Skip to main content

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI





UTANGULIZI
Vitunguu maji hulimwa kama zao la biashara katika sehemu nyingi
duniani zenye hali ya hewa ya ubaridi wastani. Zao hili lina wapatia
watu shughuli za kufanya na hivyo kuwapatia kipato kuanzia kwenye
nyanja za uzalishaji hadi kwenye matumizi. Nchini Tanzania,
vitunguu maji hulimwa kwenye mikoa ya Iringa wilaya ya Kilolo
mpakani mwa mkoa wa Morogoro na kwenye maeneo ya mto Ruaha,
mkoani Arusha sehemu za Mang’ora na Babati, Kilimanjaro, na
Morogoro wilayani Kilosa sehemu za Lumuma na Malolo na baadhi
ya sehemu za Mkoa wa Singida.
Hali ya Udongo

Vitunguu maji huhitaji udongo wenye rutuba, usiopasuka,
usiotuamisha maji na wenye mboji ya kutosha. Hali ya udongo katika
kipimo cha pH iwe kati ya 6.0 na 7.0.
Hali ya hewa
Hali ya hewa ifaayo ni ile ya ubaridi wastani. Joto linalohitajika ni
kati ya nyuzi joto 13 hadi 24°C ingawa kwa miche iliyoko kwenye
kitalu joto zuri ni la nyuzi 20 hadi 25°C. Joto la juu hufanikisha
utengenezaji wa kitunguu na ukaukaji.

Aina ya Vitunguu maji


Kuna aina nyingi ya vitunguu maji. Aina hizi zinaweza
kutofautishwa kulingana na:
(i) rangi ya ganda la nje la kitunguu kilichoishavunwa;
(ii) radha (utamu au ukali) wa kitunguu chenyewe;
(iii) mahitaji ya mwanga katika uzaaji: kuna aina yenye kuhitaji
siku fupi (mwanga wa saa 10 hadi 12 kwa siku) na aina
ihitajio siku ndefu (saa 13 hadi 14 za mwanga kwa siku) ili
kuweza kuweka kitunguu. Aina ya kwanza ndiyo ilimwayo
katika nchi za tropic.
Aina Siku za
kukomaa
Umbile
la
kitunguu
Rangi ya
ganda
Rangi ya
ndani
Red
Creole 150 Nusu
bapa Nyekundu Nyekundu -
kahawia
Red
Bombay 160 Duara Nyekundu
angavu
Nyeupe -
kahawia
Texas
Grano 165 Duara Njano
(Kaki) Nyeupe

Uoteshaji miche na Upandaji



Vitunguu maji huoteshwa zaidi kwa kutumia mbegu kwenye kitalu
na kisha kupandikizwa shambani. Kiasi cha kilo 3.5 cha mbegu hutoa
miche ya kutosha kupandikiza eneo la hekta moja ya shamba.
Kusiha mbegu kwenye kitalu
Mbegu zinasiwa kwenye kitalu kilichoandaliwa vizuri. Mbegu
hupandwa kwenye kina cha sentimita moja kwa kumiminwa polepole
kwenye mistari/mifereji iliyoandaliwa vizuri. Kisha mbegu hufukiwa
kwa kunyunyizia udongo juu ya mbegu zilizoko kwenye mifereji.
Mbegu huota baada ya siku 7 hadi 10. Lakini hii hutegemeana na hali
ya hewa. Kwani mbegu huweza kuechelewa kuota hadi mpaka siku
21 udongo unapokuwa wa baridi. Hali ya hewa ikiwa nzuri, mbegu
uota mapema zaidi, hata ndani ya siku 4.
Kupandikiza vitunguu shambani
Miche hupandikizwa inapokuwa na urefu wa sentimita 15 na unene
1/2 au 3/4 ya penseli kwenye shina. Miche hii huwa imetimiza umri
kati ya wiki 7 hadi 9 kulingana na matunzo. Miche inapandikizwa
kwenye nafasi ya upana wa sentimita 20 hadi 30 na nafasi ndani ya
mstari ni sentimita 10 hadi 15.
Kuandaa shamba
Kabla ya kupandikiza udongo utifuliwe vizuri na majani yaondolewe
kabisa. Kisha matuta au majaruba hutengenezwa ili kurahisisha
umwagiliaji.
Mbolea
Vitunguu maji vinamahitaji makubwa ya rutuba ya udongo. Hukua
vizuri vinapopata samadi ya kutosha kiasi cha tani 25 hadi 40. Kwa
hekta. Mbolea isambazwe shambani baada ya kupandikiza, lakini ni
vizuri zaidi kama ikichanganywa kwenye udongo kabla ya
kupandikiza. Kwa kuzingatia mazao ya tani 18 kwa hekta, vitunguu
huchukua kutoka katika udongo, kiasi cha wastani wa kilo 66, 11 na
70 za virutubisho aina ya Nitrojeni, Fosiforasi na Potasiam.
Hivyo kiasi cha mbolea kinachopendekezwa ni kilo 450 hadi 565 za
mbolea ya NPK (10-10-20) kwa hekta. Mbolea huwekwa siku 7 hadi
10 kabla ya kupandikiza. Kisha, inapendekezwa kuweka kiasi cha
kilo 13 hadi 18 za Nitrojeni baada ya wiki tatu hadi nne, ili kuongeza
ukuaji wa mimea. Upungufu wa kirutubisho cha Nitrojeni
unaharakisha ukomaaji na unapunguza ukubwa wa kitunguu.
Kirutubisho hiki kikizidi kupita kiasi huongeza ukubwa wa kitunguu
na unene wa shingo ya kitunguu, tabia ambayo upunguza ubora.
Umwagiliaji:
Umwagiliaji mzuri unahitajika ili kupata vitunguu bora. Umwagiliaji
wa maji yanayokwenda chini kiasi cha sentimeta moja au zaidi kwa
wiki ni mzuri kwa kupata vitunguu vikubwa. Epuka umwagiliaji
kupita kiasi au pungufu kwani hali hii huweza kusababisha
mipasuko.
Udhibiti wa magugu
Ukuaji na mavuno yanaathirika sana endapo magugu hayatadhibitiwa
mapema. Magugu yanadhibitiwa kwa kutumia madawa ama jembe
dogo la mkono. Wakati mwingine ni mchanganyiko wa madawa,
jembe la mkono na kungolea kwa mkono.
Udhibiti wa magonjwa
1. Ugonjwa wa doa la pinki (Purple blotch)
Uanza kama doa dogo linalozama ndani ya jani na kisha
linaongezeka ukubwa na kufanya rangi ya pinki. Kiini cha ugonjwa
huu huanzia kwenye mbegu na pia hubaki kwenye maozo ya majani
ya vitunguu. Aina ya Red Creole inaonyesha kutoshambuliwa sana
na ugonjwa huu.
Ugonjwa wa doa la pinki
Kuoza kwa kitunguu
Mbinu za kudhibiti ugonjwa huu ni kuendesha mzunguko (crop
rotation) wa muda mrefu wa mazao pamoja na kuzuia kutuama kwa
maji shambani. Kupunguza msongamano wa mazao shambani na
matumizi ya mbolea zenye calcium, phosphate and potassium
hupunguza kuenea kwa ugonjwa huu. Kwa upande mwingine,
matumizi ya mbolea ya nitrojeni kwa wingi au kwa kiasi pungufu
uongeza mlipuko wa magonjwa. Viatilifu kama vile Mancozeb
hutumika kuzuia mashmbulizi ya ugonjwa huu.
2. Ukungu wa unga (powdery mildew) na wa chini (Downy
mildew)
Magonjwa haya hushambulia majani ya mimea shamabani na hata
miche michanga. Kwenye majani kunaonekana vidoa vyeupe hasa
kwenye majani makuu ya mimea michanga. Ukungu mweupe
unatokea na kuongezeka kwa haraka kwenye sehemu au nyakati za
baridi. Viini huishi kwenye mabaki ya mimea ya vitunguu na huweza
kupeperushwa mbali na upepo. Kwenye mimea michanga ugonjwa
unaweza kudhibitiwa na madawa kama mancozeb.
3. Kuoza kwa vitunguu (bulb rots)
Hali hii inaweza kutokea shambani au wakati wa hifadhi ghalani.
Ugonjwa huu ni hatari zaidi kwenye sehemu za joto na zenye
kutuamisha maji. Ni vyema kuhakikisha kwamba shambani hakuna
hali ya kutuamisha maji na pia kwenye ghala kunakuwa na hali nzuri
ya mzuunguko wa hewa.
Udhibiti wa wadudu
Utitiri wa vitunguu (Onion thrips), Funza wa vitunguu (Onion
maggots) na Minyoo wa vitunguu (Onion wireworms) ni miongoni
mwa wadudu wasumbufu kwenye zao la kitunguu.
1. Utitiri wa vitunguu (Onion thrips)
Hawa ni wadudu wadogodogo sana ambao hula kwa kukwaruza juu
ya jani na kunyonya majimaji ya kwenye mmea. Hali husababisha
kutoka kwa mikwaruzo meupe kwenye majani ya vitunguu.
Mashambulizi yakizidi majani huanguka na kunyauka. Ukubwa wa
vitunguu hupungua. Hili ni tatizo kubwa zaidi hasa wakati wa ukame
kuliko wakati wa unyevu.
Utitiri wa vitunguu Madhara ya utitiri
2. Bungua weupe (White grub)
Huyu ni aina ya funza mkubwa. Hutaga mayai yake kwenye uozo wa
majani na samadi na hivyo mashamba ya vitunguu yaliyoko karibu
au kwenye maeneo ya jinsi hiyo huwa kwenye hatari zaidi.
Hushambulia mizizi na kusababisha kukauka kwa mimea. Kutifulia
shamba na kuwaweka wazi wadudu hawa kunapunguza idadi yao

Kwa  taarifa  zaidi, kuhusu  jinsi  ya  kuanza  kilimo  cha  vitunguu, wasiliana  na   SWAHILI  WATERWORKS  FARMING  LTD.

P. O. Box 1880, Morogoro
Tel: +255 758 303 090,+255 684 210 277
Email: swahiliwaterworks@gmail.com Website:

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA