Skip to main content

FAIDA ZA GILIGILIANI KAMA KIUNGO, DAWA NA UREMBO.




Giligiliani  Mboga.
Giligiliani ni kiungo cha kawaida sana,wengi tunakitumia jikoni kwenye mapishi mbalimbali,Kinaharufu nzuri na ladha ya uchachu kwa mbali.Majani na mbegu za giligiliani vyote hutumika kama viungo jikoni.

Giligiliani inawingi wa Vitamini A, B6, C,B12,pia ina wingi wa madini chuma(iron),Calcium na Magnesium
Giligiliani inasifika kwakua dawa na kinga ya magonjwa mengi.Historia inaonyesha kwamba Kiungo hiki kilitumika kama dawa tangu enzi za kale nchini Egypt.Hata hivyo,tafiti za kisayansi za karne hii ya 21 zinathibitisha taarifa hizi



Giligiliani  Mbegu

Ni vyema kujua kwamba tunaposema chakula Fulani ni dawa,basi maana yake ni kwamba chakula hicho kinavirutubisho Fulani ambavyo huweza kukabiliana na ugonjwa Fulani au laa kuupa mwili uwezo wa kukabiliana na kujikinga na ugonjwa Fulani na si vinginevyo.

Hizi ni baadhi ya faida za giligiliani katika afya :

1.     Inawezesha usagaji mzuri wa chakula mwilini,hutuliza tumbo na huondoa gesi kwenye  utumbo mwembamba  ambayo mara nyingi husababishwa na vyakula tunavyokula hivyo hupunguza utoaji  gesi chafu (kunyampa) kwa kiasi kikubwa sana
2.   Inazuia magojwa ya tumbo yasabaishwayo na bacteria aina ya Salmonella.moja ya magonjwa haya ni kuumwa tumbo na kuhara.
3.  Inazuia Ugonjwa wa UTI.Yaani Urinary tract infection
4.  Inazui kutapika na hali ya kuvurugika tumbo
5.  Inaondoa gesi tumboni
6.  Inashusha sukari kwenye damu.(lower blood sugar)
7.  Inapunguza  cholesterol mbaya mwilin
8.   Chanzo kizuri cha nyuzi nyuzi zinazoitajika mwilini ili kuwezesha usagaji mzuri wa chakula (Dietary fiber)
9.   Inawafaa sana wanawake ambao hupata hedhi nzito
10.               Inaondoa maumivu,muwasho,na uvumbe (anti inflammatory)
11. Huondoa chunusi na madoa kwenye ngozi
Unaweza kuandaa giligiliani katika njia mbalimbali ili kuitumia kama dawa
  •  Kuondoa hedhi nzito.chemsha kijiko 1 cha chai cha mbegu za giligiliani na maji vikombe viwili.Chuja kisha ongeza sukari kidogo.Kunywa ikiwa yamoto au vuguvugu
  •  Kuondoa maumivu (Inflamation) chemsha kijiko kimoja cha chai cha mbegu za giligiliani zilizosagwa  na maji kikombe kimoja.Chuja kisha kunywa ikiwa vuguvugu
  • Kushusha sukari na kushusha cholesterol.Kunywa chai ya giligiliani (mbegu) mara kwa mara,pia tumia mbegu na majani ya giligiliani kwa wingi kwenye chakula.
  • Ili kuondoa chunusi na madoa meusi.Twanga au sigina majani ya giligiliani,chuja au kamua ili kupata maji yake.Pima vijiko vinne vya maji ya giligiliani kisha changanya na kijiko 1 cha chakula cha manjano(Binzari manjano).pakaa kwenye ngozi ,acha ikauke kisha osha au nawa na maji vuguvugu.Onyo:usisugue ngozi
  •  Kutibu kuhara damu (dysentery).Changanya vijiko 2 vya chai vya maji ya giligiliani na kikombe kimoja cha maziwa fresh ambayo hayajatolewa krim
  •  Chai ya giligiliani (mbegu) husaidia kuondoa au kutuliza asidi tumboni 
Matumizi ya mara kwa mara ya vyakula ambavyo ni tiba huupa mwili nafasi nzuri ya kuvuna virutubisho na kupata tiba ya magonjwa mbalimbali.
Ni vyema kujua kwamba asilimia kubwa ya vyakula na viungo tulivyonavyo majumbani ni tiba ya magonjwa mbalimbali.Madawa na Tiba nyingi za kisasa pia hutokana na mimea,virutubisho huvunwa kutoka kwenye mimea na vyakula na kuchanganywa na Kemikali ili kutoa vidonge na madawa ya magonjwA mbalimbali.

HERI TIBA CHAKULA KULIKO TIBA DAWA


Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA