Skip to main content

FARAJA KWA WANAWAKE WASIO SHIKA UJA UZITO.

Mgomba


Muembe.


FARAJA  KWA  WANAWAKE  WASIO SHIKA  UJAUZITO.
Katika  makala  yetu  ya  nyuma  tulielezea chanzo cha  tatizo  la wanawake  kutopata  ujauzito  ( Ugumba ) tukatoa  na  mapendekezo  ya  vitu  gani  vya  kufanya  kumsaidia  mwanamke  asiye  shika  ujauzito  aweze  kushika  ujauzito.

Kabla  sijaendelea  na  makala  haya  naomba  niwaombe  radhi  wasomaji  wangu  kwa  kutumia  neno ( ugumba ) hapo  juu, kwa  sababu  “ ugumba” ni  kitu  tusicho  kiamini  kabisa!  
Badala  ya  kumuita  mwanamke  mgumba, sisi  hutumia  neno    Mwanamke  ambaye  bado  hajapata  ujauzito  “.
Kupata  ujauzito  na  kuzaa  watoto  ni  haki  ya  kila  mwanamke  anaye  ishi   katika  dunia  hii  tunayo  ishi  mimi  na  wewe.
Kila  mwanamke  anapaswa  kuwa  na  “legitimate expectation “  ya  kupata  ujauzito  kwa  sababu  kupata ujauzito  ni  jambo  ambalo  Mungu  ameliahidi  na  kuliamuru  kwa  kila  mwanamke.
Kama  wewe  ni mwanamke  ambaye  bado  haujapata  ujauzito, haupaswi  kukata  tamaa hata  kidogo na  kudhani  labda  Mungu  amekusahau au amepanga  wewe  uwe  hivyo, la!
Kama  Mungu  alikumbuka  kukupa  vitu  kama  kucha, kope, vinyweleo  vya  miguuni  nakadhalika, sidhani  kama  atakuwa  ame  sahau  kukupa  mayai  ya  uzazi.
 Zipo  dawa  za  asili  za  aina  mbalimbali  ambazo  zimewasaidia  mamia  kwa  maelfu  ya  wanawake   kushika  ujauzito  na  kuzaa  watoto.

Nitakuwa  nazieleza  hapa  kila  nitakapo  kuwa  ninapata  nafasi  ya  kufanya  hivyo.
Leo  nitaanza  na  hii  ya  mizizi  ya  muembe  na  mgomba .

MAHITAJI  ;
i.                     Bakuli  moja  kubwa  la  Mizizi  ya  mwembe.
ii.                  Bakuli  moja  kubwa  la  Mizizi  ya  mgomba.
iii.               Maji  safi  na  salama  kiasi  cha  lita tatu.


MATAYARISHO
Chukua  mizizi  ya  mwembe, changanya  na  mizizi  ya  mgomba, weka  kwenye  sufuria  kisha  ongeza  maji  safi  na  salama  kiasi  cha  lita  mbili  halafu  chemsha  mpaka  mchanganyiko  wako  utakapo  anza  kutoa  supu. Chukua  supu  yako  na  uihifadhi  kwenye    chupa  ya  chai.

MATUMIZI :
Tumia  kikombe  kimoja cha  chai  cha  dawa  yako, mara  mbili  kwa  siku, asubuhi  na  jioni  kwa  muda  wa  siku  kumi  na  nne  na  bila  wasiwasi  wowote, utabeba  ujauzito.
Kama  huwa  unabeba  ujauzito  halafu  unatoka, dawa  hii  itakusaidia  sana.

Kwa  ushauri zaidi, wasiliana  nasi  kwa  Simu ;  0766538384.


Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA