Skip to main content

Miongoni mwa sababu zinazowafanya wanawake kushindwa kubeba ujauzito



Siku chache zilizopita nilieleza kuhusu sababu kubwa zinazowafanya wanaume wengi kupoteza uwezo wa kutungisha mimba hata kama nguvu zao za jinsi zipo sawa.
Hata hivyo, utafiti unaonyesha kuwa hivi sasa asilimia kubwa ya wanaume husumbuliwa na tatizo hilo bila wao kujijua.
Lakini kutokana na maswali mengi niliyoyapokea, nawapongeza wasomaji wetu kwa mapokeo ya somo lile lililosababisha niandike makala haya.
Ni ukweli usiopingika kuwa tatizo la kupoteza uwezo wa kuzaa linawaathiri kwa kiasi kikubwa wanawake kuliko wanaume.
Wanawake wengi ndiyo waathirika wakubwa kuliko wanaume inapofikia suala zima la afya ya uzazi na matatizo yake kwa ujumla.
Dalili kubwa inayoonyesha mwanamke hana uwezo wa kuzaa inaanzia pale anapopoteza uwezo wa kushika mimba baada ya kujaribu kwa kipindi cha miezi 6 na kuendelea.
Kupata hedhi inayozidi siku 35 na kuendelea na kupata pia hedhi iliyo chini ya mzunguko (chini ya siku 21), kuyumba kwa tarehe za hedhi au kutopata hedhi kwa baadhi ya miezi, kuna tafsiri kwamba mwanamke anakosa urutubishwaji wa mayai yake.
Wanawake wengi wamejikuta wanaangukia kwenye matatizo haya kutokana na sababu mbalimbali ambazo wakati mwingine zinachangiwa na aina ya maisha wanayoishi au hata matatizo ya kurithi na kupatwa na aina nyingine ya magonjwa ambayo yanaenda kuathiri mfumo wa uzazi moja mkwa moja.
Sababu zinazowafanya kutoshika mimba
Sababu ya kwanza ni matatizo katika urutubishwaji wa mayai. Matatizo katika urubishwaji wa mayai yanajitokeza baada ya mayai yanayokua hayajakomaa kwenye ovari zake au ovari zenyewe zinashindwa kuachia mayai yaliyokomaa hadi tarehe ambazo mwanamke zinamruhusu kushika mimba. Kitaalamu, tatizo hili linaitwa premature ovarian failure.
Tatizo hili huwa linawapata wanawake wengi na ni vigumu kwao kushika mimba.
Dalili za tatizo
Zipo dalili zinazoashiria kuwa mwanamke ana tatizo hilo ambazo ni pamoja na kukosa baadhi ya mizunguko yake ya hedhi.
Nyingine ni pale anapokaribia kupata hedhi, hujisikia maumivu ya kawaida ya tumbo au maumivu ya kawaida au muwasho kwenye matiti na maumivu ya kiuno.
Sababu nyingine ni baadhi ya matatizo yanayojitokeza kwenye mfuko wa uzazi.
Hata hivyo, wataalamu wa magonjwa ya wanawake wanasema wakati mwingine tatizo la kutopata ujauzito husababishwa na mwanamke mwenyewe.
Kwani baadhi yao wana tabia ya kutoa mimba kiholela bila kujua kuwa kufanya hivyo kunaweza kuwasababishia matatizo kwenye mfumo wa uzazi.
Kwani wengi wao hutoa mimba bila kufuata ushauri wa wataalamu wa afya.
Tatizo hilo linapaswa kufahamika kwa wanawake wenyewe kuwa utoaji wa mimba na hasa mara kwa mara bila kufuata ushauri wa wataalamu wa afya au madaktari husababisha kuacha baadhi ya mabaki ya uchafu wa mimba zilizoharibiwa kwenye mfuko wa uzazi bila wao kujua.
Hivyo, si ajabu kwa mwanamke huyu akashindwa kushika ujauzito hapo baadaye atakapoamua kuzaa, kutokana na mfuko wake wa uzazi kuvurugika.
Lakini pia baadhi ya matatizo mengine yanayojitokeza kwenye mfuko wa uzazi ni uwapo wa uvimbe ambao kitaalamu huitwa fibroids.
Na wakati mwingine nje ya ukuta wa mfuko wa uzazi kunaweza kujitokeza baadhi ya tishu zinazojijenga kwenye ukuta wa mfuko wa uzazi.
Tishu hizo zikikua na kuongezeka zinaweza kumletea mwanamke tatizo la kushindwa kubeba ujauzito.
Tatizo hilo kwa jina la kitaalaamu linaitwa endometriosis na ni muhimu kupata ushauri wa daktari ili kuchunguza uwezekano wa kuwapo kwa tatizo hilo.
Endometriosis mara zote huambatana na dalili za maumivu makali wakati wa hedhi au wakatiwa tendo la ndoa au kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhi ikiambatana na mabonge mazito na maumivu kwenye mfumo wa uzazi hadi kwenye kiuno.
Ni vema kuwaona watoa huduma za afya ukiona dalili hizi mara moja.
Tatizo lingine ni mabadiliko yanayojitokeza kwenye mfumo wa homoni.
Wanawake wengi wanasumbuliwa na tatizo hilo bila kujijua. Kuyumba kwa uwiano wa mfumo wa homoni mwilini ni tatizo lingine ambalo kwa asilimia kubwa pia huwakumba wanawake.
Kisayansi, imethibitika kuwa kuyumba kwa mfumo wa homoni ni moja ya matatizo makubwa yanayowafanya wanawake washindwe kushika mimba.
Mchakato mzima wa upevushwaji na urutubishwaji wa mayai kwenye mfumo wa uzazi wa mwanamke kisayansi, unaratibiwa na mfumo wa homoni.
Hivyo, kuyumba kwa mfumo huo huathiri moja kwa moja mchakato mzima wa utungishwaji mimba.
Ni vema kumuona daktari kwa ajili ya vipimo kama ikitokea mwanamke anashindwa kupata ujauzito ili kubaini kinachosababisha tatizo hilo.
Sababu nilizozieleza ni chache kati ya nyingi zinazosababisha matatizo haya. Ushauri wangu ni kujenga ukaribu na watoa huduma za afya kwa ajili ya msaada wa uchunguzi na matibabu.


CREDIT : MWANANCHI NEWSPAPER
      MAKALA  NYINGINEZO
JINSI  KISUKARI  KINAVYO  SABABISHA  MARADHI  YA  NGUVU  ZA  KIUME


JINSI  KITAMBI  KINAVYO PATIKANA  NA  JINSI  UNAVYO WEZA  KUKIONDOA  KWA  TIBA  ASILIA


JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU  NA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME

IJUE  SAYANSI  YA  NGUVU  ZA   KIUME

UHUSIANO  KATI  YA  UNENE  ULIO  ZIDI  NA  TATIZO  LA  UKOSEFU  NA  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZAP  KIUME


KISA  UGONJWA  WA  KISUKARI  MWANAMKE  AMKIMBIA  MUMEWE  WA  NDOA  NA  KWENDA  KUISHI  NA  JIRANI


KUTANA  NA  MWANAMKE    AIYE  JITOLEA  KUMTIBU   MUMEWE  MARADHI  YA  AJABU


PUNYETO  ILISABABISHA  NINUSURIKE  KWENDA  JELA


Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA