Skip to main content

UNENE KUPITA KIASI WAFANYA ASHINDWE KUAMINIKA




Quantasia  Sharpton


Kama   majaji na  mahakimu  wangekuwa  wanatoa  maamuzi  yao  kwa  kuzingatia  muonekano  au  maumbile  ya  mtu  basi  watu  wengi  sana  wangenyimwa  haki  zao.






Quantasia  kushoto  akitoa  maelezo  yake  kwenye  media.

Hivyo  ndivyo  unavyo  weza  kusema   mara  baada  ya  kupata  taarifa  hii  inayo  muhusu  mwanadada  Quantasia   Sharpton  (  21 ), ambae  madai  yake  mazito  dhidi  ya  mwanamuziki  mmoja  maarufu  nchini  Marekani, yame bezwa  na  watu  wengi , huku  sababu  ikitajwa  kuwa   unene  na  uzito  kupita  kiasi.

Wiki  kadhaa  zilizo  pita, vyombo  mbalimbali  vya  habari  nchini  Marekani, viliripoti  kuhusu mwanamuziki  nguli  nchini  humo  Usher  Raymond  kudaiwa  kumlipa  fidia  ya  zaidi  ya  Shilingi  Bilioni  mbili  za  kitanzania, mwanamke  mmoja  kwa  madai  ya  kumuambukiza  maradhi  ya  kaswende.

Baada  ya  kutoka  kwa  taarifa  hii, wanawake  kadhaa  nchini  humo  wameibuka  wakidai  nao  pia  wameambukizwa  maradhi  hayo  na  Usher.
Mmoja  kati  ya  wanawake  hao  ni  mwanadada  Quantasia  Barino  mwenye  umnri  wa  miaka 21  ambae  anadai  uambukizwa  maradhi  hayo  na  Usher  mwaka  juzi, wakati  ana  sherehekea  kutimiza  miaka  kumi  na  tisa.

Mwanamke  huyo  amekiambia  chombo  kimoja  cha  habari  nchini  humo  kuwa,  alikutana  na  Usher  kwenye  concert . 

Aliongeza  kuwa, mmoja  kati  ya walinzi wa Usher  alimfuata  mwanadada  huyo  na  kumwambia  kiuwa  Usher  amevutiwa  nae  na  kwamba  anataka  kupitisha  nae usiku  wa  siku  hiyo , ambapo  mwanadada  huyo  hakuwa  na  hiana  na  kumpatia   mlinzi  huyo  namba  zake  za  simu.
   Baadae  nilipigiwa  na  Usher  kupitia  private  number  ambapo  aliniomba  niende  kwenye  hoteli  aliyo  fikia.  Nilifanya  mapenzi  na  Usher  usiku  huo    Alieleza  Quantasia.
Habari  ya  mwanadada  huyu  ilienea  kwa  kasi  kwenye  mitandao  mbalimbali  ya  habari  nchini  Marekani, ambako  idadi  kubwa  ya  watumiaji  wa  mitandao  hiyo  walionekana  kutokukubaliana  na  maelezo  ya  mwanadada  huyo  huku  sababu  kuu  ikionekana  kuwa  unene  kupita  kiasi  wa  mwanadada  huyu.
Watu  wengi  walio changia  mawazo  yao  kwenye  habari  hii  walikuwa  wanaonekana  kuwa  na  maoni  kuwa   Usher  hawezi  kutoka  kimapenzi  na  mwanamke  mnene  kama  Quantasia, jambo  ambalo  lilipingwa  vikali  na  wachangiaji  wengine  ambao  walisema mapenzi  hayachagui na  kwamba  wapo  wanaume  wengi  tu  ambao  wanapendezwa  na  wanawake  wanene:

Mchangiaji  mmoja  aliandika  “This Chick 300 + Lbs Talkin About Usher Chose Her Out The Crowd And Smashed... “
Mchangiaji  mwingine  aliandika “   Nitaanza  kuamini  kwanza  Usher  ni  shoga  kabla  sijaamini  alitembea  na  mwanamke  huyu “
Hayo  ni  baadhi  ya  maoni  ya  wachangiaji  ambao  walikataa  kata  kata  kukubaliana  na  madai  ya  mwanadada  huyu.
Hata  hivyo  pamoja  na  wachangiaji  walio  mbeza  dada  huyu, wapo  wachangiaji  walio  onekana  kukubaliana  na  madai  yake.
Baadhi  ya  maoni  ya  wachangiaji  hao  ni   mmoja  aliye  sema  Usher been into big girls for a while y'all better believe it     Na  mwingine  akasema  “If y'all don't believe Usher slept with ol' girl cause she big, y'all need to wake up. I need all the big girls to show yall their DM's. “


Tatizo  la  unene  na  uzito   kupita  kiasi  linazidi  kushamiri  kwa kasi  katika  jamii  nyingi  duniani  . Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, tatizo  la  unene na  uzito  kupita  kiasi  linasababishwa  na  mambo mbalimbali  kama  vile  ulaji mbaya  wa  chakula  unao endana  na  kutokufanya  mazoezi
Kufahamu  zaidi  kuhusu  uzito,unene  na  au  kitambi  vinavyo  patikana  tafadhali, tembelea  link  hii  hapa  chini :


Comments