Skip to main content

ULEVI WA SHISHA : CHANZO CHA SARATANI YA MAPAFU





Watumiaji wa kilevi cha shisha wako katika hatari kubwa ya kuugua maradhi ikiwemo saratani na kuathirika katika mfumo wa hewa.




Wataalamu wa afya wameonya kwamba ulevi huo ambao kwa sasa umeshika kasi na kuteka watu wengi hasa vijana, una hatari kubwa kuliko uvutaji wa sigara.
Iinasadikiwa watu wengi, hususani vijana, hivi sasa wameibukia katika uvutaji huo, wakiamini ndiyo mbadala wa  sigara kwa kudhani kuwa haina madhara.

Daktari wa Kitengo cha Matibabu ya  Saratani, Hospitali ya Aga Khan, Dk Amiyn Alidina, alisema hayo  kwenye majadiliano ya ufahamu wa magonjwa ya saratani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.


Dk Alidina alisema kilevi hicho  hakina tofauti na sigara, ambayo mvutaji wake hawezi kukwepa magonjwa ya saratani, maradhi ya moyo na maradhi ya mfumo wa hewa.

"Shisha haiwezi kuwa mbadala wa sigara kwa kudhani kuwa mtu hawezi kupata saratani na magonjwa mengine, hii ni hatari zaidi," alisema.

Ulevi huo hutengezwa kwa kutumia chombo maalumu chenye bomba la kutolea moshi, ambacho huwekewa tumbaku, maji na moto huku ikiaminika mvuke husaidia kuchuja nguvu ya tumbaku inayoathiri mwili.

Kwa mujibu wa taarifa za Shirika la Afya Duniani (WHO), mkupuo mmoja wa shisha una kemikali hai  4,800 na kwamba kemikali hizo husababisha saratani ya mapafu, maradhi ya moyo na matatizo katika mfumo wa hewa.

Taarifa hizo za WHO  zinaeleza kwamba,  kiasi cha uvutaji wa shisha kwa saa moja ni sawa na kuvuta sigara kati ya 100 na 200.

Hii ni kutokana na kwamba, mvutaji wa sigara hupata mikupuo kati ya minane na 12 ambayo huingiza lita 0.5 hadi 0.6 za moshi. Lakini kwa upande wa shisha, taarifa hizo za wataalamu zinaonesha anaweza kuvuta mara 200, kiasi ambacho huingiza kati ya lita 0.15 hadi moja ya moshi.

Dk Alidina anafafanua kwamba saratani imekuwa tatizo kubwa ambalo kwa kiasi kingine huchangiwa na mtindo wa maisha ambao umefanya watu kushindwa kufahamu utaratibu wa kujikinga.

Wakati huo huo alisisitiza kwamba iwapo kwenye familia ipo  historia ya  watu wenye saratani, inatakiwa kuwa  waangalifu zaidi.
Miongoni mwa mambo ambayo jamii na familia kwa ujumla zinasisitizwa kuzingatia, ni ulaji wa matunda  na kuacha matumizi ya pombe na sigara. Mtaalamu huyo pia anahimiza  kufanya mazoezi ili kujiepusha na hatari ya kuugua saratani.

Wakati hapa nchini, hususani  jijini Dar es Salaam, lipo wimbi kubwa la vijana wakiwemo wasichana wanaojihusisha na uvutaji wa kilevi hiki katika baa mbalimbali, vile vile taarifa kutoka maeneo mbalimbali duniani, zinaonesha  kundi hili kutekwa na matumizi ya shisha.

“Uvutaji wa shisha unazidi kukua kwa sababu watu wengi hawajui madhara yake kama wanavyofahamu uvutaji wa sigara,” Profesa wa Chuo Kikuu cha London, Robert West, alikaririwa hivi karibuni na gazeti la Daily Mail la Uingereza.

Comments

Popular posts from this blog

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na...

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ...

FAIDA KUMI ZA MTI WA MKOMAMANGA

Mti   wa   Mkomamanga   ni   mti   wenye   faida   nyingi   sana   katika   afya   ya   mwanadamu. Mti   huu   una   virutubisho –afya     mbalimbali   ambavyo   ni   muhimu   katika   afya   ya   mwanadamu.   Virutubisho   hivyo   vinapatikana   kwenye   magome, majani, mbegu, maganda   ya   matunda, juisi   ya   matunda   pamoja   na kwenye   maua   ya   mti   wa   mkomamanga. Zifuatazo   ni   faida   muhimu   za   mti   wa   mkomamanga : 1.           Maganda   ya   tunda   la   mkomamanga   yakichemshwa    hutoa   juisi    ambayo   hutumika   kama   dawa   ya   kufunga   kuhara. 2.   ...