Skip to main content

FAIDA ZA JUISI YA UKWAJU




Ukwaju ni tunda ambalo wengi hulitizama kama dawa.Tunda hili linasifika kwa kusaidia kutibu magojwa mbalimbali hii husababishwa na wingi wa virutubisho vinavyopatikana katika tunda hili,hasa madini mwili.

Juisi ya ukwaju
Watu wengi hawapendi juisi ya ukwaju kwasababu ya uchachu mkali na ambavyo inajitenga kwenye glasi (maji huja juu na ukwaju hubaki chini).Unaweza kutengeneza juisi hii na isiwe na uchachu mkali,wala isijitenge kwenye glasi .Juisi huwa nzito na tamu.
Mahitaji
  • Ukwaju robo kilo
  • Parachichi moja –ukubwa wa kati
  • Maji kwa kiasi upendacho
  • Sukari kwa ladha upendayo
Njia
1.loweka ukwaju kwenye maji ,acha uloane kwa saa moja.Tumia mwiko au kijiko kizito kuchanganya na kuponda ukwaju.chuja na weka  pembeni.
  • Ukipenda kutumia mikono,hakikisha umevaa glovzi za jikoni zakushikia vyakula ,si salama kushika na mikono wazi (mara nyingi hutumika mara moja tu kisha unazitupa)
  •   Loweka ukwaju kama uliununua sokoni ukiwa na maganda ukaumenya mwenyewe,kama umenunua ukwaju uliokwisha menywa,badala yakuloweka hakikisha unachemsha ukwaju ukiwa na maji.Lengo ni kuuwa vijidudu vinavyoweza leta magonjwa,kwani unakua umekaa wazi muda mrefu na Hujui aliyeushika kama alikua na mikono safi.
 2.Kata,menya parachichi kisha saga na maji kiasi (tumia mashine yakusagia juisi).chuja  weka pembeni
  • Usiweke parachichi jingi sana,litakata ladha ya ukwaju,weka kiasi tu kwani lengo la kuongeza parachichi ni ili kupunguza uchachu wa ukwaju na kuipa  juice uzito ili maji na ukwaju visitengane.
3.Katika chombo kipana changanya juisi ya ukwaju na parachichi kwa pamoja,ongeza maji adi upate uzito uupendao,ongeza sukari kwa kiasi upendacho kisha changanya adi upate juisi nzuri.isiwe chachu sana,iwe nzito kiasi na hakikisha umeweka sukari yakutosha.Chuja  na Adi hapa juisi tayari kwakunywa.

Ukipenda weka frijini iwe baridi.juisi hii inafaa kwa watu warika zote na unaweza kunywa wakati wowote.Kwa wagonjwa wa kisukari au wale ambao wanakwepa kunywa sukari ili kupunguza uzito,unaweza kuweka asali badala ya sukari.

FAIDA  ZA    JUISI  YA  UKWAJU

1.Chanzo kizuri cha viuasumu mwilini 'antioxidants' ambavyo huzuia Saratani (cancer)
2. Chanzo cha Vitamini B na C vile vile "carotentes"
3.Hushusha joto la mwili na kuondosha homa, hasa homa ya malaria na homa ya matumbo
4. Huulinda mwili dhidi ya mafua na kero za mafua kooni
5. Husaidia myeyusho na mmengenyo wa chakula na kuondosha kuvimbiwa
6. Husaidia kutibu matatizo ya nyongo (bile disorders)
7.Husaidia kurahisisha choo (laxative)
8.Husaidia kupunguza wingi wa lehemu (cholesterol) na hivyo kuimarisha moyo
9.Husaidia ngozi kuwa nyororo, vile vile husaidia ngozi inayopona baada ya kuungua au yenye vidonda
10.Husaidia kuua minyoo tumboni (kwa watoto wadogo)

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA