Skip to main content

MTUMISHI WA MUNGU ANUSURIKA KATIKA AJALI KIMIUJIZA!!!!




Rev. John  Komanya.
Mwimbaji anayetamba na wimbo wa "Zawadi gani nitamtolea BWANA" ambaye pia ni mtume akichunga kanisa jijini Dar es Salaam John Komanya amepata ajali mbaya juzi mchana maeneo karibu na daraja la Mto Wami akiwa njiani kuelekea mkoani Arusha kukutana na viongozi wanaohudumu na mwalimu Christopher Mwakasege, kwa ajili ya mkutano wa injili ambao utakuwa na lengo la kuombea taifa kwa siku nne mwezi Disemba.






Akizungumza na GK mtume Komanya amesema lengo lilikuwa ni kupeleka barua kwa viongozi hao ili wamfikishie mwalimu Mwakasege kwaajili ya mkutano huo. Amesema akiwa njiani katikati ya Msata na Wami na wakati huo hakuwa amefunga mkanda wa gari, ndipo akasikia sauti ya Roho Mtakatifu ikimwambia kwa upole afunge mkanda lakini akawa anapuuzia na kuanza kujiuliza kwanini, sauti ikarudia tena kwa upole ikimwambia afunge mkanda akiwa bado anajiuliza ndipo anasema akasikia sauti ya Mungu ikizungumza kwa haraka na ukali "John funga mkanda" ndipo akafunga mkanda.
Mtume Komanya amesema akiwa anateremka kuelekea wami akiwa katika mwendo wa 180 wakati akipita katika kona kulikuwa na malori matatu mbele yake kukawa na lori lingine likifuatiwa na mabasi matatu yakipandisha kutoka Arusha kuja Dar, kwa wakati huo aliona malaika saba ambapo walishuka mithili ya makomandoo washukavyo kutoka kwenye kamba ya helikopta, mmoja akiwa amekaa kwenye boneti mbele, mwingine kulia, kushoto na mwingine nyuma yake ambaye alimwambia Komanya afuate maelekezo yake, anasema akiwa anamwangalia malaika aliyekaa karibu naye katika kiti cha dereva aliambiwa afuate maelekezo anayopewa na malaika wa nyuma yake.
Alipokuwa akiangalia mbele akaona gari linayapita mengine kwa spidi hali iliyomfanya Komanya kutaka kuingia katikati ya magari mengine lakini malaika akamwambia afuate maelekezo yake na kuambiwa aachie uskani jambo ambalo alilipinga kwakuwa aliona kifo mbele yake na kutaka kuingia katikati ili kukwepa, lakini malaika akamwambia ukiingia katikati utakufa, wewe achia usukani kama ninavyokwambia kwakuwa wametumwa kumlinda, akawa bado anatafakari kutokana na kuliona korongo kubwa upande wake huku malaika wakimwambia asiguse kitu chochote ikiwemo kutokanyaga breki lakini bila kusikia akakanyaga na kusababisha gari kuyumba sana, malaika akamwambia tena aachie breki na kuweka mikono yake kifuani. Anasema alipoweka mikono kifuani aliona wakiligonga lori huku malaika akiwa ameshika usukani na kuonyonga sana huku yeye akisema alijikuta akiwekwa kwenye kitu kama chupa ya maji, na yeye kwa wakati huo kuona kama vile yupo ndani ya glasi ya maji, ila anaona kinachoendelea.




Kisha baada ya hapo, upande wake wa usukani ndio uliogongwa, mara baada ya malaika kuchezesha usukani kidogo ili kuepusha madhara zaidi, na kisha ile semi-trailler ikamtupia kwenye korongo na kubinuka mara tatu hewani kabla ya kutua chini kwa mara ya nne, ambapo gari ilikuwa juu chini, yaani matairi yakiwa yanatazama juu.

Baada ya hapo kilichofuata ni kuendelea kusikiliza malaika wasemacho, ambapo hapo alisikia sauti ikisema fungua mkanada utoke, na kwa wakati huo kulikuwa na moshi ullioanza kutoka kwenye gari - na hapo akapewa dakika 12 kuchukua baadhi ya vitu alivyokuwa navyo kwenye gari. Maajabu ya Mungu, hakuna kitu chochote kilichogusa mwili wake, na wala hakuna damu iliyovuja kutokana na gari hilo kupindukia kwenye korongo.



Hakika utukufu ulimrudia Mungu kwa wakati huo kwani baadhi ya mashuhuda walikiri hapohapo ya kwamba hakuna mtu anayeweza kusalimika kwenye ajali hiyo, bali ni lazima tu mkono wa Mungu umehusika hapo kuokoa.

Baadhi ya mashuhuda ambao walikuwapo kwenye mabasi ya mkoa (hadi mkoa) walimtambua mtumishi wa Mungu ya kwamba ni John Komanya na hatumaye kumshukuru Mungu hapohapo, ambapo baadae Polisi walifika kwa ajili ya kazi yao - lakini hilo halikumzuia Mchungaji Komanya kupiga magoti na kumshukuru Mungu licha ya umati wa watu - na tukio hilo liliambatana na yeye kuisikia sauti ya Mungu ikimwambia "Nimekupa kazi ya kutengeneza kanisa langu,... usiogope nitakulinda, ila kuwa mwaminifu na nitakuweka kwenye uaminifu"

Sauti hiyo ilitoka kwa kiumbe ambacho kilikuwa na muonekano wa malaika, Pastor Komanya anaieleza GK na kusema kuwa sauti yake ilikuwa ya tofauti, na mavazi yake yalikuwa ni meupe na kwamba alielezwa dhahiri kuwa hiyo semi trailer ilikuwa imetumwa kummaliza, lakini ndio maana malaika walitumwa kumlinda.

"Zawadi Gani" kama ambavyo alikuwa akiitwa akiwa hospitali ya Muhimbili, alifanyiwa vipimo na kuonekana ya kwamba hana shida yoyote. Na hili linadhihirika hata pale alipotoka kwenye gari lililopiinduka, kwa kuwa alitoa vifaa vyake na kuanza pia kupiga picha, picha ambazo kama mtu akiziona zote, hakika hawezi kuamini kama kuna kusalimika hapo.

Mwisho wa yote Mchungaji Komanya anakiri kuwa amepona kwa rehema ya Mungu, na baada ya hapo amemuahidi kumtumikia kwa kazi aliyompa licha ya kwamba ni ngumu na ina vikwazo vingi. Jumapili hii, Mchungaji Komanya ataimba wimbo mpya kumshukuru Mungu kutokana na kumuepusha na kifo. Kwa wasafiri wote, hapa kuna funzo la kujikabidhi mikononi mwa BWANA kila mara safari inapotokea, katu tusienende kwa mazoea.

INATOKA :  www.gospelkitaa.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA