Skip to main content

KUTANA NA MWANAMKE BIKIRA MWENYE UMRI WA MIAKA 64.


Ngipeni, mwanamke  raia  wa  Afrika  Kusini, anaye  daiwa  kuwa  bikira  katika  umri  wa  miaka  64.



Ngipheni   kutoka   KwaMafunze ,Pietermaritzburg,Afrika  Kusini  ni  bikira  mwanamke  bikira  mwenye  umri  wa  miaka  64.  Alilazimika  kubaki  bikira  kwa  muda  wote  huo  kwa  sababu  hiyo ndio  ilikuwa njia pekee  ya  kushiriki  katika   ngoma za  utamaduni  wa  kabila  lake, ngoma  inayo  fanyika  kila  mwaka  kwa  ajili  ya  mfame  wao  Goodwill  Zwelithini ambaye  huitwa    Umkosi  Womhlanga.

Amekuwa  sehemu  ya  ngoma  hiyo  tangu akiwa teenager

“ Kabla  hatujaenda  kwenye  sherehe  za  ngoma, walezi  wetu   walitumia  kuhakikisha  kuwa  tupo  bikira  kwa  sababu  ngoma  hizo  ni  kwa  ajili  ya  wanawake  bikira “alisema .

Ingawa bado  yupo  bikira, Ngipheni anasema  amekuwa  akipata  hamu  ya  kufanya  mapenzi  kwa muda  mrefu.
  Njia  pekee  niliyo  itumia  kujizuia  na  hamu ya  kufanya  mapenzi, ni  kwa  kukumbuka  ushauri  wa  wazazi wangu kwamba  kupatwa  na  hamu  ya  kufanya  mapenzi  ni jambo  la asili  kwa  kila  mwanadamu.

Anasema  alipokuwa msichana, vijana  wengi  walijitokeza  kumchumbia. “ Wote  niliwatolea  nje  kwa  sababu  nilitaka  kuendelea  kuwa  bikira.”

Ngipheni  anatoboa pia  aliwahi  kuwa  na  rafiki  wa  kiume  ambaye  baadaye  alikuja  kuwa  mchumba  wake.


“ Enzi  zetu  wachumba  zetu  hawakuwa  na  haraka  ya  ngono. Walituheshimu  sana. Niliachana  na  mchumba  wangu  kwa  sababu  ali cheat.”

Ngipheni  anaongeza  kuwa  yupo  salama  na  magonjwa  ya  zinaa. Anasisitiza  kuwa  hamaanishi  kuwa  wasichana  wasifanye  mapenzi  au  wasiolewe.
“ Kama  unafanya    mapenzi, fanya  mapenzi  salama  na  ufanye  hivyo  baada  ya  kufunga  ndoa. Utakapo  funga  ndoa  mwambie  mume  wako  muende  mkapime  v.v.u.  Hii  itasaidia  kupunguza  kasi  ya  maambukizi  ya  v.v.u  pamoja  na  mimba  za  utotoni. “

Mlezi wa  Ngipheni, Zithobile  Mbhele  anasema  amefanya  kazi  na   Ngipheni  kwa  zaidi  ya  miaka  thelathini  na  anamsifu  kwa  kuwa   mfano  mzuri  kwa wanawake  wanaoishi  katika  jamii  yake.
CREDIT :  MASHIRIKA  MBALIMBALI  YA  HABARI


Comments