Skip to main content

BAO LA NICKLAS BENDTNER LAZUA MAMBO

Nicklas  Bendtner



MSHAMBULIAJI   WA  Arsenal   Nicklas  Bendtner  Jumatano  usiku  wiki  iliyopita  alifunga  bao  maridadi  la  kwanza  la  kuongoza  la  Arsenal  katika  pambano  dhidi  ya  Hull  City  na  kuendelea  kuiweka  kileleni  timu  yake  hiyo  ambayo  imekuwa  ikimsugulisha  benchi.
Bendtner  alivaa  jezi  ya  Arsenal  na  kuanza   mechi  kwa  mara  ya  kwanza  ikiwa  zimepita  siku 1,005  tangu  alipoanza  mechi  yake  ya  mwisho  Emirates  kabla  ya  kutimka  kwa  mkopo  katika  klabu  za  Sunderland  na   Juventus.
Alibakizwa  na  kocha  wa  Arsenal , Arsene  Wenger  katika  siku  ya  mwisho  ya  uhamisho  wa  wachezaji  England  baada  ya  kocha  uyo  Mfaransa  kumkosa  mshambuliaji  wa  Chelsea, Demba  Ba  al;iyekuwa  anatarajia  kutimka  kwa  mkopo  klabuni  hapo.
Hilo  lilikuwa  bao  lake  la  kwanza  tangu  alipo fanya  hivyo  Machi  2011  huku  akikosa  mabao  ya  wazi  katika  pambano  la  kombe la  Ligi  dhidi  ya  West   Brom.
Hata  hivyo, bao  hilo  limezua  kasheshe  kubwa  katika  mitandao  ya  kijamii  baada  ya  watu  wengi  kuanza  kumkejeli  kutokana  na  kukaa  miaka  mingi  bila  ya  kufunga.
Mtu  wa  kwanza  kumkejeli  Bendtner  alikuwa  mshambuliaji  wa  zamani  wa  Tottenham  na  timu  ya  taifa   ya  England, Gary  Lineker.  Huyu  aliandika  katika  akaunti  yake  ya  Twitter  akisema     Baadhi  ya  washambuliaji  mahiri  Ligi  Kuu  England  wanafunga  mabao  leo. Suarez, Aguero  na  Bendtner “
Alifanya  hivi  wakati  akijua  wazi  kwamba  kwa  sasa, Bendtner  hachukuliwi  kama  mshambuliaji  hatari  katika  Ligu  Kuu England, achilia  mbali  ukweli  kwamba  hafikii  kabisa  katika  anga  za  Luis  Suarez  na  Sergio  Aguero.
Shabiki  mwingine  wa  soka  aliyejulikana  kama  Nooruddean  akitumia  akaunti  yenye  jina  la  @ BeardedGenius  alitumia  ujumbe   akisema  “ Chamakh  amefunga  jana, Bendtner  amefunga  leo, kesho  ni  mwisho  wa  dunia 
Alikuwa  akimaanisha  bao  lililofungwa   na  mshambuliaji  wa  Crystal  Palace, Maroune  Chamakh, Jumanne  usiku  katika  pambano  dhidi  ya  West  Ham, huku  pia  akilikejeli  bao  la Bendtner  dhidi  ya   Hull City.
Mtandao  wa  kituo  cha  BBC  cha  Uingereza   nao  uliandika  ukweli  ambao  ulionekana  kama  kejeli. Wao  waliandika “ Nicklas  Bendtner  amefunga  mabao  mengi  mwezi  huu  kuliko  Christiano  Ronaldo, Lionel  Messsi, Franck Ribbery  na  Robin  Van  Persie  ukiwajumlisha  pamoja 
Ni  kweli  kwamba  mastaa  wote  hao  hawajafunga  bao  lolote  tangu  mwezi  huu  wa  Desemba  uanze  kutokana  na  kuwa  majeruhi, lakini  ujumbe  huu  ulitumwa  kama  kejeli  kwa  Bendtner.
Shabiki  aliyefahamika  kwa  jina  la  Rich  B  naye  alituma  ujumbe  ulio  kuwa  na  lengo  la  kumkejeli  Bendtner. Yeye  aliandika  akidai  “ Bendtner  amefunga  bao  dhidi  ya  Hull. Suarez  hakuweza  kuwafunga. Kwa  hiyo  Bendtner  ni  bora  kuliko  Suarez ‘
Shabiki  mwingine  aliye  itwa  Christa  naye  alitoa  kali  ya  mwaka  baada  ya  kutuma  ujumbe  katika  mtandao  wake  wa  Twitter  akionesha  kumkejeli  mshambuliaji  huyo  wa  kimataifa  wa  Denmark.
Christa  alisikika  akisema :
  Nimeamka  leo  asubuhi  katika  dunia  ambayo  Nicklas  Bendtner  amefunga  bao. Na  ndio  maana  upepo  unavuma  kwa  kasi  sana, nadhani  ulimwengu  umetingishika  vibaya  sana”
Wakati  Christa   akiwa  ametoa  kejeli  hiyo, shabiki  mwingine  wa  Arsenal  aliyetambulika  kwa  jina  la  Faisal  alituma  ujumbe  wa  kejeli  ambayo  uliashiria  kuwa  Bendtner  alikuwa  anastahili  kuwa  mwanasoka  bora  wa  dunia.
“ Jina  Bendtner  huwa  linaanza  na  herufi B na  huwa  linaishia  na  herufi  R,  hii  ni  kama   ilivyo  jina la  BALLON  D’OR, aliandika  Faisal  kwa  kejeli  kubwa.
Shabiki  mmoja  aliyejulikana  kwa  jina  la  Ken  alikwenda  mbali  zaidi  baada  ya  kumlinganisha  Bendtner  na  mastaa  wa  zamani  wa  Arsenal, Dennis  Bergkamp  na  Thiery  HENRY.
“ Bergkamp  kisha  Henry…na  sasa  Bendtner !”
Ameonyesha   jinsi  alivyo  bora  katika  kufunga  pindi  anaporudi  uwanjani  kwa  namna  ya  kushindana  na  wakongwe  hawa “
Faraja  pekee  ambayo  Bendtner  ameipata  ni  kutoka  katika  kauli  ya  nahodha   wake, Mikel  Arteta  ambaye  alisema  staa  huyo  mwenye  majigambo  bado  ni  mchezaji  muhimu  katika  kusaka  ubingwa  wa  England.
“ Hicho  ndicho  tunacho  taka. Wachezaji  waliopo  kikosini  wanaweza  kuchangia  timu  kupata  mafanikio. Kila  mtu  ni  muhimu. Tunamuhitaji  kila  mmoja  kama  tunataka  kushinda  kitu. Nadhani  ni  kitu  kizuri. “ Bado  ni  mchezaji  wa  Arsenal  na  wakati  akiwa  hapa  atatoa  asilimia  100  ya  nguvu  zake. Hatafikiria  tofauti  au  kufanya  tofauti” alisema  Arteta.
CHANZO :  GAZETI  LA  MWANASPOTI, TOLEO  Na. 1440, Desemba  9, 2013.

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA