Skip to main content

Waziri aeleza chanzo cha wanawake kubakwa Zanzibar





Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Zanzibar, Balozi Amina Salum Ali amesema sababu kubwa ya wanawake wengi kubakwa wakiwa wanaokota karafuu ni kutokana na kujipamba vizuri wakati wakifanya kazi hiyo shambani.

Balozi Amina amesema hayo leo Jumatatu katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea Zanzibar wakati akijibu swali la nyongeza la Mwakilishi wa Kikwajuni, Nassor Salum Ali.

Mwakilishi huyo alitaka kujua kuna sababu gani za msingi kwa Serikali kupiga marufuku uokotaji wa karafuu za mpeta wakati zilikuwa zinawaingizia fedha watu hasa wanawake.

Akijibu swali hilo Balozi Amina amesema kutokana na malalamiko mengi ya wanajamii kwa kuibuka matendo ya ubakaji kwa wanawake wanaokota karafuu za mpeta ndio maana kwa makusudi Serikali imeamua kupiga marufuku uokotaji wa aina hiyo.
Utakuta wanawake wanatoka nyumbani kwao wakielekea Mkoani kuokota karafuu za mpeta huku wakiwa wamejipamba, hali ambayo huwa ni kishawishi kikubwa kwa wanaume kuwafanyia vitendo viovu vikiwamo vya ubakaji, hivyo upigaji marufuku huu tunaamini utasaidia sana kurudisha heshima za wanawake, amesema.
Amesema kutokana na agizo hilo Serikali imeandaa adhabu kali kwa yule atakayepigana na agizo hilo kwa kuchukuliwa hatua za kisheria.
 CREDIT : MWANANCHI NEWSPAPER


      MAKALA  NYINGINEZO
JINSI  KISUKARI  KINAVYO  SABABISHA  MARADHI  YA  NGUVU  ZA  KIUME


JINSI  KITAMBI  KINAVYO PATIKANA  NA  JINSI  UNAVYO WEZA  KUKIONDOA  KWA  TIBA  ASILIA


JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU  NA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME

IJUE  SAYANSI  YA  NGUVU  ZA   KIUME

UHUSIANO  KATI  YA  UNENE  ULIO  ZIDI  NA  TATIZO  LA  UKOSEFU  NA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZAP  KIUME


KISA  UGONJWA  WA  KISUKARI  MWANAMKE  AMKIMBIA  MUMEWE  WA  NDOA  NA  KWENDA  KUISHI  NA  JIRANI


KUTANA  NA  MWANAMKE    AIYE  JITOLEA  KUMTIBU   MUMEWE  MARADHI  YA  AJABU


PUNYETO  ILISABABISHA  NINUSURIKE  KWENDA  JELA

Comments