Skip to main content



Majani  ya  mti  wa  mwarobaini.
Mti  wa  mwarobaini.
TUMIA  MWAROBAINI  KUJITIBU  MAGONJWA  YA  NGOZI.

Mwarobaini (Azadirachta indica) ni mti unaofahamika kwa uwezo wake wa kutibu magonjwa ya aina mbalimbali. Inaaminika kuwa mti huu umetoka huko India  na Burma . Mwarobaini hushamiri zaidi katika nchi za tropiki  na una uwezo mkubwa wa kuhimili ukame. Nchini  Tanzania, mti  wa  mwarobaini  huweza  kupatikana  kwa  urahisi  kabisa  katika  maeneo  mengi  ya  mijini  na  vijijini.

Jina “mwarobaini” linatokana na imani kuwa mti huu una uwezo wa kutibu magonjwa yapatayo arobaini. Majani na mbegu za mwarobaini vimekuwa vikitumiwa kama tiba kwa miaka maelfu  katika  nchi  mbalimbali  duniani.

Kati ya magonjwa ambayo mti huu umetumika kutibu au kupoza ni pamoja  na  matatizo ya kusaga chakula tumboni, kisukari, kansa, magonjwa ya ngozi, malaria, ukungu (fungus), n.k. Matawi yake hutumiwa kama mswaki na magome yake hutumiwa kama dawa ya kusafisha meno.

Mafuta ya mibegu ya mwarobaini hutumika kutengenezea vipodozi na sabuni. Kiziduo cha mibegu au mafuta yake hutumiwa kama dawa ya kuulia wadudu wanaoharibu mimea shambani.

Tumekwisha   ziona  faida  mbalimbali  za  mti  wa  mwarobaini,  leo  nitakufundisha  namna  ya  kutumia  mti  wa  mwarobaini  kujitibu  magonjwa  ya  ngozi.

 

                        MAHITAJI :

i.             Majani  ya  mti  wa  mwarobaini.

ii.          Sufuria

iii.        Mwiko

iv.         Jiko  la  gesi, mkaa  au  jiko  la  mafuta.

                       HATUA   ZA  KUFUATA:

1.  Chukua   majani  mabichi   ya  mti   wa  mwarobaini  na  uyaweke   kwenye   sufuria.

2.  Chukua  sufuria   yako  yenye  majani  ya  mti  wa  mwarobaini  na  ui injike  kwenye  jiko lenye  moto  wa  wastani.

3.   Chukua  mwiko  wako  na  uanze  kuyakoroga  majani  yako  taratibu  hadi  yakauke   bila  kuungua.

 

Majani  yako  yakiisha  kauka, ipua sufuria  yako, chukua  majani  yako  yaliyo  kauka, yasage  kisha  hifadhi  unga  unga  wako  kwenye  chombo  cha  plastiki.

                              MATUMIZI :

Tumia    vijiko  viwili  vya  chai  kwenye  kikombe  cha  robo  lita  chenye  maji  ya  moto, mara  mbili  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  ishirini  na  moja.


UTAPATA  MATOKEO  MAZURI   SANA. NGOZI  YAKO  ITAKUWA  LAINI, NYORORO  NA  YENYE  AFYA.

Makala  haya  yameandaliwa  na  NEEMA  HERBALIST  &  NUTRITIONAL  FOODS  CLINIC.  Kwa  taarifa  zaidi  kuhusu   huduma  zetu wasiliana  nasi  kwa  SIMU : 0766538384.

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA