Skip to main content

NAMNA YA KUONDOA ASIDI INAYOSABABISHA KIUNGULIA KWENYE MAHARAGE-Epukana na kiungulia na tumbo kujaa gesi.



Maharage ni moja ya vyakula ambavyo mimi hukwepa kula nje ya nyumbani ,naweza kula maharage nje ya nyumbani kwangu endapo tu ninauakika na ambavyo mpishi  kaandaa maharage hayo,kwa maana nyingine nakula kama yameandaliwa na ndugu,jamaa na marafiki ambao ninauhakika na uandaaji wao.
Hii yote ni kwasababu maharage yasipoandaliwa vizuri hunipa kiungulia kikali sana kwa muda mrefu na wakati mwingine tumbo hujaa gesi na kuninyima raha.
Maharage ni chanzo kizuri cha protini daraja B(protini itokanayo na mimea)na Nyuzinyuzi.

Asidi aina ya  Phytic au phytates ipatikanayo kwenye maharage ikutanapo na madini mwili kama zinc,copper,calcium,magnesium namadini  chuma husababisha tatizo la kiungulia na tumbo kujaa gesi kwa baadhi ya watu,tatizo hili huwasumbua zaidi wale wasiokula Nyama na vyakula vitokanavyo na wanyama(vegeterians)kwani vyakula  vyao  hua na asidi nyingi ya phytic.
Tafiti zilizofanywa na American Dietetic Association zinaonyesha kwamba huwezi toa asidi yote ya phytic kwenye maharage ila unaweza kuipunguza kwa kiasi kikubwa  kwa kuloweka maharage kwenye maji.
Wengi mnaloweka maharage kwenye maji ili kuyalainisha na kufanya yaive haraka wakati wakupika,Lakini msichojua ni kwamba kuloweka huko hupunguza  asidi ya Hyptic kwenye maharage  ambayo ni chanzo cha kiungulia kwa wengi,asidi hiyo pia hutonesha vidonda vya tumbo na kuleta maumivu makali kwa wale wenye tatizo la vidonda vya tumbo.
Ulowekaji wa maharage kwa muda mrefu
Watu wengi wamezoea kuloweka maharage usiku na kuyapika siku inayofatia,ikimaanisha yanalowekwa kati ya masaa manane hadi kumi na nane.Ingawa kuloweka huku kumezoeleka kwa wengi.
Tafiti  zinaonyesha kwamba,njia hii ya ulowekaji wa maharage ni hatari sana kwa afya kwani hutoa nafasi, mazingira sahihi na  muda mrefu kwa  vijidudu viletavyo magonjwa vipatikanavyo  kwenye maharage kuzaliana na kukua .
Ingawa maharage hupikwa kwa muda mrefu na kwa moto mkali bado haitoshi kuuwa vijidudu vya aina yote,bakteria watengenezao sumu au spore mara nyingi hubakia hai na huweza kua chanzo cha magonjwa kwa  mlaji wa maharage hayo.Ukiamua kutumia njia hii,basi loweka maharage na uyaweke ndani ya friji ili kupunguza uwezekano wa vijidudu hao kuzaliana kwenye maharage.
Ulowekaji wa maharage kwa muda mfupi-Njia iliyo bora
Kuloweka maharage kwa muda mfupi ni njia nzuri na bora zaidi ya kupunguza asidi ya phytic kwenye maharage,kwani huipunguza kwa kiwango kikubwa na kwa haraka zaidi kuliko njia ya kuloweka maharage kwa muda mrefu.

Njia hii fupi kwa upande mwingine haitoi nafasi ya vijidudu viletavyo magonjwa kuzaliana kwenye maharage,na huokoa muda kwani huchukua muda mfupi.
Ulowekaji huu huchukua kati ya saa moja adi manne na si zaidi,ni uamuzi wa mpishi kuchagua aloweke masaa mangapi,ata hivyo ni vyema kujua kwamba ukiloweka kwa masaa manne utatoa kiasi kikubwa cha phytic kuliko ukiloweka  kwa saa moja.
Njia.
1.Pima kiasi cha maharage unachotaka kuandaa/kupika,mfano:vikombe vinne.(nashauri utumie kikombe kupima)kariri idadi ya vikombe ulivyopima





2.Chambua maharage  ili kuondoa maharage mabovu,mawe na uchafu mwingine wowote



3.Osha maharage,adi yawe safi.


4.Kwa kutumia kikombe ulichopimia maharage ,pima maji mara mbili ya kipimo cha maharage na uweke kando.mfano:kwakua tumepima maharage vikombe vinne,tutapima maji vikombe nane.(vikombe vya maji,mara mbili ya vikombe vya maharage)



5.Katika sufuria weka maharage na kisha ongeza maji uliyopima


6.Bandika maharage jikoni yachemke kwa dakika mbili tu.Hesabu dakika mbili kuanzia pale yanapoanza kutokota na sio dakika mbili kuanzia ulipoyabandika jikoni.Epua jikoni baada ya dakika hizo kuisha.




7.Acha  kwa kati ya saa moja adi manne(kutokana na muda ulionao)

Muonekano wa maharage baada ya masaa manne

8.Chuja maji yote kwenye maharage.
 

Maji yaliyochujwa kwenye maharage.maji haya yamebeba phytic iliyotoka kwenye maharage.
9.weka maharage kwenye sufuria, ongeza maji ,bandika jikoni  kisha chemsha adi maharage yaive.

Maharage yaliyoiva,baada ya kuchemshwa
Baada ya kuivisha maharage ,unaweza kuyapika au kuyaunga  katika namna upendayo.
Maelezo ya ziada.
Ingawa  njia hii hupunguza  phytic  kwa kiasi kikubwa sana na hutosha kufanya mtu asipate kiungulia au tumbo kujaa gesi,kuna wale wenzangu ambao hata iyo hyptic kidogo sana iliyobaki kwenye maharage inatosha kuwapa kiungulia.Ipo namna ya kukata nguvu ya hiyo phytic kidogo iliyobaki na kufanya maharage yawe mazuri zaidi.Nitakueleza hilo katika makala ijayo.
Ipe familia yako  kilicho bora zaidi.






Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA