Skip to main content

LISHE NA ULAJI UNAO FAA KWA WATU WANAO SUMBULIWA NA SHINIKIZO KUBWA LA DAMU ( HIGH BLOOD PRESSURE )



Mtu  mwenye  shinikizo  kubwa  la  damu  anashauriwa  kuepuka  matumizi  ya  chumvi.


Shinikizo kubwa la damu
Shinikizo kubwa la damu hutokea pale panapokuwa na ongezeko la nguvu ya msukumo wa damu katika mishipa inayochukua damu kutoka kwenye moyo kwenda kwenye viungo na tishu mwilini.
Ukubwa wa shinikizo kubwa la damu hutegemea wingi na nguvu ya msukumo wa damu kutoka kwenye moyo na ukubwa wa mishipa inayopeleka damu mwilini.

Viwango vinavyoashiria shinikizo kubwa la damu mwilini

Blood pressure machine (sphignomanometer) hutumika kupima shinikizo kubwa la damu.Kipimo kinachochukuliwa kuwa ni kawaida ni 120/80 mmHg au chini yake. 8
Kiwango kinapokuwa 140/90 mmHg au zaidi hali hiyo huwa ni shinikizo kubwa la damu.Ikumbukwe kuwa panaweza kuwepo tofauti kati ya mtu na mtu.

Viashiria hatarishi vya shinikizo kubwa la damu

Historia ya shinikizo kubwa la damu katika familia, Umri wa zaidi ya miaka 40, Jinsi ya kiume (huwapata wanaume zaidi kuliko wanawake),Uzito uliozidi kiasi, Msongo wa mawazo, matatizo mengine ya kiafya mwilini kama magonjwa ya figo, matatizo ya mishipa ya damu, magonjwa ya moyo, matatizo ya vichocheo mwilini, kisukari au saratani.Matumizi ya baadhi ya dawa na Kutokufuata mtindo bora wa maisha.

Dalili za shinikizo kubwa la damu:

Kichwa kuuma mara kwa mara hasa sehemu ya kisogo, Kizunguzungu, Kutokwa kwa damu pumuani, Maumivu ya kifua, Moyo kwenda kasi wakati umepumzika, Kushindwa kufanya mazoezi kwa kushindwa kupumua, Mapigo ya moyo kushuka wakati umepumzika, na Uchovu wa mara kwa mara.

Ulaji unaoshauriwa kwa mtu mwenye shinikizo kubwa la damu:

• Kuepuka vyakula venye chumvi nyingi, ikiwa ni pamoja na vile vilivyosindikwa kwa chumvi
• Kutumia viungo mbalimbali kuongeza ladha ya chakula( vitunguu swaumu, tangawizi, mdarasini, )
• Kuepuka vyakula vyenye mafuta na sukari nyingi
• Kula mlo kamili angalau mara tatu kwa siku ukizingatia kula vyakula vya aina mbalimbali
• Kula matunda na mbogamboga kwa kiasi cha kutosha katika kila mlo
• Kutumia nafaka zisizokobolewa na vyakula vya jamii ya kunde kwa wingi.

Mbinu za kupunguza uwezekano wa kupata shinikizo kubwa la damu

• Kuepuka vyakula venye mafuta mengi, sukari na chumvi nyingi
• Kuepuka mafuta yenye asili ya wanyama
• Kuepuka vyakula vyenye lehemu kwa kiasi kikubwa 

Comments

Popular posts from this blog

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na...

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ...

FAIDA KUMI ZA MTI WA MKOMAMANGA

Mti   wa   Mkomamanga   ni   mti   wenye   faida   nyingi   sana   katika   afya   ya   mwanadamu. Mti   huu   una   virutubisho –afya     mbalimbali   ambavyo   ni   muhimu   katika   afya   ya   mwanadamu.   Virutubisho   hivyo   vinapatikana   kwenye   magome, majani, mbegu, maganda   ya   matunda, juisi   ya   matunda   pamoja   na kwenye   maua   ya   mti   wa   mkomamanga. Zifuatazo   ni   faida   muhimu   za   mti   wa   mkomamanga : 1.           Maganda   ya   tunda   la   mkomamanga   yakichemshwa    hutoa   juisi    ambayo   hutumika   kama   dawa   ya   kufunga   kuhara. 2.   ...