Skip to main content

Dr. LWAITAMA ATOA UFAFANUZI KUHUSU KILICHO TOKEA KWENYE NDEGE YA PRECISION AIR



  
 
Dk.  Azaveli  Fedha  Lwaitama


Baada  ya  kuenea  kwa  habari  kuhusu Dr.  Azaveli  Fedha  Lwaitama  kupishana  kauli  na  wahudumu  wa  ndege  ya  Shirika  la  Precision  Air  ambako  kulipelekea  yeye ( Dk.Lwaitama )  kushushwa  kwenye  ndege  na  kwenda  kuhojiwa  kwa  masaa  kadhaa  kwenye  kituo   kidogo  cha  Polisi  cha  kwenye Uwanja  wa  Ndege  wa   Mwanza, hatimaye  Dr. Lwaitama  ametoa  ufafanuzi  kuhusu  kilicho  tokea.    Kwa  wale  mliokuwa  mnafuatilia  kutaka  kujua  kitu  gani  kilitokea, huu  hapa  chini  ni  ufafanuzi  wa  Dk. Lwaitama  ambao  ameutoa  kupitia  kwenye  mitandao  mbalimbali  ya  kijamii

Mwalimu  Lwaitama  :
 
Nawashukuru wote kwa kunipa pole. Wanasheria wa rafiki yangu binafsi Dr Antony Diallo, mmiliki wa Star Tv na Radio Free Africa, na wanasheria waliotumwa na Nd. Sungusia wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu
( Legal and Human Rights Centre, LHRC) chenye makao makuu Dar es Salaam walifika kituo cha polisi cha kiwanja cha ndege Mwanza na wakafanikiwa kuniwekea dhamana na hivyo niko nje kwa dhamana vinginevyo ningelala selo ndugu zangu _Kesho nitaripoti polisi kufuatilia juu ya kesi iliyofunguliwa dhidi yangu na Precision kanma itaenda mahakamani au vipi.

Kilichotokea kifupi ni hivi. Nilipanda ndege Flight PW 0492 iliyotarajiwa kuondoka Mwanza saa 3 dakika 50 asubuhi kuelekea Bukoba.
Nilikuwa nimekaa kiti namba 2B na mtafiti mmoja anayefanya kazi Maruku Tea Estate huko Bukoba alikaa kiti na. 2A kwenye dirisha kushoto kwangu. Wakati ndege inaanza kukuelekea inakoruka alikuja mhudumu wa kike akatuuliza na yule mwenzangu kama tunajua Kiingereza na mimi nikasema kwa utani huku nikicheka kuwa tunajua kidogo. Yule muhudumu gafla akatahamaki akasema kama sijui kiingereza aniamishe kiti.

Mimi nikamjibu kuwa hakukuwa na haja maana mimi najua kiingereza maana ni mwalimu wa siku nyingi wa Kiingereza lakini nilichokuwa nashangaa ni kwa nini nyie wahudumu mnapenda kutoa maelezo kwa Kiingereza wakati mgeyatoa maelezo hayahayo kwa Kiswahili mara baada ya kujua kuwa sisi ni Watanzania na tunajua Kiswahili vizuri zaidi kuliko Kiingereza. Binti huyo nikaona ametaamaki na kuanza kusema lazima niteremshwe.

Mimi nilidhani masihala maana niliwahi kutoa ushauri huu hapo nyuma kwa mhudumu mwingine wa Precision Air na yeye alinijibu kwa heshima kabisa kuwa wao maelezo wameambaiwa lazima wayatoe kwa Kiingereza.
Mara yule mhudumu wa kwanza akaondoka akaja mhudumu mwingine wa kike akasema kama sijui Kiingereza niamishwe nikamjibu wa taratibu na tabasamu langu la kawaida ninalolitoa katika mazingira kama haya ya dalili za kukosekana busara na mtoa huduma kukimbilia kwenye mambo ya kugombana bila sababu kuwa hakukuwa na tatizo jamani kwani Kiingereza nakijua na nilichokuwa nimempa mwenzake ni ushauri tu.

Yeye wala hata hakuzungumza na mimi tena aliondoka ndipo nikasikia rubani akitangaza eti kuna tatizo la kiusalama na ndege itachelewa kuruka ili litatuliwe. Mara polisi wane hivi na muhudumu wa Precision wa kiume mmoja wakaingia ndani ya ndege na kusimama mbele yangu nilipokuwa nimekaa na kufunga mkanda. Mhudumu akaniambia inabidi au nikuamishwe kiti au ni ushushwe.
Wakati huo huo wale polisi wakang'angania eti lazima nishuke.
Nikauliza nitii amri ya nanai sasa? Polisi mmoja aliyeonekana kama mwenye kuwaongoza wale polisi wenziwe akainama akanifungua mkanda wa kwenye ndge akaninyanyua mkuku mkuku na kunitoa nje ya ndege.Hata begi zangu mbili za mkononi ilibidi niombe nikiwa chini nipewe.

Abiria waliokuwa karibi na nilipokuwa walishangaa na kusema kwani amefanya nini huyu baba .
Lakini waliokuwa nyumba mabali hawakujua kilichotokea zaidi ya manaeno waliokuwa wamelishwa na rubani na wlae wahudu kuwa kuna baba kule mbele amnaleta fujo inabidi ateremshwe.
Nikapelekwa kituo cha polisi hapo uwajani huku nikisikia wakinongonezana kuwa lazima kuniweka selo (lockup ).

Nikafanikiwa kumpigia Dr Antony Dialo simu akazungumza nao wale askari na wakaanza kuchukua maelezo yangu nikiwa nimeketi ofisini kwao kwenye kochi walau badala ya kuwekwa lockup.
Baadaye nilipigia Ndugu Sungusia wa LHRC na Dr Antony Diallo wote wakanitumia wanasheria walionisaidia kuandika na kutia saini maelezo yangu. Wale wanasheria wakaniombea dhamana nikapata nikaruhusiwa kutoka pale kituoni lakini nikaamriwa kuripoti kituoni pale asubuhi kesho Jumatatu kwa maelekezo zaidi.

Wakati huo ndege ile ya Precision iliondoka ikaenda Bukoba na ikarudi tena baadaye kutoka Bukoba na ndipo nikamuona yule muhudumu wa kike wa pili eti ndiye anatoa maelezo juu ya eti mimi kufanya fujo. Yule muhudumu aliyewadanganya wenzake wote pamoja na rubani kuwa eti mimi nimefanya fujo wala hakutoka nje ya ndege iliporudi kutoka Bukoba kutoa maelezo.

Katika sakata lote ili yule abiria aliyeketi kushoto kwangu siti namba 2A wala hakuhojiwa na rubani wa ndege ile kujiahakikishia kama madai ya eti mimi kufanya fujo yalikuwa ya kweli na wala hata polisi waliotekereza maelekezo ya rubani yakuniondoa ndani ya ndege mkuku mkuku hawakujiangaisha kuuliza yule abiria jirani yangu aliye kuwa siti 2A kama ni kweli mimi nilifanya fujo yoyote au nilitoa maoni tu juu ya matumizi ya Kiswahili katika kutoa maelezo ya juu ya kipi cha kufanywa wakati wa dharura.

Hadi sasa bado sijaelewa kisa kilichomfanya yule mhudumu atahamaki na kunibambikizia tuhuma ya kufanya fujo yarabi... maana hakukuwepo hata na kubadirishana maneno kwa ukali kwa upande wake au wangu. Nimebaki nimeduwaha hadi sasa kuwa hivi ni kweli miaka zaidi ya 50 baada ya uhuru nimekatishiwa safari yangu kwa kutoa maoni tu ambayo mhudumu yule wa shirika la ndege binafsi angeweza kupuuza.
Bado sipati maelezo kwa nini haya yalinitokea zaidi ya kuhisi kuwa haya ni matokeo ya mfumo wa kuandaa wahudumu wa ndege wa Precision unaowavimbisha kichwa kuwa kwa kutamka kwa rubani kuwa kuna abiria anafanya fujo hiyo inatosha abiria yule kunyanyaswa kama nilivyonyanyaswa na kudhalilishwa kwa kutuhumiwa kufanya fujo ndani ya ndege.
Lazima nikiri hata hivyo kuwa maafisa Kadhaa wa kituo cha polisi cha uwanja wa ndege pale Mwanza walinionesha uungwana sana na walikuwa wakarimu kwangu kuliko hata wahudumu wale wawili wa Precsion Air.iyeketi kushoto kwangu siti namba 2A wala hakuhojiwa na rubani wa ndege ile kujiahakikishia kama madai ya eti mimi kufanya fujo yalikuwa ya kweli na wala hata polisi waliotekereza maelekezo ya rubani yakuniondoa ndani ya ndege mkuku mkuku hawakujiangaisha kuuliza yule abiria jirani yangu aliye kuwa siti 2A kama ni kweli mimi nilifanya fujo yoyote au nilitoa maoni tu juu ya matumizi ya Kiswahili katika kutoa maelezo ya juu ya kipi cha kufanywa wakati wa dharura. ondoka ikaenda Bukoba na ikarudi tena baadaye kutoka Bukoba na ndipo nikamuona yule muhudumu wa kike wa pili eti ndiye anatoa maelezo juu ya eti mimi kufanya fujo. Yule muhudumu aliyewadanganya wenzake wote pamoja na rubani kuwa eti mimi nimefanya fujo wala hakutoka nje ya ndege iliporudi kutoka Bukoba kutoa maelezo. o simu akazungumza nao wale askari na wakaanza kuchukua maelezo yangu nikiwa nimeketi ofisini kwao kwenye kochi walau badala ya kuwekwa lockup... Baadaye nilipigia Ndugu Sungusia wa LHRC na Dr Antony Diallo wote wakanitumia wanasheria walionisaidia kuandika na kutia saini maelezo yangu. Wale wanasheria wakaniombea dhamana nikapata nikaruhusiwa kutoka pale kituoni lakini nikaamriwa kuripoti kituoni pale asubuhi kesho Jumatatu kwa maelekezo zaidi. walishangaa na kusema kwani amefanya nini huyu baba . Lakini waliokuwa nyumba mabali hawakujua kilichotokea zaidi ya manaeno waliokuwa wamelishwa na rubani na wlae wahudu kuwa kuna baba kule mbele amnaleta fujo inabidi ateremshwe. Nikapelekwa kituo cha polisi hapo uwajani huku nikisikia wakinongonezana kuwa lazima kuniweka selo (lockup ). tena aliondoka ndipo nikasikia rubani akitangaza eti kuna tatizo la kiusalama na ndege itachelewa kuruka ili litatuliwe. Mara polisi wane hivi na muhudumu wa Precision wa kiume mmoja wakaingia ndani ya ndege na kusimama mbele yangu nilipokuwa nimekaa na kufunga mkanda. Mhudumu akaniambia inabidi au nikuamishwe kiti au ni ushushwe. Wakati huo huo wale polisi wakang'angania eti lazima nishuke. Nikauliza nitii amri ya nanai sasa? Polisi mmoja aliyeonekana kama mwenye kuwaongoza wale polisi wenziwe akainama akanifungua mkanda wa kwenye ndge akaninyanyua mkuku mkuku na kunitoa nje ya ndege.Hata begi zangu mbili za mkononi ilibidi niombe nikiwa chini nipewe.hi kutoa ushauri huu hapo nyuma kwa mhudumu mwingine wa Precision Air na yeye alinijibu kwa heshima kabisa kuwa wao maelezo wameambaiwa lazima wayatoe kwa Kiingereza. Mara yule mhudumu wa kwanza akaondoka akaja mhudumu mwingine wa kike akasema kama sijui Kiingereza niamishwe nikamjibu wa taratibu na tabasamu langu la kawaida ninalolitoa katika mazingira kama haya ya dalili za kukosekana busara na mtoa huduma kukimbilia kwenye mambo ya kugombana bila sababu kuwa hakukuwa na tatizo jamani kwani Kiingereza nakijua na nilichokuwa nimempa mwenzake ni ushauri tu. na haja maana mimi najua kiingereza maana ni mwalimu wa siku nyingi wa Kiingereza lakini nilichokuwa nashangaa ni kwa nini nyie wahudumu mnapenda kutoa maelezo kwa Kiingereza wakati mgeyatoa maelezo hayahayo kwa Kiswahili mara baada ya kujua kuwa sisi ni Watanzania na tunajua Kiswahili vizuri zaidi kuliko Kiingereza. Binti huyo nikaona ametaamaki na kuanza kusema lazima niteremshwe.ipanda ndege Flight PW 0492 iliyotarajiwa kuondoka Mwanza saa 3 dakika 50 asubuhi kuelekea Bukoba. Nilikuwa nimekaa kiti namba 2B na mtafiti mmoja anayefanya kazi Maruku Tea Estate huko Bukoba alikaa kiti na. 2A kwenye dirisha kushoto kwangu. Wakati ndege inaanza kukuelekea inakoruka alikuja mhudumu wa kike akatuuliza na yule mwenzangu kama tunajua Kiingereza na mimi nikasema kwa utani huku nikicheka kuwa tunajua kidogo. Yule muhudumu gafla akatahamaki akasema kama sijui kiingereza aniamishe kiti. awashukuru wote kwa kunipa pole. Wanasheria wa rafiki yangu binafsi Dr Antony Diallo, mmiliki wa Star Tv na Radio Free Africa, na wanasheria waliotumwa na Nd. Sungusia wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ( Legal and Human Rights Centre, LHRC) chenye makao makuu Dar es Salaam walifika kituo cha polisi cha kiwanja cha ndege Mwanza na wakafanikiwa kuniwekea dhamana na hivyo niko nje kwa dhamana vinginevyo ningelala selo ndugu zangu _Kesho nitaripoti polisi kufuatilia juu ya kesi iliyofunguliwa dhidi yangu na Precision kanma itaenda mahakamani au vipi.




Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA