Skip to main content

MAAJABU YA MUNGU : Maiti Azaa Mtoto Baada Ya Kunyongwa!




Katika  hali  isiyo  ya  kawaida, watu  wa  mji  wa Kaharisi  nchini  Uturuki  wameshuhudia  tukio  la  ajabu  la  kuzaliwa   kitoto  kichanga  cha  miezi saba baada  ya  mama  yake  kunyongwa.

Kwa  mujibu  wa mtandao  wa  Intaneti  wa  Televisheni  ya  Al  Alam, toto  huyo  wa  kiume  amezaliwa  akiwa  na  afya  nzuri.

Habari  zaidi  zinasema  kuwa, daktari  wa  gereza  aliukimbilia  mwili  wa Sabah  Mosilibasa, mwenye  umri wa  miaka 28  baada  ya  kujifungua  mtoto huyo, huku  akikata  roho.

Aidha  habari  zinasema  kuwa, hadi  mwanamke  huyo  anatiwa  kitanzi, hakuna  aliyekuwa  anajua  kwamba  alikuwa  na  ujauzito  wa  miezi  saba  kutokana  na  unene  wa  mwili  wake,  suala  ambalo  limezidi  kuwashangaza  watu.

Sabah  alihukumiwa  kifo  baada  ya  kupatikana  na  hatia   ya  kumuua  kwa  sumu  mumewe  na  watoto  wake  wawili  na  alisalia  gerezani  kwa  muda wa  miezi  mitatu  akisubiri  hukumu  dhidi  yake.

Duru  za  habari  zinasema  kuwa, watu  walishangaa  baada  ya  kuwekwa  kamba  ya  kitanzi  shingoni  mwake na  kufyatuliwa  kitanzi  kama  ishara  ya  kumalizika  adhabu  hiyo, lakini  Mosilibasa  aliendelea  kutikisika  miguu  licha  ya  kwamba  adhabu  hiyo  ilikuwa  imeshatekelezwa  dhidi  yake.

Muda  mchache  baadaye   alizaa  mtoto  wa  kiume  ambaye  awali alidhaniwa  kuwa  naye  ameshakufa, lakini  baada  ya  kumsaidia  pumzi  mtoto  huyo  aliweza  kupumua  na  kisha  kupiga  kelele.



CREDIT  :  GAZETI  LA KISIWA, Toleo Na. 165, Desemba 6. 2013.

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA