Skip to main content

MCHUNGAJI DAR, AANZISHA KLABU YA USIKU.



Mchungaji  Harris  Kapiga.
SIKU  ya  kupeana  zawadi  , maarufu  kama  Boxing  Day, ambayo  huangukia  Desemba  26, kila  mwaka, zamu  hii  itakuwa  ya  kipekee  kwani  itaambatana  na  uzinduzi  wa  Klabu  ya  Usiku  (Night  Club )
Iliyo  anzisha  na  Mchungaji  mmoja  katika  maeneo  ya  Mbezi  Beach, jijini  Dar  Es  salaam, imefahamika.
Kwa  mujibu  wa  Mchungaji  huyo, Harris  Newman  Kapiga, ingawa  klabu  hiyo  itakuwa   baadhi  ya  vifaa  kama  vilivyo  katika  klabu  za  usiku  za  kidunia, ikiwa  ni  pamoja  na  taa  za  rangi  zinazo  badilika   badilika, kutakuwa  na  ibada  moto  moto  za  kusifu  na  kuabudu.
“ Sio  mikesha, ni  Night  Club ( Klabu  ya  Usiku ), na  kutakuwa  na  kiingilio  kidogo.  Tunataka  kutumia  muda  ambao  shetani  anautumiwa  kuabudiwa, na  sisi  tumwabudu  Mungu wetu “ alisema  Mchungaji  Kapiga, alipo  ongea  na  Nyakati  kwa  njia  ya  simu  wiki  iliyopita.


Kapiga  ambaye  pia  ni  mtangazaji  wa  Redio  ya  Clouds  ya  jijini  Dar  Es  salaam, na  pia  ni  mchungaji  wa  kanisa  maarufu  la  Nchi  Ya  Ahadi, alisema klabu  hiyo inayoitwa  Ela  Gospel  Club, itazinduliwa  rasmi  Desemba  26, 2013, siku  ya  pili  baada  ya  Krismasi.
Alieleza  kuwa, jina  hilo  la “ Ela”  linatokana  na  jina  jina  la  bonde  ambalo  Daudi  alimwangamiza  Goliathi, na  kwamba  anaamini  huduma  hiyo  ya  usiku  itaangusha  Goliathi  wengi.

Mchungaji  Kapiga, alisema  klabu  hiyo  itakuwa n inafunguliwa  kuanzia  saa  tatu  za  usiku  na  kufungwa  saa  kumi  za  usiku, na  itafanya  kazi  siku  za  Ijumaa, Jumamosi  na  Jumapili.

“  Watu  wasio elewa  sasa, wanaweza  kuniita   Freemason, lakini  si lazima  wote  waelewe  wakati  mmoja, wataelewa  taratibu. Unapoanzisha  kitu  kipya, usitegemee  watu  wote  wakupigie  makofi “,  alisema  Kapiga  alipoulizwa  iwapo  hiyo  isingemfanya  aonekane  mtu  wa  ajabu.
Mchungaji  Kapiga, alisema  klabu  ya aina  hiyo siyo  ya  kwanza  duniani  ingawa  itakuwa  ya  kwanza  kwa  hapa  nchini.
Alisema  zipo  klabu  za  aina  hiyo  Ulaya  na  hata  Marekani  pia.
Alisema  katika  ukumbi  wa  klabu  hiyo ulioko  karibu  na  Shule  ya  Msingi  Mwalimu  Nyerere, eneo la  Tangi  Bovu, kutakuwa  na  kucheza  nyimbo  za  injili, kutakuwa  na  nyama  choma na  mambo  kama  hayo, isipokuwa  pombe, na  kwamba  mara  kadhaa  itatolewa  nafasi  kwa  ajili  ya  wanao  taka  kuokoka, na  wanao hitaji  maombezi.
“ Tumewalenga  zaidi vijana  kati  ya  miaka  19  hadi  25, ingawa  hatuwazuii  wenye  umri  zaidi  ya  hapo ‘, alisema  Kapiga  na  kuongeza  “ Tunataka hawa  wa  umri  wa  kujirusha, ila  wazee  na  hata  watu  wa  dini  nyingine  waje  tu, ila  wajue  habari  za  Yesu zitakuwapo.
CHANZO : GAZETI  LA   NYAKATI, TOLEO Na.680, Desemba 08-14, 2013

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA