Skip to main content

MATUMIZI SABA YA BAKING SODA(MAGADI SODA)USIOYAJUA-magadi soda si chakula tu.



DSC06962
Leo asubuhi Dada yangu alinichekesha sana,alifanya siku yangu ianze vizuri pale aliponiletea kibao kichafu cha kukatia nyama alichobeba kutoka nyumbani kwake ili nimsaidie kukisafisha.Nilicheka sana kwani kila mara najitaidi kumfundisha mbinu mbalimbali za jikoni lakini hasikilizi.sasa leo yalipomfika,na kufikia hatua ya kutaka kukitupa kibao hicho ndipo alipokumbuka kua niliwai mfundisha namna ya kukisafisha.Akaamua kujibeba yeye na kibao chake  akanifata.Na ndipo hapo nilipomuweka kwenye darasa la vitendo kwa makubaliano kwamba siku nyingine sitamsaidia.
Najua wengi mnaifaham Baking soda au Bicarbonate of soda kwa lugha ya Kiswahili huitwa magadi soda ,kwa wale msioifahamu,Baking soda au bicarbonate of soda ni  hitaji la kawaida kabisa jikoni,hutumika sana katika vyakula vya kuhoka kama keki na mikatepia hutumika katika maandazi,pan cakes,chapatti na vyakula vingine vingi.Hata ivyo Baking soda wakati mwingine hutumika kulainisha vyakula ambavyo ni vigumu kuiva au visivyolainika haraka  vinapopikwa kama mahindi yasiokobolewa,mboga za majani za kienyeji kama mgagani, msusa,majani ya kunde yaliyo komaa na kadhalika.Hapa nchini Baking soda ya jina kubwa  na kufaamika kwa wengi inaitwa SIMBA.
Baking soda hupatikana kwa wingi madukani na hata sokoni.kuna ile ambayo imepita kiwandani na kusindikwa kitaalam na kuna ile ya kienyeji ambayo iko kiasili zaidi.
Siri kubwa ambayo wengi hawajui kuhusu baking soda,Ni ambavyo huweza kutumika kufanya shughuli nyingi za usafi.Uwepo wa alkalini ndani ya baking soda huipa uwezo wa kuondoa uchafu wenye asili ya asidi.
1.Kusafisha kibao cha kukatia nyama au mboga.
Kwa wale mnaotumia kibao cha plastiki au mbao kukata nyama mnajua ambavyo kibao hushika uchafu  na hata kubadilika rangi,hata baada ya kukiosha.Kutatua tatizo hilo na kufanya kibao chako kiwe safi na cheupe tena,Nyunyuzi  baking soda ya kutosha kisha sugua na dodoki adi kibao kiwe safi,kama ni uchafu wa muda mrefu loanisha kibao na maji kisha nyunyuzi baking soda na uache kwa dakika 15 ndipo usugue na dodoki
Kibao cha kukatia nyama kilichobadilika rangi.
Kibao cha kukatia nyama kilichobadilika rangi.
2.Kuzibua sinki la jikoni.
Sinki la jikoni mara nyingi huziba na kugoma kupitisha maji machafu kwasababu ya mafuta na uchafu wa chakula.Mwaga kikombe kimoja cha baking soda kwenye tundu la sinki,kisha mwaga vikombe vitatu vya maji ya moto sana.Acha kwa angalao masaa manne kabla hujatumia sinki.Ni  vyema ukafany ivyo usiku unapoenda kulala kwani sinki halitatumika adi asubuhi.
Baking soda ikiwa kwenye tundu la sinki na maji ya moto pembeni tayari kwa kuzibua sinki
Baking soda ikiwa kwenye tundu la sinki na maji ya moto pembeni tayari kwa kuzibua sinki
3.Kukata harufu ya mkojo chooni.
Kama unasafisha choo lakini bado kuna harufu mbaya ya mkojo.Chukua nusu kikombe cha baking soda changanya na nusu kikombe cha vinegar nyeupe kisha mwaga ndani ya choo  na unyunyuze kwenye sakafu ,na baada ya nusu saa unaweza kudeki sakafu ili pabaki safi.
4.Kusafisha na kung’arisha sinki,bathtab na tiles.
Ingawa wengi hupenda kuweka tiles,masinki na Bathtubs kwenye nyumba zao,utakubaliana na mimi nikisema wengi hawajui namna ya kuzifanyia usafi,unakuta sinki au tiles nyeupe zimegeuka na kua za rangi ya njano kwa uchafu.
Chukua nusu kikombe cha baking soda changanya na nusu kikombe cha sabuni ya majichanganya vizuri ili kupata kama uji mzito.Kisha tumia kusugua sinki,tiles au bathtub.
Baking soda ikitumika kusafisha tiles
Baking soda ikitumika kusafisha tiles
5.Kusafisha Oven
Kawaida unapohoka vyakula kama nyama,samaki,mboga za majani na matunda kama nanasi,mchuzi au umajimaji kutoka kwenye vyakula hivi humwagika ndani ya oven.Wakati mwingine unapo rost vyakula ndani  ya mafuta kwenye grill,mafuta huruka na kuchafua oven.Kwa kawaida uchafu wa aina hii Uganda haraka sana ndani ya oven.
Ili kusafisha .weka baking soda yakutosha kwenye sehem ya chini kabisa ya oven,kisha iloanishe na maji,usiweke maji mengi,kiasi tu cha kutosha kuloanisha baking soda.Fanya hivi usiku kabla ya kulala na ifikapo asubui uchafu wote ulioganda utakua umelainika,tumia dodoki kusafisha.
6.Kukata /Kuondoa harufu mbaya ndani ya friji.
Kutokana na uwekaji wa vyakula iana mbalimbali vyenye harufu tofauti tofauti mara nyingi friji huwa na harufu isioeleweka.Kwa sisi yunaoishi Tanzania na kukabiliwa na tatizo la umeme,umeme unapokatika kwa muda mrefu friji hutoa harufu.
Chukua boksi la baking soda,lifungue na kisha fungua mfuko wa plastiki uliobeba baking soda ili ukae wazi,kisha weka baking soda hiyo kwenye sehem ya chini ya friji yako,itanyonya harufu yote  ndani ya friji na kuiacha ikiwa fresh.Ukiweka boksi lenye baking soda kidogo utendaji wake huwa wataratibu sana,hivyo ni vyema ukaweka boksi jipya.
Baking soda ndani ya friji ili kukata/kuondoa harufu mbaya
Baking soda ndani ya friji ili kukata/kuondoa harufu mbaya
7.Kukata harufu kwenye nguo mpya
Mara nyingi unaponunua nguo mpya inakua na harufu ya upya na ndio maana watu wengi hufua nguo mpya kabla hawajavaa.Nguo za mtumba nazo hua na harufu kali inayolazimu kufua kabla hujavaa,hizi zote ni harufu za kemikali zilizotumika katika utengenezaji wa nguo,na kwa nguo za mitumba ni harufu ya madawa yenye kemikali zinazotumika kuhifadhi nguo.
Ili kuondoa harufu hizo,pima kikombe kimoja cha baking soda changanya kwenye maji lita tano ,kisha loweka nguo kwenye maji hayo kwa masaa matatu au zaidi,suuza na uanike.
Kwakua baking soda inaweza fanya yote haya,unakila sababu ya kua nayo jikoni kwako,hasa kwa ajili ya kusafishia kibao cha kukatia Nyama na mboga,pamoja na kuzibua sinki lako la jikoni.Ukweli ni kwamba,kibao cha kukatia nyama kikiwa kichafu,au kimebadilika rangi na mabaki ya nyama yamenata au kuganda  kwenye kibao hicho,inatia kinyaa na pia ni hatari kwa afya ya familia yako.Sinki la jikoni nalo likiziba na kuacha kupitisha maji machafu ndio mwanzo wa kurundika viombo vichafu na kua na maji machafu kwenye beseni kila wakati,chanzo kikubwa cha inzi jikoni na magonjwa ya tumbo.
Kama kawaida,naboresha maisha ya familia yako,Kazi yangu ni kukuelimisha tu,utendaji ni juu yako.
Jali afya ya familia yako.

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA