Skip to main content

FAHAMU KUHUSU MADHARA YA MATUMIZI YA DAWA YA PANADOL

Panadol


Watu wengi wana mtizamo kuwa dawa zinazouzwa katika maduka ya dawa baridi na maduka ya kawaida ya vyakula, yaani zile ambazo hazihitaji agizo la daktari ( over-the-counter (OTC) drugs ) ni salama.
Ukweli ni kwamba hali haiko hivyo kabisa. Nyingi ya dawa zilizoko katika kundi hili huko nyuma zilikuwa ni miongoni mwa zile zilizosimamiwa na kuratibiwa kwa karibu, huku zikitolewa tu kwa agizo la daktari.


Pamoja na kuondolewa katika kundi la dawa zinazohitaji kutolewa kwa agizo la daktari, bado dawa za OTC ni kemikali ambazo mara nyingi haziondoi kiini cha tatizo ulilonalo, na zinaweza kukupelekea kupata madhara makubwa, ikiwa ni pamoja na kifo.
Mfano mmoja wapo ni dawa ya panadol, ambayo pia hujulikana kama paracetamol, acetaminophen, tyenol, nakdhalika.
Panadol ni dawa maarufu kweli kweli. Ni dawa maarufu hasa kutokana na uwezo wake wa kutuliza maumivu na pia kushusha homa haraka.
Watu wengi hunywa panadol bila ya kujiuliza chochote kuhusu usalama wake. Kupitia kwa wazazi na walezi wao, watoto wengi sana pia ni wabugiaji wa dawa hii.
Hii ni kutokana na wazazi/walezi wao kuamini kuwa kila mtoto anapolia basi mtoto ana maumivu, na au kila anapopata homa basi kuna ulazima wa kuishusha homa hiyo.
Kwa kiasi kikubwa tabia hii imejengwa na madaktari na wafamasia ambao nao hutoa dawa hii kwa wagonjwa bila kuzingatia usalama wake, na hivyo bila kutoa ushauri wowote kana kwamba dawa hizi ni salama kama maziwa!
Hatuna miundo mbinu ya kubaini idadi ya watu wanaoudhuriwa na matumizi haya ya kiholela ya panadol, lakini kwa kuangalia takwimu za nchi nyingine, bila shaka watu hao watakuwa ni wengi sana.
Nchini Marekani utumiaji uliopindukia wa panadol (overdose) umetambuliwa kuwa ndio sababu kuu ya simu zinazopigwa kuomba msaada katika vituo vya udhibiti wa sumu (Poison Control Centers) nchini humo, kila mwaka.
Panadol pia inatuhumiwa kuwa kila mwaka inasababisha kiasi cha watu zaidi ya 56,000 kupatiwa matibabu ya dharura, watu 2,600 kulazwa hospitalini, na kiasi cha watu 458 kupoteza maisha, katika taifa hilo. Sababu ya madhara haya inatajwa kuwa ni kushindwa kwa kiwango cha juu kwa ini kufanya kazi.
Taasisi ya chakula na dawa ya Marekani (US Food and Drug Administration (FDA)) mnamo mwaka 2009 ilitoa maelekezo kuwa vifungashio vya dawa hii viwekewe onyo kuhusu uwezekano wa dawa hii kuharibu ini la mtumiaji.
Hatua hii ilikuja miaka 32 baada ya jopo la wataalamu kutoa ushauri kwa FDA kuwa onyo hili lilikuwa ni suala la ‘lazima’!
Katika hatua nyingine, kwa nia ya kupunguza madhara, mnamo tarehe 14 Januari, 2014 FDA ilitoa kauli iliyokuwa ikiwahimiza wataalamu wa afya kuacha kuandika maagizo ya dawa (prescriptions) kwa dawa mchanganyiko ambazo miongoni mwake kulikuwa na vidonge (au vimiminika) vilivyokuwa na kiambata cha panadol kilichokuwa kikifikia kiasi cha miligramu 325. 
Ni vizuri kuzingatia kuwa baadhi ya dawa za maumivu zinazotolewa kwa maagizo ya daktari kama vile Vicodin na Percocet, pia zina kiambata cha panadol na kwa hivyo hazipaswi kuchanganywa na dawa zingine zenye kiambata hiki.
UTUMIAJI WA PANADOL WAKATI WA UJA UZITO UNAWEZA KUCHOCHEA UGONJWA WA UTUKUTU MKUBWA KWA WATOTO (Attention Deficit Hyperactivity Disorder –ADHD)
Hivi sasa kuna kundi la watafiti ambao wanahoji matumizi ya panadol kwa kina mama wajawazito.
Hoja yao ni kwamba matumizi ya dawa hii katika kipindi cha ujauzito yanaweza kusababisha mtoto atakayezaliwa kuwa na tabia ya utukutu uliokithiri.
Matokeo ya utafiti yaliyochapishwa katika jarida la JAMA Pediatrics, yanaonyesha kuwa panadol ni kitibua homoni ( hormone disruptor), na uwepo wa homoni usio wa kawaida mwilini wakati wa ujauzito unaweza kuathiri maendeleo ya kukua kwa ubongo wa mtoto anayeendelea kubadilika na kukua tumboni.
Utafiti huu ambao ulijumuisha takwimu zilizohusisha zaidi ya kina mama na watoto 64,000 kutoka katika kituo cha Taifa cha Kujifungulia cha Denmark (Danish National Birth Cohort), ulionyesha kuwa zaidi ya 50% ya wanawake waliohusishwa walitoa taarifa za kutumia panadol wakati wakiwa waja wazito.
Utumiaji huu wa panadol kwa wanawake hao olionyesha matokeo yafuatayo: 

• Ongezeko la 30% la hatari ya mtoto kukumbwa na ADHD katika miaka saba ya kwanza ya maisha yake. 
• Ongezeko la 37% la hatari ya mtoto kukumbwa na ugonjwa wa hyperkinetic disorder (HKD), ambao ni aina ya ADHD iliyopindukia mipaka.
Utafiti pia ulibaini kuwa kiwango cha madhara kilitegemeana na dozi. Kadri mama mjamzito alivyotumia panadol kwa wingi wakati wa ujauzito ndivyo jinsi ambavyo uwezekano wa mtoto kukumbwa na magonjwa yenye uhusiano na ADHD ulivyoongezeka. 

Aidha kwa mujibu wa utafiti huu watoto wa wanawake ambao walitumia panadol kwa majuma 20 au zaidi wakati wa ujauzito walikuwa na kiwango karibu mara mbili cha hatari ya kukutwa na ugonjwa wa HKD.

MADHARA MENGINE YA KIAFYA YANAYOHUSISHWA NA MATUMIZI YA PANADOL
Ukiondoa uharibifu wa ini, panadol pia imehusishwa na madhara mengine ya hatari kama uharibifu wa figo pale inaponywewa na pombe, saratani za damu, madhara yanayopelekea ngozi kukumbwa na magonjwa kadhaa kama Stevens-Johnson Syndrome (SJS), toxic epidermal necrolysis (TENS), na acute generalized exanthematous pustulosis (AGEP), na kuzuia chanjo zisifanye kazi vizuri pale vinapotumiwa pamoja..
KUDHIBITI MAUMIVU
Kwa kuwa watumiaji wengi wa panadol, hasa kwa watu wazima, hufanya hivyo kwa nia ya kupambana na maumivu, ni muhimu wakajifunza mbinu salama na mbadala za kuondoa hayo maumivu.
Moja ya mbinu mujarabu sana katika suala hili ni kuhakikisha kuwa muda wote mwili wako haukabiliwi na uhaba wa maji. Mwili wako unapokabiliwa na uhaba wa maji akili iliyoko mwilini mwako inawasha mfumo wa mgawo wa maji kidogo yaliyoko ndani ya mwili, ili kuzuia shughuli muhimu zinazotakiwa kuendelea mwilini zisije zikasimama.

Mfumo huu huratibiwa na kusimamiwa na homoni ya HISTAMINE, ambayo kunapokuwa na haja ya mgawo mwili huizalisha kwa wingi.

Kwa bahati mbaya ni kwamba katika harakati za kufanya kazi yake homoni hii pia huzalisha kiasi fulani cha maumivu katika maeneo mbalimbali ya mwili.
Ukiondoa uhaba wa maji mwilini, pia viko aina ya vyakula ambavyo huuchochea mwili kuzalisha kiasi kikubwa cha HISTAMINE.
Ulaji wa vyakula hivi ni kichocheo kikubwa cha maumivu ndani ya mwili kwa muda wote.
Mungu akipenda katika post yetu ijayo tutaviongelea vyakula hivi kwa kina.
Tatizo lingine linalosababisha maumivu mwilini ni seli za mwili kukumbwa na mfuro/uvimbe mwako (inflammation) kutokana na baadhi ya vyakula tunavyokula, au kutokana na kuugua ugonjwa wowote ule.
Mfuro/uvimbemwako ni zao la kinga za mwili pale zinapoingia katika mapambano na magonjwa mbalimbali.
Mfuro/uvimbemwako unapotokea kwa muda mfupi tu siyo tatizo sana.
Tatizo linakuwa pale ambapo mfuro/uvimbemwako huo umekuwa ni kitu cha kudumu.
Miongoni mwa dawa nyingi za kifamasia utakazopewa na daktari wako kwa ajili ya maumivu ni zile zinazolenga kuzuia mfuro/uvimbemwako.
Hata hivyo kutokana na dawa nyingi za kifamasia kuwa na usalama unaotia shaka ni bora mtu ukajaribu njia za asili (natural) za kuzuia mfuro/uvimbemwako.
Upunguzaji wa vyakula vya wanga, hususan vile vilivyochakatuliwa, na upunguzaji wa matumizi ya mafuta ya kupikia yanayotokana na mbegu (polyunsaturated fats) ni moja ya njia nzuri sana za kudhibiti hali hiyo.
Baadhi ya vitu vinavoliwa pia ni visawazishaji vikubwa vya mfuro/uvimbemwako.
Hivi ni pamoja na chai ya kijani (green tea), manjano (turmeric), karafuu, vitunguu saumu, matunda ya jamii ya berries (mfano zambarau), zabibu, na vitamini C.
Tatizo lingine linalosababisha maumivu ni makovu yanayojitokeza ndani kwa ndani mwilini kufuatia kuumia kwa tishu mbalimbali ndani ya mwili.
Ulaji wa vyakula vyenye vimeng’enya vyenye uwezo wa kuyeyusha makovu hayo (proteolytic enzymes) ni njia moja mujarabu sana katika kupambana na maumivu ya aina hii.
Bromelain ni kimeng’enya kinachopatikana katika kigogo cha katikati ya tunda la nanasi. Kimeng’enya hiki kimebainika kuwa na nguvu sana katika kufanya kazi hii.
Kimeng’anya kingine kinachpatikana katika matunda ambacho pia kinaweza kufanya kazi kama bromelain ni papain.
Papain ni kimeng’enya kinachopatikana kwa wingi katika tunda la papai.
Sababu nyingine kubwa ya maumivu ndani ya mwili ni kemikali zinazoitwa prostaglandins.
Prostaglandins ni kemikali muhimu sana katika kuratibu shughuli kadhaa za baadhi ya viungo ndani ya mwili kama vile utambuzi wa maumivu, upanukaji na usinyaaji wa mishipa ya damu, ufanyaji kazi wa mafigo, ufanyaji kazi wa mfumo wa uzazi wa mwanamke, ufanyaji kazi wa utando wa ndani wa njia ya chakula, nakadhalika.
Kutokana na moja ya kazi za prostaglands kuwa ni utambuzi wa maumivu, basi mfumo wa tiba za kisasa huchukulia kwamba kemikali hizi ni moja ya vyanzo vikubwa vya maumivu, na zimebuniwa dawa nyingi za kuzuia mwili kuzalisha kemikali hizi, au kuzizuia zisifanye kazi pale ambapo tayari ziko mwilini! Moja ya dawa maarufu sana katika suala hili ni asprin.
Tafiti za kisasa zinaonyesha kuwa asprin inafanya kazi hii kwa weledi mkubwa mno kiasi kwamba inafikia kuharibu seli za utando wa ndani wa njia ya chakula na kumsababishia mtumiaji vidonda hatari vya tumbo! Hata hivyo tafiti pia zimebaini kuwa kiungo cha tangawizi ni mujarabu sana na salama katika kudhibiti maumivu yanayooanishwa na prostaglandins. Chai ya tangawizi ya moto itakuondolea tatizo hili na kukuacha huru bila maumivu, lakini pia ukiwa salama kabisa.
Mbinu ingine ya asili na salama inayotumika kutuliza maumivu, hasa ya misuli, ni kutumia losheni au cream zenye kiambata cha menthol. Menthol ni kemikali inayochujwa kutoka katika kiziduo cha mmea unaoitwa mint au pepper mint. Losheni au cream yenye menthol hupakwa kwenye eneo lenye maumivu.
Menthol inapenya na kuingia ndani ambapo hupelekea mishipa ya damu katika eneo hilo kupanuka na kuongeza mtiririko wa damu katika eneo hilo. Kutokana na hali hii kemikali na virutubisho vinavyohitajika kufika katika eneo hilo na kurekebisha tatizo hufika kwa wingi ndani ya muda mfupi na kufanya kazi yake. Menthol pia hujenga mazingira ya kufanya eneo husika lijione kama limeingiwa na ubaridi. Ubaridi huu hupelekea kupoozwa kwa hali ya kujisikia moto kunakozalishwa na mfuro/uvimbe mwako katika eneo hilo.
KUDHIBITI HOMA
Tofauti na inavyodhaniwa na watu wengi, homa ya kawaida siyo kitu kibaya. Homa inakuwa tishio tu pale joto la mwili linapopanda sana na kuzidi nyuzi joto 104 katika kipimo cha Fahrenheit sawa na nyuzi joto 40 katika kipimo cha Celcius.
Homa ni silaha inayotumia pia na kinga za mwili katika jitihada za kukulinda. Vimelea vingi vya maradhi havina uwezo wa kuishi mwilini na kuzaliana katika joto la mwili linalofikia nyuzi joto hizi. Joto la mwili linapozidi nyuzi joto hizi kunakuwa na hatari ya kuzuka kwa uharibifu wa protini za mwili, haswa vimeng’nya pamoja na mafuta ya mwili.
Kutokana na hali hii ni vizuri kuisimamia homa yoyote kwa ukaribu kuhakikisha kuwa joto haliendi nje ya mipaka iliyokusudiwa. Homa yoyote ambayo joto litakuwa ndani ya mipaka iliyokusudiwa itakuwa ni msaada mkubwa kwa mgonjwa katika kuhakikisha kuwa anapona haraka.
Ni vizuri kuwa na kipima joto nyumbani kwa ajili ya kazi hiyo, badala ya kukimbilia kunywa panadol kila tunapoona kuwa homa imepanda. Kupitia kipima joto tukiona kuwa homa inataka kupindukia mipaka ni vizuri kutumia sponji au kitambaa kilicholowekwa kwenye maji ya baridi kumkanda mgonjwa na pia kumpa maji ya kunywa ya kutosha. Mbinu hii itasaidia kushusha joto la mwili la mgonjwa bila kumsababishia madhara. Dawa kama panadol zitumike tu pale ambapo jitihada nyingine zote za kurejesha joto katika hali ya kawaida zimeshindikana.

                 Credit   : HERBAL IMPACT

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA