Skip to main content

JE NI SAWA KUTOKUMPA MTOTO MAJI ADI AFIKISHE MIEZI 6?




Nianze lini kumpa mtoto wangu maji na nimpe kiasi gani ni swali ambalo kinamama wengi wenye watoto wachanga hujiuliza.
Mara Nyingi sana nimesikia kinamama wakijadiliana juu ya hili na kubadilishana uzoefu.Ingawa nimesikia wengi wakiliongelea kinachoshangaza ni kwamba sijawahi kusikia jibu moja ambalo naweza sema ndilo jibu sahihi au laa basi kuambiwa kwamba hili ndilo jibu sahihi na kupewa sababu za kuridhisha .
Kwakua lengo langu ni kukuza mapishi nyumbani na kuhakikisha afya ya familia iko vizuri,niliamua kufanya Utafiti  binafsi kwa kusoma vitabu,majarida na kuongea na baadhi ya madakitari wa watoto ninaowafahamu.Si kuishia hapo tu,nimeongea na akina mama waliolea watoto miaka yazamani na wanaolea watoto hivi sasa.Na haya ndio majibu niliyopata.
Majibu kutoka taasisi za afya.
Taarifa za wataalam wa afya kutoka kwenye  taasisi zinazoaminika duniani kama World health organization na Association of American Pedietrisions,zinasema Mtoto mdogo kati ya siku moja adi miezi sita(1-6)  hatakiwi kupewa maji wala chakula kingine chochote zaidi ya maziwa ya mama au maziwa maalum ya watoto(baby formula) au maziwa ya Ngombe.

                       

Wameelezea kwamba kiasi cha maji mtoto anachopata kwenye maziwa kinatosha kabisa .Kumpa mtoto maji si salama kwani yataharibu uwezo wa mwili wa mtoto kunyonya virutubisho kutoka kwenye maziwa.Maji pia yatafanya mtoto ashibe na ashindwe kunywa maziwa kwa kiasi kinachohitajika,Mbaya zaidi ni kwamba maji mengi kwa mtoto wakati mwingine huweza kuleta hali iitwayo water intoxication,hali hii huweza kumfanya mtoto azimie na wakati mwingine kuingia katika  coma.Hali hii huja pale ambapo wingi wa maji mwilini utapunguza kiasi cha sodium mwilini(low sodium concentration).
Taarifa inasema kwamba,ingawa unaweza kumpa mtoto maji baada ya miezi 6,wanashauri mtoto apewe maji kidogo na kwa kipimo maalum adi pale atakapo timiza mwaka mmoja ambapo anaweza kunywa maji kwa kiasi atakacho.
Majibu  kutoka kwa madaktari wetu.
Madktari wanne tofauti niliyobaatika kuongea nao,majibu yao yalifanana kwa kiasi kikubwa.Kwanza waliunga mkono taarifa za World health organization(taarifa hapo juu) .Lakini pili walikua na yao yakuongeza.
Walisema kwamba maziwa ya mama na formula zinamtosha mtoto endapo tu mtoto huyo anapewa maziwa yanayomtosha kushiba na yenye virutubisho vyote.Walieleza kwamba kina mama wengi hawanyonyeshi mtoto adi akashiba.Si kwasababu hawana maziwa au hawataki bali ni kwasababu hawajui mtoto anaitaji maziwa kiasi gani ili ashibe na anyonyeshe kwa muda gani ili mtoto apate kiasi hicho cha maziwa.Na kwasababu wakati mwingine maziwa  ya mama yenyewe hayana virutubisho vyakutosha kwani mama mwenyewe hali, au mwimili wake hauna virutubisho vyakutosha na wakati mwingine anapungukiwa baadhi ya virutubisho .
Walisema kua hali hii hufanya maziwa ya mama yasitoshe kabisa kwa mtoto na kulazimu mtoto aanze kupewa uji mwepesi mapema kabla ya miezi sita ili kufidia lishe yake.Na Pale tu unapoanza kumpa mtoto chakula zaidi ya maziwa basi  ni vyema ukaanza kumpa maji kwani uji na vyakula kama hivyo huesabika kama vyakula vigumu kwa mtoto.Moja alisema kwamba endapo mtu analazimika kumpa mtoto uji mapema basi  ni vyema mtoto afikishe angalao miezi minne.
Mwingine alisema kwamba,moja ya sababu zinazochangia kabisa kuwakataza kina mama kuwapa watoto maji ni pamoja na uwezekano mkubwa wa mtoto kupata magonjwa kutoka kwenye maji ya kunywa. Mara nyingi maji hayawi safi na salama.Alinieleza kwamba,magonjwa ya tumbo yanayoleta kuhara kwa mtoto ni moja kati ya magonjwa yanayosababisha vifo vya watoto  kwa haraka.
Majibu ya Mama aliyelea watoto miaka ya 60 –  80
Mama huyu aliyeanza kulea mtoto wake wakwanza mwaka 1967 alikua na haya yakusema.Alisema enzi zile walikua wanafundishwa namna ya kulisha mtoto kila wanapoenda kliniki.Alisema Walikua wakipewa karatasi yenye  picha za vyakula na majina ya vyakula hivyo na kuambiwa zaidi ya kunyonyesha ni lazima wawape watoto wao vyakula hivyo.Wakati mwingine walienda kwenye vikundi vya akinamama na kufundishwa namna ya kuandaa vyakula hivyo kwaajili ya mtoto.
Alinieleza kua vyakula hivyo viliwekwa kwa makundi,na kulikua na kundi lenye maji ya kunywa na maji ya matunda.Hivyo wao waliwapa watoto maji na maji ya matunda kama kadi ilivyoelekeza,aliniambia kua walikua wakipewa karatasi hizo miezi  miwili baada ya kujifungua.(akimaanisha mtoto akiwa na miezi miwili).
Kwa maana hiyo ,walianza kuwapa watoto uji,maji na maji ya matunda wakiwa na miezi miwili.
Majibu ya Mama anaelea watoto  hivi leo.
Niliongea na mama wawili tofauti,mmoja anawatoto wanne na mwingine ana wawili.
Mwenye watoto wanne,alisema watoto wake wote walianza kunywa maji na uji mwepesi wakiwa na miezi miwili.Alisema kwamba ingawa watoto wake walikunywa maziwa bila shida aliona wazi kabisa kwamba hawashibi na ndipo alipoamua kuongeza uji mwepesi kwenye lishe yao.
Alinieleza kwamba huandaa uji huo na kisha kuuchuja na kuhakikisha ni mwepesi kama maziwa na kisha kumpa mtoto kwenye chuchu kama anavyompa maziwa.Uji huo huandaliwa kwa maziwa,maji na unga.
Mwenye watoto wawili alikua na haya yakusema.Alisema kwamba watoto wake walikunywa maziwa tu adi walipofikisha miezi 6.Pale alipoona maziwa ya mama hayatoshi aliongeza maziwa ya ng’ombe ili kuhakikisha mtoto anashiba.
Alinieleza kwamba,ili kuhakikisha mtoto anakunywa maziwa kwa kipimo sahihi,alikamua maziwa yake kwakutumia pampu maalum na kuyaweka kwenye chupa ili apime kipimi sahihi.Na kwakua mtoto wake hushiba vizuri na wataalam husema mtoto asipewe maji basi hakua na sababu yoyote ya kumpa mtoto maji kabla ya wakati uliothibitishwa.



Mtizamo wangu
Baada ya kukusanya yote haya na kutafakari ,nimegundua kwamba pale ambapo mtoto anapewa chakula chochote zaidi ya maziwa basi ni sawa apewe maji  kwa kiasi Fulani,kwani tayari mwili wake unapokea chakula kigumu na huitaji maji zaidi.
Kwa upande mwingine,sioni sababu ya kumpa mtoto maji endapo anapata maziwa katika kiasi kilicho sahihi kwa mwili wake na anashiba.kinachonitia wasiwasi ni uwezekano wa  mtoto kupata maziwa yakutosha.
Kwa maisha yetu ya kitanzania Gharama ya kumlea mtoto kwa kumpa  maziwa ya kopo ni kubwa sana na wazazi wengi hawawezi mudu gharama hizo.Gharama za maziwa ya ng’ombe pia ziko juu na maziwa niyashida hasa kwenye miji mikubwa hivyo ni ngumu kwa mwananchi wa kipato cha kawaida na cha chini kufidia lishe ya mtoto kwa kuongeza maziwa hayo yakununua.Hii humlazimu mzazi kumuanzisha mtoto uji mapema ili kufidia lishe yake.Jambo linalopelekea mtoto kula chakula kigumu na kunywa maji akiwa chini ya miezi sita .
Hata hivyo ni vyema kujua kwamba ingawa kuna kiasi au kipimo Fulani cha maziwa ambacho mtoto anatakiwa kupewa si kweli kwamba watoto wote hushiba kwa kipimo hicho.Watoto hutofautiana ukubwa wa mwili kitu ambachi hufanya hata kula yao itofautiane.Kwa mantiki hiyo basi ni wazi kwamba watoto wa rika moja si lazima wapewe kipimo sawa cha maziwa,tofauti ya hatua tano juu ya kipimo cha kawaida huruhusiwa.
Ushauri
Nawashauri kina mama,kuongea na madaktari wa watoto juu ya wakati sahihi wakumpa mtoto maji.Ni vyema mkalijadili hili kwa pamoja na kuona wakati upi ni sahihi zaidi kumpa mtoto maji kwa kuzingatia ubora au mapungufu ya afya yake.Kumbuka tu kwamba ukosefu wa maji mwilini pia huzaa matatizo makubwa ya afya kwa mtoto.
Naamini makala hii imekupa mwanga juu ya swala hili,na hata utakapoongea na daktari basi unaweza bishana nae hapa na pale katika kuhakikisha anakupa jibu linaloeleweka.
Busara za Tolly.
Siku zote daktari wa watoto anapokwambia jambo,jifunze kumuuliza kwanini kakwambia hivyo au kwanini anaona hivyo.Mfano:Akikwambia usimpe mtoto maji ya adi afikishe miezi nane.Muuliza: Kwanini?.Hii itakusaidia kuelewa Jambo kwa undani.
MAJI NI UHAI

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA