Skip to main content

Tatizo La Kutokwa na Kinyama Sehemu Ya Haja Kubwa : Chanzo, Athari Zake na Tiba Yake .


Tatizo  La  Kutokwa  na  Kinyama Sehemu  Ya  Haja Kubwa :  Chanzo, Athari  Zake  na  Tiba   Yake .


Tatizo  la  kutoka  na  kinyama  ama  uvimbe  katika  sehemu  ya  haja  kubwa  hujulikana  kama  Bawasiri.

Katika  lugha  ya  kitaalamu  ugonjwa  huu  hujulikana  kama haemorrhoids  ilihali  katika  lugha  ya  kiingereza, hujulikana  kama  Piles.

Tatizo hili husababishwa na kuvimba, kuharibika na kuondoshwa katika eneo lake kwa  mishipa ya damu  katika eneo la mfereji wa haja kubwa.

Tatizo hili huwaathiri zaidi watu wazima kuliko watoto na inakadiriwa kuwa karibu asilimia 50 ya idadi ya watu wote wako hatari ya kupata tatizo hili katika umri wa miaka 50.

Ingawa dalili zake zinaweza zisijitokeze, lakini tatizo hili huwa na madhara kama kuvuja damu, kuporochoka kupitia tundu la haja na maumivu.

Aina  Za   Bawasiri :  

Kuna  aina  mbili  za  bawasiri

Bawasiri ya nje:
Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa, na huweza kuambatana na maumivu, pamoja na kuwashwa kwa ngozi katika eneo hilo. 

Mara nyingine, mishipa hiyo ya damu (vena) hupasuka na damu huganda na kusababisha aina ya bawasiri ambayo kitaalam inaitwa Thrombosed hemorrhoid.
Bawasiri ya ndani:

Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa  na   huwa haimbatani na maumivu na wengi huwa hawatambui kuwa wanatatizo hili.

Hutokana na kuvimba na kuharibika kwa vimishipa vya aina ya artery za ndani ya mfereji wa haja kubwa.

Aina hii imegawanyika katika mainisho yafuatayo:
-Daraja I- Bawasiri kutotoka katika mahali pake pa kawaida
-Daraja II- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na kurudi yenyewe baada ya tukio hilo.
-Daraja III- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kuirudisha mwenyewe baada ya tukio hilo.
-Daraja IV- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na vigumu mtu kuirudisha baada ya tukio hilo.

Je, bawasiri husababishwa na nini?
Chanzo chake kikuu kitaalam hakijulikani, ingawa mambo yafuatayo yanaweza kusababisha au kukuweka katika hatari ya kupata bawasiri:
i.                    Tatizo sugu la kuharisha
ii.                   Kupata kinyesi kigumu
iii.               Ujauzito
iv.                uzito kupita kiasi (obesity)
v.                  Mazoezi ya kunyanyua vitu vizito
vi.                Kuingiliwa  kinyume  na  maumbile
vii.              Umri mkubwa
viii.           Mambo yanayoongeza shinikizo katika utumbo  mpana kama kukaa muda mrefu mahali pamoja
ix.               Matumizi ya vyoo vya kukaa kwa muda mrefu kuliko vya kuchuchumaa na kujisaidia kwa mda mrefu wakati wa haja.
                Dalili za bawasiri
i.                    Damu kunuka kinyesi wakati wa kujisaidia
ii.                  Maumivu au usumbufu wakati wa kujisaidia
iii.                Kinyesi kuvuja
iv.                kijiuvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa
v.                   Ngozi  kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa
vi.                Na kujitokeza kwa kinyama (bawasiri) wakati wa haja kubwa.
Matatizo yanayoweza kutokana na bawasiri:
Upungufu wa damu mwilini (Anaemia) na bawasiri iliyojikaba (Strangulated haemorrhoids)

Vipimo na uchunguzi:

Kipimo cha kidole cha shahada kwa njia ya  puru (Digital Rectal Examination), Kipimo cha njia ya haja kubwa cha kutazama moja kwa moja (Proctoscope) na Kipimo cha utumbo mpana (Sigmoidoscope)

Matibabu yake

Matibabu hutegemea na hali na aina ya Bawasiri, pia tiba mara nyingi si ya upasuaji, mfano mgonjwa ataelekezwa kukalisha eneo la haja kubwa katika maji ya vuguvugu kwa mda fulani, ipo tiba rahisi iitwayo Rubber band ligation
Hapa mishipa hufungwa na rubber band ili kuzuia damu kwenda kwenye eneo liloathirika, njia hii hutumika kwenye aina ya ndani ya bawasiri.

 Tiba  Ya  Asili   Ya  Bawasiri :
Unaweza  kujaribu  mwenyewe  mojawapo kati  ya tiba  zifuatazo.  Kila  tiba  inajitegemea  hivyo  unahsuariwa  kuanza  na  tiba  moja  kwanza na  uangalie  matokeo  yake kabla  ya  kuhamia  na  tiba  nyingine,usitumie  tiba  zote  kwa  wakati  mmoja.
i.                     Tiba  1  :   Kula  kijiko  kimoja  cha  chakula  cha  unga wa Habbat-Sawdaa pamoja na  glasi  moja  ya  maji  mara mbili  kwa  siku  kwa  muda  wa  siku  kumi  na  nne.

ii.                    Tiba  2  :  MAKAL-ARZAK
Chukua 100grm kwa kila lita moja na robo ya

maji (1250ml).

Chemsha mpaka ibakie lita moja kamili.
Kunywa ujazo wa kikombe kimoja cha kahawa (50ml) kutwa mara tatu (1×3) mpaka dawa imalizike.

N:B : Mgonjwa asitumie nyama nyekundu aina yoyote,asile pili pili na wala asitumie vitu vikali.Badala yake atumie kwa wingi mboga za majani,matunda,maziwa na samaki.

iii.                  TIBA  3  : Changanya unga wa Habat soda na Asali safi ya nyuki vipimo vya sawa kwa sawa.Halafu kunywa kijiko kimoja kimoja mara kwa mara.Fuatilishia na kumywa maji glasi moja (250ml) kila umalizapo kunywa hiyo dawa.

iv.                 Tiba  4  : Jipake mafuta ya Nyonyo  kwenye utupu wa nyuma ambapo ndipo bawasiri hutokea.Fanya hivyo mara kwa mara, kwa sababu huirudisha hiyo bawasiri ndani.
Mbarika hujulikana vile vile kwa majina ya mbono,nyonyo au “castor oil”.

Kwa  ushauri  zaidi,  fika  katika  ofisi  za  Neema  Herbalist  zilizopo  katika  eneo  la  CHANGANYIKENI  karibu  na  CHUO CHA  TAKWIMU au  wasiliana  nasi  kwa  Simu : 0766538384.


Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA