Skip to main content

MAELFU WAFURIKA KWENYE MTO WA UPONYAJI!


Watu  wakioga  kwenye   kwenye  mto wa  Orimiri  Jordan
Maelfu  ya    watu  kutoka   maeneo  mbalimbali  ya  nchini  Nigeria  na  nchi  za  jirani  wanaendelea  kumiminika  katika   mto  wa  ajabu  ulio  batizwa  jina   Orimiri  Jordan  yaani  Mto  Yordani, kwa  ajili  ya  kupata    tiba  ya  magonjwa  na  matatizo  mbalimbali  yanayo  wakabili.
 Vyombo  vya  habari  nchini  Nigeria, vimekuwa  vikiripoti  mamia  ya  shuhuda  kutoka  kwa  watu  mbalimbali  walio  pokea  uponyaji     kwenye  mto  huo  wa maajabu.

Watu  wakiwa  kwenye  foleni  ya  kuingia  kwenye  mto  wa  uponyaji.
Taarifa  zinasema  kuwa, siku  ya   tarehe  11  Novemba  2013  mfugaji  mmoja  kutoka  katika  jamii  ya  wa  Fulani  alikuwa   anachunga   mifugo  wake  katika  eneo    moja  linalo julikana   Nachi  Orji   lililopo  katika  jimbo  la  Enugu.  Taarifa  zaidi  zinasema  kuwa  mtu  huyo  baada  ya  kupita  katika  eneo  hilo  ghafla  eneo  hilo  lilifunikwa  na  maji  na  kuonekana  kama  mtu.   Baada  ya  kushuhudia  tukio  hilo, mfugaji  huyo  alipeleka  habari  hizo  kwa  wenyeji  wa  eneo  hilo  akiwaambia  kuwa   maji  yameonekana  ghafla  katika  eneo  ambalo  halikuwa  na  maji. 

Mmoja kati  ya wazee  wenyeji  wa  eneo  ulipo  tokea  mto  huo  wa  maajabu, akitoa  maelezo  kwa  waandishi  wa  habari kuhusu   mto  huo  wa  maajabu.

Taarifa  zilisambaa  kwa  haraka  sana   kuanzia  kwa  wakazi  wote  wa  eneo  hilo, jimbo  la  Enugu  na  nchi  nzima  ya  Nigeria.
Ilifahamika  kuwa  wazee  wa  eneo  hilo  wanasema  si  mara  ya  kwanza  kwa  mto  huo  kutokea,  kwani  mara  ya  mwisho  mto  huo   ulitokea  ghfala  mnamo  mwaka  1971  na  kwamba  watu  mbalimbali  waliponywa  magonjwa  na  matatizo  yao  baada  ya  kuoga  katika  mto  huo  wa  maajabu.
Baada  ya  kuenea  kwa  taarifa  kuhusu  mto  huo, mamia  kwa  maelfu  ya  wananchi  wa  Nigeria  na  nchi  jirani  wamekuwa  wakifika  na  kuoga  katika  mto  huo  kwa  nia  ya  kupata  suluhisho  la  matatizo  mbalimbali  yanayo  wakabili.
Mpaka  wakati  huu, bado  hayajapatikana  maelezo  yoyote  ya  kisayansi  kuhusu  tukio  hilo  la  ajabu.
Kwa  habari  zaidi, tembelea  : http://naijagists.com/healing-river-orimiri-jordan-in-enugu-state-nigeria-fulanis-found-mysterious-pool-in-nachi-orji/

Comments

Popular posts from this blog

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na...

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ...

FAIDA KUMI ZA MTI WA MKOMAMANGA

Mti   wa   Mkomamanga   ni   mti   wenye   faida   nyingi   sana   katika   afya   ya   mwanadamu. Mti   huu   una   virutubisho –afya     mbalimbali   ambavyo   ni   muhimu   katika   afya   ya   mwanadamu.   Virutubisho   hivyo   vinapatikana   kwenye   magome, majani, mbegu, maganda   ya   matunda, juisi   ya   matunda   pamoja   na kwenye   maua   ya   mti   wa   mkomamanga. Zifuatazo   ni   faida   muhimu   za   mti   wa   mkomamanga : 1.           Maganda   ya   tunda   la   mkomamanga   yakichemshwa    hutoa   juisi    ambayo   hutumika   kama   dawa   ya   kufunga   kuhara. 2.   ...