Skip to main content

UNASUMBULIWA NA MAFUA ? Kula Vifuatavyo :



Picha  ya  mtu  mwenye  mafua.
Mafua  ni  ugonjwa  unao   sumbua  watu  kila  mwaka, hasa  yanayo  anza  kutokea  mabadiliko  ya  hali  ya  hewa  kutoka  msimu wa  kiangazi  kuingia  masika.

Ili  kujikinga  na  ugonjwa  wa  mafua  ni  lazima  mwili uwe  na  kinga  ya  kutosha.

Orodha  ya  vyakula  vifuatavyo  vimeelezwa  kuwa  na  uwezo  mkubwa  wa  kuimarisha  kinga  ya  mwili na  kupambana  na  maambukizi  mengine  kwa  kuwa  na  kiasi  kikubwa  cha  protini  na  virutubisho  vingine.

                              SUPU  YA  KUKU

Supu ya  kuku  wa  kienyeji  inaelezwa  kuwa  na  virutubisho  vinavyo  saidia  kupunguza  utokaji  wa  makamasi. 
Supu  ya  kuku



Utapata  virutubisho  vingi  zaidi  ukitengeneza  supu  ya  kuku  kwa  kuchanganya  na  mboga  za  majani. Weka  chumvi  kiasi  kidogo  katika  supu  hiyo.

                          VITUNGUU  SAUMU
Vitunguu  saumu  vina  kirutubisho  aina  ya  ‘ allicin’  ambacho  kina  uwezo  wa  kutoa  kinga  dhidi  ya  magojwa  mbalimbali  ya  kuambukiza. 

Vitunguu  Saumu


Kitunguu  saumu  kinatoa  kinga  halikadhalika  kinapunguza   muda  wa  mtu  kuumwa  na  mafua.
Tumia  kitunguu  hicho  kwa  kupika  kwenye  chakula  au  kwa  kutafuna  punje.

                                      CHAI
Chai  hasa  ya  kijani, ( Green  Tea ) ina  virutubisho  vya  kuimarisha  kinga  ya  mwili .

Chai  Ya  Kijani

Utafiti  wa  hivi  karibuni  ulio  fanywa  na  jarida  moja  la  masuala  ya  virutubisho  nchini  Marekani ( Journal Of  the  American College  of  Nutrition )  umeonyesha  kuwa  watu  wanao  tumia  chai  kwa  mpangilio  maalumu, hawasumbuliwi  mara  kwa  mara  na  mafua  pamoja  na  magonjwa  mengine  ya  kuambukiza, huwa  salama  na  mafua  au  siku za  kuumwa  mafua  hupungua  kwa  asilimia  36 ukilinganisha  na  wale wasio  kuwa  na  kinga  imara.
Hata  hivyo, tahadhari  inatolewa  kwa watoto wa  shule kutokupewa  kiasi  kingi  cha  chai kwa  siku.

Unywaji  wa  kikombe  kimoja  kwa  siku  kwa  motto  wa  shule  siyo   mbaya.

Kwa  mtu mzima, usizidishe   vikombe vitatu  kwa  siku.
Ikumbukwe  kuwa, chai  inapotumika  kwa  wingi  kupita  kiasi, huweza  kusababisha  pia  tatizo  la  kukosa  choo  kwa  muda  mrefu.
Kunywa  kiasi  kwa  afya  yako.

  MACHUNGWA, PILIPILI  KALI

Utafiti  unaonyesha  kwamba, ulaji  wa  vyakula  vyenye  Vitamin  C  kwa wingi  kila  siku  husaidia  kuondoa  au  kuzuia  ugonjwa  wa  mafua.

Machungwa

Miongoni  mwa  vyakula  vyenye  kiwango  kikubwa  cha  Vitamin  C ni  pamoja  na  machungwa, mboga  za  majani  aina  ya  Brokoli  na  pilipili kali.

Pilipili Kali

Ili  kupata  kiasi kingi  cha  Vitamin C, inashauriwa  machungwa  yaliwe   pamoja  na  nyama  zake  za  ndani  au  kunywa  juisi  yake.

                  
Brokoli

                                       ASALI
Kama  inavyo  julikana, asali  ni  tiba  ya  matatizo  mengi  ya  kiafya, miongoni  mwa  hayo  ni  pamoja  na  mafua.
Asali  inasaidia  kuondoa  kikohozi  na  muwasho  kwenye  koo.  Halikadhalika, asali  inaweza  kutumiwa  na  watoto wadogo  kama  dawa.



Asali

Watoto  wanao  ruhusiwa kutumia  asali  kama  tiba  ni  wa  umri  wa  kati  ya  miaka  2  hadi  5.
Hawa  dozi  yao  ni  nusu  kijiko  kidogo  cha  asali, wenye umri  wa  miaka  6 hadi  11  wapewe  kijiko  kimoja  kidogo  na  wenye  umri  wa  kuanzia   miaka  12  hadi  18, wapewe  vijiko  vidogo  viwili  vya  asali  wakati  wa  kulala.

                            MTINDI


Mtindi



Kutokana  na  kiwango kikubwa  cha  protini  ilicho nacho, Mtindi  ni  chakula  kingine  kinachofaa  kuliwa  na  mtu  mwenye  mafua  ili  kupunguza  siku  za  kusumbuliwa  na  ugonjwa  wa  kukohoa.

                  CHOKOLETI  NYEUSI




Chocolate Nyeusi.

Wataalamu  wanakubaliana  kuwa, ulaji  wa  ‘chocolate’ nyeusi ( Dark  Chocolate ), huimarisha  kinga  ya  mwili, hivyo  inapoliwa  na  mgonjwa  wa  mafua, huweza  kumpa  ahueni  mgonjwa  kwa  namna  moja   ama  nyingine, na  pia  huwa  kinga  kwa  magonjwa  mengine.

                           PWEZA 



Supu  Ya  Pweza.

Samaki  aina  ya  pweza  wana virutubisho  vingi  vya  kuongeza  kinga ya  mwili  yenye  uwezo  wa  kupambana  na  bacteria  pamoja  na  virusi  vya  mafua.
Kiasi  kidogo  cha  pweza, awe  wa  kukaangwa  au  kuchemshwa  kama  supu,  anafaa  kuliwa  mara  kwa  mara  kukmarisha  kinga  ya  mwili.

                        VIAZI  VITAMU
Kirutubisho  aina   ‘ Beta carotene’  huimarisha  kinga  ya  mwili.



Viazi  Vitamu.

Kirutubisho  hicho  huwa  ni  muhimu  kwa  ustawi  na  uimarishaji  wa   kinga  mwilini  na  kinapatikana  kwa wingi  kwenye  viazi  vitamu na  vyakula  vingine  kama  vile  karoti, maboga  na  mayai ( kiini)
Kwa  ujumla , suala  la  kuimarisha   kinga  ya  mwili  ni  muhimu  kwa  afya  zetu.

Ulaji  wa  vyakula  vilivyo  tajwa  hapo  juu  na  vingine, unatakiwa  kuwa  ni wa  mara  kwa  mara  kama  siyo  wa  kudumu, kwa sababu  mwili  unapokosa  kinga  imara, ni  rahisi  kushambuliwa  na  maradhi  ya  kuambukizwa.

CREDIT :  GAZETI  LA KISIWA, Toleo Na. 165, Desemba 6. 2013.



Kwa  Taarifa  zaidi  kuhusu  masuala  ya  dawa  za mimea  na  vyakula  lishe, endelea  kutembelea NEEMA  HERBALIST  BLOG  kila  siku.  

Na  kwa  msaada  wa  Dawa   Za  Mimea  na  Vyakula  -Lishe, tembelea  katika  ofisi  zetu  zilizopo  katika  eneo  la  CHANGANYIKENI karibu  na  CHUO  CHA  TAKWIMU au  Wasiliana  nasi  wa SIMU  0766538384. 

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA