • Fungi: fangas (ukungu) mbalimbali hushambulia kwenye mizizi na majani – Nyunyiza dawa, fungicides Kumbuka: Uangalizi wa shamba unahusisha; – Palizi, Kukata mapukutu, kufyeka – Kunyweshea – Uwekaji mbolea – Uwekaji dawa kwa wadudu waharibifu

Uvunaji   wa  Rozela
• Uvunaji wa matunda na vikonyo hufanyika majuma 3 baada ya maua kuchipua.
• Inashauriwa vikonyo viondolewe baada ya kupika matunda
• Kwa Rosela ya kamba: kupanda hadi kuvuna ni miezi 3-4 na ivunwe wakati mimea inatoa maua –
Mimea ikatwe chini kabisa na kisha kuning’iniza ili kamba ziachane na mti – Kamba zioshwe na kuanikwa juani – Mashine zipo na zinaweza kutumika kwa ajili ya kutenganisha kamba na mti • Ukaushaji Unafanywa kwa kutumia – solar dryer – chekecheke – Kuanika moja kwa moja juani – Kutumia majamvi kwa kukaushia matunda yenye mbegu
Maandalizi:
• Andaa turubai, jamvi, mkeka nk
• Bandua vikonyo
• Hifadhi matunda yenye mbegu Kuhifadhi
• Weka rosela iliyokauka kweye mifuko safi ya nailoni au viroba
• Hifadhi mifuko kwenye chumba kisafi chenye mzunguko mzuri wa hewa na kisiwe chenye unyevunyevu
·        Uvunaji wa kiuchumi
• Uvunaji wa vikonyo kilo 1.5-7.5 kwa mmea
• Kilo 17000-19000 kwa hekta
• Uzalishaji wa kamba ni kg 1700 – 3500 kwa hekta
• Kiasi cha kamba kwenye rosela ni 5%
Matumizi ya Rosela – Majani, matunda, maua, vikonyo, mbegu, mizizi
i.                   Vikonyo vya matunda hutumika kutengenezea jams, jellies, sauces na mvinyo
ii.                 Vikonyo pia hutumika kuweka rangi na ladha kwenye vyakula
iii.              Majani machanga huliwa kama mboga
iv.              Mbegu hutumika kwa ajili ya kuongeza nguvu za kiume
v.                 Matunda yake yanaliwa
vi.              Kamba zake hutengenezea vitu mbali mbali
vii.            Rosela pia hutoa mafuta
viii.         Inatumika  kutengeneza  mvinyo  mzuri  sana.

Matumizi  Ya  Rozela  kama dawa asilia
i.                   Huongeza nguvu za kiume
ii.                 Hutibu magonjwa ya tumbo, majipu, matatizo ya moyo, kikohozi, kansa (vikonyo), homa homa, na magonjwa ya akili
iii.              Hupunguza kiwango cha kulewa kwa mtu anapokunywa pombe
iv.              Maua yake ni mazuri sana katika kupunguza lehemu ( Kolestrol ) kwenye damu.

·        Hitimisho
Rozela  ni zao lenye matumizi mengi yenye faida  licha  ya  kutumika  kama  chakula, lakini  pia  linaweza  kutumika  kama  zao  la  biashara  na  hivyo  kutengeneza  nafasi  nyingi  za  ajira.  Ewe  kijana  mjasiriamali, una  ngoja  nini ? Anza  sasa, lima  Rozela,upate  ubadilishe  maisha yako.



Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA