Skip to main content

Mwanamke Aeleza Kwa nini hataki kushiriki tendo la ndoa na mume wake.


Kwa miaka kadhaa Stacey alishindwa kufumbua fumbo la ni kwa nini hakutaka kushiriki ngono na mtu yeyete hata mumewe.
Inaaminika kuwa asilimia 1 hadi 3 ya idadi ya watu hawana hisia zozote za kingono.
Kwa miaka kadhaa Stacey alishindwa kufumbua fumbo la ni kwa nini hakutaka kushiriki ngono na mtu yeyete hata mumewe.
Kama anavyoelezea hapa ni daktari wake aliyemwambia ukweli.
Kwa muda mrefu sana nilidhani nina matatizo ya kiakili na kiumbile.
Nilihisi kwamba sio jambo la kawaida kutoshiriki ngono.
Marafiki zangu wangezungumza kuhsu marafiki zao wa kiume ama hata watu maarufu ambao wangependa kushiriki nao ngono lakini mimi sikuwa na mtu yeyote akilini ambaye nahisi tungeshiriki naye ngono.
Wakati nilipokuwa katika miaka yangu ya ishirini nilianza kuona tofauti niliyo nayo , lakini singeweza kuambia mtu yeyote kwa sababu yalikuwa mawazo, watanifikiria mimi sio mtu wa kawaida, kwa hivyo nikaamua kunyamaza.
Kutokuwa na hisia zozote za ngono ACE sio jambo la kawaida ijapokuwa mara nyengine uhisi kuvutiwa ki-mahaba.
Nilikutana na mpenzi wangu ambaye sasa ni mume wangu wakati nilipokuwa na miaka 19, na sikujua maana ya kutokuwa na hisia za kushiriki ngono, hivyobasi nilidhani niko nyuma na kwamba sielewi mambo.
Nilikuwa nikifikiria kwamba nampenda sana mwanamume huyu na iwapo atanichumbia nitakubali asiliia 100 kwa sababu najua ningependa kutumikia maisha yangu yote naye, lakini kwa nini sitaki kushiriki naye ngono? ni jambo la kushangaza.
Tulizuru maeneo mbali mbali na aliniambia kwamba yeye atasubiri hadi siku ninayohisi kushiriki ngono naye.
Alinisaidia sana na hakutaka kunilazimisha kufanya kitu ambacho sikupendelea.
Nilifanya makosa makubwa kwa kutafuta katika mtandao sababu za kimatibabu ambazo husababisha mtu kutokuwa na hisia za kushiriki tendo la ngono.
Maadili ya kijamii yanaelezea kwamba ngono na watoto ndio sababu ya ndoa na marafiki zangu wote walikuwa wakiolewa na kupata watoto.
Nilifikiri mungu wangu kuna hili tarajio kwamba ninafaa kushiriki tendo la ngono na mumewe wangu ili kupata watoto.
Nilianza kuota ndoto za ajabu kwamba mumewe wangu huenda ataniwacha kwa msichana mwengine anayefanana nami lakini ambaye atakubali kulala naye na ikafikia kiwango ambacho wasiwasi wangu nilishindwa kuuvumilia.
Nilifikiria, wajua nini? ni muhimu kusuluhisha swala hilo , nilitaka kujua ni nini kilichokuwa kikiendelea, wakati huo nikiwa kati ya miaka 27 ama 28.
Nilifanya makosa ya kufanya utafiti katika mtandao na hayo yalikuwa makosa makubwa sana, kulikuwa na mambo mengi ambayo yalikuwa ya kawaida kama vile homoni zilizokuwa zikitoweka mara kwa mara , lakini kile ambacho niliiona ni kuwa na uvimbe katika ubongo.
Nilisema, mungu wangu nitafariki kutokana na uvimbe katika ubongo.
Nilienda kwa daktari wangu na kusema, tazama ni hatari?, nitafariki?
Aliniambia, tulia una tatizo la kutokuwa na hisia za kushiriki ngono.
Nilisema, ni nini hiyo? nini?
Sijawahi kuhisi kile watu wengi hutaja kuwa na hisia za kingono.
Hivyobasi alinielekeza katika mitandao na hapo ndipo nilipokutana na watu kama mimi.nilifurahi.
Sikuwahi kusikia kwamba kuna watu wasiokuwa na hisia za ngono.
Nilifanya utafiti zaidi na kuanza kujihisi kawaida, hivyobasi nilizungumza na mume wangu kuhusu swala hilo.
Na alisema, nilidhani kwamba kila kitu kilikuwa sawa .
Amekuwa mtu mzuri sana, amekuwa akinielewa sana.Baadhi ya watu walio na tatizo kama langu walikuwa na haya ya kusema:
Nina umri wa miaka 60 na sijawahi kukutana na mtu mwengine ambaye yuko kama mimi. Sijawahi kusikia hadharani .
Nilipotambua kwamba sina hisia za kushiriki ngono nilizungumza na watu kadhaa na huku wengine wakijitokeza na kuliangazia swala hili kwa uwazi nimepata majibu mabaya sana.
Kundi moja la wachezaji wenzagu katika chuo kikuu waliamua kunipangia kwenda kujiburidisha usiku kwa lengo la kutaka nishiriki ngono walipogundua kwamba sijashiriki ngono bila kujali kwamba nilikuwa na tatizo.
Kuna watu wengi wasio na hisia za ngono ambao wanapoanza uhusiano na mtu mwengine wanashiriki ngono na wanaendelea kama kawaida , lakini kwangu mimi kila wakati ninapokaribi kufanya tendo hilo mwili wangu unakataa kabisa.
Ni utoto mwingi na watu ninapowaambia hushangaa na kuniuliza ni vipi unaweza kupata watoto.
Ijapokuwa kuna njia nyingi za kupata watoto iwapo ninataka, ni swala ambalo linawezekana.
Nimegundua tatizo lango kwa miaka mitatu sasa.
Nasherehekea kuwa mtu mwenye tatizo hili, nafurahia na napenda kuzungumza na wengine ili watu zaidi kuelewa na sio kuwahukumu watu wasio na hisia za kufanya ngono.
Nadhani iwapo ningejua kwamba nina tatizo hili nilipokuwa na miaka 18 ama 19 nadhani afya yangu ya kiakili ingekuwa bora wakati mwingi wa miaka yangu ya 20.
La kushangaza zaidi ni kwamba wakati kabla ya kugundua tatizo langu mume wangu alikuwa akiniita Stace Ace


CREDIT :  BBC  SWAHILI

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA