Skip to main content

UNENE UNAVYO MTESA BINTI HUYU



Grace Simon mwenye miaka 14 anateseka na uzito.
GRACE Simon mwenye miaka 14 anateseka na uzito wa kupindukia  wa kilo 111 (kama gunia moja la mahindi na viroba vitatu) hali iliyomsababishia akatishwe masomo na walimu katika Shule ya Msingi Amani, Ukonga, Ilala jijini Dar es Salaam alikokuwa anasoma.Grace ambaye mwaka huu angekuwa darasa la saba lakini aliachishwa shule mwaka 2010 akiwa darasa la nne na walimu wakimtaka akatibiwe.

MAMA MZAZI ASIMULIA
Akizungumza na Uwazi kuhusu mkasa mzima wa mtoto Grace, mama yake mzazi, Ashura Bakari alisema binti yake alimzaa salama mwaka 2000 lakini ilipofikia mwaka 2002 akiwa na miaka miwili alianza kuvimba tumbo hali ambayo hakujua chanzo chake.


ATENGWA NA WANAFUNZI
Mama huyo akizungumza kwa masikitiko alisema kuwa, Grace alipofika darasa la nne, akiwa na umri wa miaka kumi baadhi ya wanafunzi wenzake walianza kumnyanyapaa kutokana na unene ambao ulikuwa ukiongezeka siku hadi siku.
“Walikuwa wakimtania sana  mwanangu hadi kukosa amani. Hali hiyo iliwafanya walimu kumsimamisha masomo ili atibiwe. Hadi sasa sijapata msaada wa kupona kwake,” alisema mama huyo  huku machozi yakimtoka.



HOSPITALI ZIMESHINDWA?
Aidha, mama Grace aliongeza kuwa amekwishahangaika katika hospitali mbalimbali za jijini Dar es Salaam, ikiwemo Muhimbili bila mafanikio.
“Muhimbili waliniambia ili mwanangu aweze kufanyiwa vipimo pamoja na matibabu gharama zake ni shilingi laki nane (800,000) ambazo nimezikosa na hakuna mtu wa kunisaidia,” alisema.
NDUGU NAO
Alisema mbali na kutafuta tiba hospitalini, amekuwa akipita huku na huko kuomba msaada wa fedha kutoka kwa ndugu na jamaa lakini hakuna aliyemsadia.
KWA NINI BABA MZAZI ASIMSAIDIE?
Katika hali ya kushangaza, mama huyo alisema ili kupata fedha hizo anahangaika peke yake kwa sababu baba mzazi wa Grace, Simon alikataa kutoa msaada wowote.
“Baba yake yupo hai, alikuwa anatoa msaada kipindi cha mwanzo lakini miaka kama mitano imepita hakuna msaada anaonipa. Ni kweli hatuishi pamoja lakini mtoto tulizaa wote,” alisema kwa masikitiko makubwa mama huyo.
WALICHOKIONA MADAKTARI
Akizungumzia kiini cha tatizo, mama huyo alisema: “Kwa mujibu wa madaktari mwanangu anasumbuliwa na moyo kujaa mafuta mengi, kwa hiyo homoni zake zimekosa uwiano na ini pia lina sumu nyingi.”
GRACE  AWALILIA WATANZANIA
Akizungumza na mwandishi wetu, mtoto huyo anayetamani kuendelea kusoma aliwaomba Watanzania wamsaidie fedha ili aweze kutibiwa na kurejea darasani.
“Niliachishwa shule ili nitibiwe, nikipona nirejee shuleni, lakini hadi sasa sijapata nafuu, na ninajua ni kutokana na kutopata matibabu sahihi,” alisema Grace huku akilia.
UONGOZI WA SHULE 
Mmoja wa walimu waandamizi wa Shule ya Msingi Amani alipokuwa akisoma mwanafunzi huyo (hakuwa  tayari kutaja jina lake), alikiri kumtambua mwanafunzi huyo na kusema aliachishwa  shule kwa hofu ya uongozi wa shule.
“Hatukumwachisha shule kwa nia mbaya, lakini lengo letu lilikuwa akatibiwe kisha arudi shuleni lakini matibabu anayopata hajaweza kupona na hali aliyokuwa nayo inazidi kuongezeka siku hadi siku,” alisema mwalimu huyo.
Akaongeza: “Mwaka huu Grace ilikuwa awe darasa la saba, lakini hata kutembea ni tatizo hali ambayo tuliona kuwa unene ule si afya bali ni ugonjwa.”
MSAADA UNAAOHITAJIKA
Kwa yeyote aliyeguswa na tatizo la Grace ambaye anasaka shilingi laki nane tu ili atibiwe, anaweza kuwasiliana na mama yake mzazi  kwa simu: 0719 465445, ASHURA BAKARI.

CREDIT :  GLOBALPUBLISHERS


Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA