Skip to main content

MAAJABU YA MUNGU : Maiti Azaa Mtoto Baada Ya Kunyongwa!




Katika  hali  isiyo  ya  kawaida, watu  wa  mji  wa Kaharisi  nchini  Uturuki  wameshuhudia  tukio  la  ajabu  la  kuzaliwa   kitoto  kichanga  cha  miezi saba baada  ya  mama  yake  kunyongwa.

Kwa  mujibu  wa mtandao  wa  Intaneti  wa  Televisheni  ya  Al  Alam, toto  huyo  wa  kiume  amezaliwa  akiwa  na  afya  nzuri.

Habari  zaidi  zinasema  kuwa, daktari  wa  gereza  aliukimbilia  mwili  wa Sabah  Mosilibasa, mwenye  umri wa  miaka 28  baada  ya  kujifungua  mtoto huyo, huku  akikata  roho.

Aidha  habari  zinasema  kuwa, hadi  mwanamke  huyo  anatiwa  kitanzi, hakuna  aliyekuwa  anajua  kwamba  alikuwa  na  ujauzito  wa  miezi  saba  kutokana  na  unene  wa  mwili  wake,  suala  ambalo  limezidi  kuwashangaza  watu.

Sabah  alihukumiwa  kifo  baada  ya  kupatikana  na  hatia   ya  kumuua  kwa  sumu  mumewe  na  watoto  wake  wawili  na  alisalia  gerezani  kwa  muda wa  miezi  mitatu  akisubiri  hukumu  dhidi  yake.

Duru  za  habari  zinasema  kuwa, watu  walishangaa  baada  ya  kuwekwa  kamba  ya  kitanzi  shingoni  mwake na  kufyatuliwa  kitanzi  kama  ishara  ya  kumalizika  adhabu  hiyo, lakini  Mosilibasa  aliendelea  kutikisika  miguu  licha  ya  kwamba  adhabu  hiyo  ilikuwa  imeshatekelezwa  dhidi  yake.

Muda  mchache  baadaye   alizaa  mtoto  wa  kiume  ambaye  awali alidhaniwa  kuwa  naye  ameshakufa, lakini  baada  ya  kumsaidia  pumzi  mtoto  huyo  aliweza  kupumua  na  kisha  kupiga  kelele.



CREDIT  :  GAZETI  LA KISIWA, Toleo Na. 165, Desemba 6. 2013.

Comments

Popular posts from this blog

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na...

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ...

FAIDA KUMI ZA MTI WA MKOMAMANGA

Mti   wa   Mkomamanga   ni   mti   wenye   faida   nyingi   sana   katika   afya   ya   mwanadamu. Mti   huu   una   virutubisho –afya     mbalimbali   ambavyo   ni   muhimu   katika   afya   ya   mwanadamu.   Virutubisho   hivyo   vinapatikana   kwenye   magome, majani, mbegu, maganda   ya   matunda, juisi   ya   matunda   pamoja   na kwenye   maua   ya   mti   wa   mkomamanga. Zifuatazo   ni   faida   muhimu   za   mti   wa   mkomamanga : 1.           Maganda   ya   tunda   la   mkomamanga   yakichemshwa    hutoa   juisi    ambayo   hutumika   kama   dawa   ya   kufunga   kuhara. 2.   ...