Skip to main content

FAHAMU KUHUSU TIBA A SILIA YA KUUNGANISHA MIFUPA

Watu  wengi wanao pata  ajali  za barabarani  na  kuvunjika  viungo  vya mwili  ni  nadra sana  kukimbilia  kwa  wataalamu  wa tiba a silia.
Goodluck  Eliona  na  Warioba  Igombe, Gazeti  la  Mwananchi.
Morogoro  na  Dar Es  salaam.

Watanzania  walio  wengi  hukifahamu  kitengo  cha  mifupa  cha  Hospitali  ya  Taifa  ya   Muhimbili ( MOI )  kuwa  ni  kimbilio  muhimu  kwa  watu  walio   vunjika  mifupa  ya  viungo  vyao.
Lakini  kuna idadi  kubwa  ya  waganga wa  tiba asilia  wanao  dai  wana  uwezo  wa  kuunganisha  mfupa  ulio  vunjika  na  wanaaminika sana.






Hata  hivyo  tiba  hiyo  ya  asili  inakinzana  na  utaalamu  wa  tiba  za  kisasa.
Idadi  ya  watu  wanao  amii  uponyaji  wa  mifupa  unao  fanywa  na  waganga  wa  jadi  inaonekana  kuzidi  kuongezeka .
Lakini  tiba  hiyo  hufanywa  bila  ya  kufahamu  ukubwa  wa  tatizo.  Ni  wapi  wanapo kinzana ?

 AONAVYO  MGANGA  WA  TIBA  ASILIA
Joel  Kisome  (  57 ), mtaalamu bingwa  wa  mifupa  anaye  ishi  Morogoro, anaeleza  kuwa  anatibu  mifupa iliyo  vunjika  akitumia  mitishamba.
Uwani  mwake  kuna  zaidi  ya  wagonjwa  150  ambao  wamevunjika  mifupa   sehemu  mbalimbali  za  miili  yao.
  Sisi  hatuna  elimu  ya kisayansi kama  walivyo  wenzetu  wazungu, lakini  Mwenyezi  Mungu  alitujaalia  taaluma  hii  inayo wasaidia  watanzania  wenzetu”  anasema.

Laiti nasi  tungekuwa  tumeelimika  kisayansi, naamini  tungefika  mbali  hasa  katika  tiba  ya  mitishamba.
“ Mzungu  humpima  mwanaye  na  kujua  kitu  anachopenda  kukifanya  kimaisha  tangu  akiwa  mdogo  na  kumwendeleza  kielimu ili  kukuza  kipaji  chake  kitaaluma  kwa  kile  anachokipenda  tofauti  na  waafrika “
Hata  hivyo  Kisome  anaeleza  kuwa   tiba   ya asili  inaweza  kuwasaidia    watu  wengi  ndani  na  nje  ya  nchi, tatizo  ni  kwa  wataalamu  wake  kutothaminiwa  na  kusaidiwa  na  serikali.
Kisome  anasema   aliianza  kazi  hiyo  ya  tiba  mwaka  1972  wilayani  Bagamoyo  mkoani  Pwani  baada  ya  kuonyeshwa  dawa  hizi  na   baba  yake  mzazi, ambaye  pia  alikuwa  mganga  mahiri  wa  tiba  asili  wa  matatizo  ya  mifupa.  Anasema  ukaribu  na  baba  yake  mzazi  ndio  ulio mwezesha  kurithi  kazi  ile.

                 NI   WAPI    HUPATA   WATEJA    ?
Kisome  hupata wateja  wengi  kutoka  hospitalini, zikiwamo  za  Muhimbili  au  Bugando.  Wagonjwa  wengi  wao  wakiwa  wale   wasio  na  uwezo  wa  kugharimia  tiba  zao.
Hata hivyo  anaeleza  kuwa  wagonjwa  ni  wengi  kiasi  kwamba  wengine  hawezi  kuwahudumia.
Kuhusu  yeye  kufanya  kazi  hospitalini  kusaidiana  na  wataalamu  wa  tiba  ya  ya  kisasa  kuokoa  maisha  ya  wagonjwa,  Kisome  anajibu  kuwa  hawezi  kufanya  hivyo  ingawa   wamekuwa wakimhitaji.
 Anasema  hapendi  wala  hawezi  kufanya  hivyo  kwa  kuwa  hatakuwa  huru.
Anaeleza  kuwa serikali  haiwezi  kumpa  fedha  anazo  hitaji  mbali  na  kufanya  katika  mazingira  magumu, lakini  pia  hatakuwa  na  muda  wa  kupumzika.
ASEMAVYO  MTEJA  WAKE
Hosel  Juma  ambaye  amepachikwa  jina  la  utani “ Moi”  kwa  kuwa  alikaa  Muhimbili  kwa  mwaka  mmoja   na  miezi  minane  bila  nafuu, anasema  kuwa  tiba  za  asili  ni  bora  kuliko  zile  za  hospitalini.
“ Nimekaa   Muhimbili  ( Moi )  kwa  mwaka  mmoja  na  miezi  minane  bila  kupata   hata  nafuu.  Nimetumia  fedha  zangu  zaidi  ya   Sh. 2 milioni, lakini  ni  kama  nilizitupa “ anasema  Juma.
Anaeleza  kuwa  alipata   ajali  ya  gari alipokuwa  amepewa  lifti  na  kuvunjika  mguu  na  alipofikishwa   Moi  alipigwa   picha  ya  x-ray  mara  62, kufungwa  bandeji  ngumu  ( P.O.P )  mara  kumi, kuwekewa  vyuma  mara  mbili  bila  nafuu.
“ Mungu  mkubwa! Mbali  na  kupigwa  x-ray, kuwekewa  antenna  ( chuma  mguuni )  na  POP  kwa muda  mrefu  wakati  nikiwa   Muhimbili, sikupata  nafuu.
Tangu  nilipoletwa  hapa  kwa  mganga  na  mama  mdogo  anaye ishi  Morogoro, nina  miezi  mitatu  sasa  na  mguu  wangu  umepona” anasema.

KAULI  YA  KITAALAMU
Dk. Moiz  Vejlan  ambaye  ni  bingwa  wa  mifupa  katika  Hospitali  ya  Rufaa  ya    Mkoa  wa  Morogoro, anasema  kuwa  dawa  za  asili  za  mitishamba  si  mbaya  kwa  afya  ya  binadamu  katika  matumizi  ya  tiba, bali  inategemea    mgonjwa  mwenyewe  anavyo  iamini  hiyo  dawa  kama  tiba  yake.
“ Katika  tiba, kila  mtu  ana  imani  yake, kuna  wanao  amini  kuwa  dawa  za  mitishamba  ni  bora  kuliko  za  kitaalamu  na  wengine  huamini  kuwa  dawa  za  mitishamba  haziwasaidii  kwa  tiba” anasema  Dk. Vejlani.
Mtaalamu  huyoi  anaeleza  kuwa  wataalamu  wa  mitishamba  wamekuwa  wakipata  umaarufu  mkubwa  kutokana  dawa  wanazo  zitumia  kudaiwa  kuwaponyesha  wagonjwa  wengi, lakini  kitaalamu siyo  vizuri  kwani  wao  hutibu  mgonjwa bila  kujua  ukubwa  wa  jeraha  kwa  undani.
“ Kwa  kawaida  mtu  aliyevunjika  mfupa  lazima  apigwe  x-ray  ili  kujua  ukweli  na  ukubwa  wa  tatizo, lakini  kwa  wenzetu  wa  miti  shamba  hilo  halipo. Wao  hutumia  utaalamu  na  uzoefu  walio  jaliwa  na  Mungu  wao” anasema.
Dk. Vejilani  anasema  Hospitali  nyingi  hasa  za  serikali zinakabiliwa  na  changamoto  ya  vifaa  vya  kutibu  na  kuunganisha  mifupa, kitu  ambacho  kimekuwa  kikiwafanya   wagonjwa  wengi  kukimbilia  kwa  wataalamu    wa  mitishamba wakiamini  kuwa  hospitalini  hakuna  tiba.

“ Tunakabiliwa  na  changamoto  ya  ukosefu  wa  vifaa, kitu  kinacho  wafanya  wagonjwa  wengi washindwe  kuamini  kuwa  dawa  za  kitaalamu zinatibu  na  kukimbilia  kukimbilia  mitishamba”  anasema.
Anashauri  serikali  iwatambue  na  kuwathamini  kwa  kuwaandalia  mazingira  mazuri  wataalamu hao  wa  tiba a sili  kwani  wanawasaidia    watu  wengi, hususani  walio  vunjika  viungo.
Mtafiti   Mkuu  wa  Taasisi  ya  Utafiti  wa  Tiba  ( NIMR ), Dk. Julius  Massaga  anasema NIR haijawahi  kupokea   mganga  yeyote  wa  tiba  asilia ambaye   anataka  kuthibitisha  kuwa  dawa  yake  ya  asili  inaweza  kutibu  mifupa.
“ NIMR   kwa  sasa  inafanya  kazi  za  utafiti  wa  dawa  nyingie  tu  za  asili  lakini  si  zinazohusu  tiba  ya  mifupa.  NIMR  haifanyi  wala   hakuna  mganga  yeyote aliyeleta  maombi  ya  dawa  yake  kufanyiwa  utafiti “  anasema  Dk.  Massaga.

TIBA  YA  KIMASAI
Wamasai  hawako  nyuma, wao  ni  mabingwa  wa  tiba  asili  ya  mifupa;  kazi  ambayo  wameifanya muda  mrefu.
Wamekuwa  wakitumia  dawa  aina  ya ‘ beneuni’ kutibu  majeraha katika  mwili wa  mwanadamu  au  mnyama.
Jina  la  dawa  hiyo  limetokana  na  mti  wa  mbeneuni  ambao  unaaminika  kuwa  na  nguvu  ya  kuunga  jeraha  kwa  muda  mfupi  na  kuiacha  sehemu  hiyo  ikikauka  ndani  ya  saa  24.
Mtaalamu wa  dawa  za  kimasai, Simon  Ole  Kipayi  anasema  mti  wa  dawa  hiyo  unapatikana  katika  sehemu  chache  nchini  na  kwamba  kijiko  kimoja  cha  chai  huuzw  kati  ya  sh. 5,000  hadi  8,000  kutokana  na  uwezo  wake  mkubwa  wa  kutibu.
Ole  Kipayi  anasema  kuwa  mgonjwa  aliyejeruhiwa  au  kuvunjika  mfupa  anatakiwa  kuweka  unga  wa  dawa  hiyo  kwenye  jeraha  na  kuliacha  wazi  bila  kufunga, kwa  kuwa  kama  litafungwa  linaweza  kuoza.
“ Beneuni  huivuta  ngozi  na  kuliunganisha jeraha.  Kama  jeraha  likikaa  kwa  siku  tatu, utatakiwa  kuosha   kwanza  kwenye  sehemu  uliyo  umia  halafu  uweke  dawa”  anasema  Ole  Kipayi.

WENGINEO
Vero  Masinga , anayeuza  dawa  za  asili  katika stendi  ya  mabasi  ya  daladala  ya  Mbagala  Rangi-Tatu  jijini  Dar  Es  salaam, anasema  mwanaye  alijeruhiwa  kwa panga  mkononi, lakini  baada  ya  kuitumia  dawa  hiyo  aliyopewa  na  jirani  yake, jeraha  lilipona  kabisa   baada  ya  siku  tatu.
Anasema  ingawa  hafahamu  kama   dwa  hiyo  imethibitishwa  na  wataalamu  wa  afya, anasema  inaonyesha  uwezo  mkubwa  wa  kutibu  haraka  tofauti  na  baadhi  ya  dawa  zitolewazo  hospitalini.
“ Siku  hizi  ukienda  hospitali  kununua  dwa  unaweza  kuuziwa  dawa  feki, lakini  beneuni  ni  mti  ambao  mtu  yeyote  anaweza  kuutafuta  na  kuuweka  nyumbani  kwake”  anasema.
Hata  hivyo,  Masinga   anatoa  angalizo  kwa  wagonjwa  waio  fahamu  dawa  hiyo  kuwa  haitumiki  kutibu  mtu  aliyejeruhiwa  na  mnyama  au  nyoka  mwenye  sumu  kwa  kuwa  haina  uwezo  wa  kuondoa  sumu.
Alipotakiwa  kuzungumzia  ubora  na  matumizi  ya  dawa  hizo  na  nyingine  nchini, ofisa  uhusiano  wa  Mamlaka  ya  Chakula  na  Dawa  ( TFDA), Gaudensia  Simwanza  anasema  ofisi   hiyo  haihusiki  na  dawa  za  asili  ila  kuna  idara  maalumu  Wizara  ya  Afya inayo  shughulikia  dawa  za  asili.
 CHANZO : GAZETI   LA  MWANANCHI, TOLEO  Na. 4983, Ijumaa, 14  Machi  2014.

Comments

Popular posts from this blog

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ya  kupata  wapenzi  wa  kike  ama  kuoa  na  wengine  huendelea  na  tabia  hiyo  hata  baada  ya  kuoa .  Zipo  sababu  mbalimbali  zinazo  wapelekea  wanaume  kupiga  punyeto, ila  kubwa  kati  ya  hizo  ni  pamoja  na  kutokuwa  na  wapenzi, kutokuwa  na  wapenzi  wanao  kidhi vigezo  vyao, kuwa  katika  mazingira  yasiyokuwa  na  wanawake  ( mfano  katika  shule  za  sekonda

CHANZO NA TIBA ASILIA YA TONSILS

Dawa ya TONSILS ni (kugargar)  kusukutuwa maji yalokuwa si moto sana pamoja na chumvi mara 4 kwa siku yafike kooni. Pia unatakiwa usitumie pili pili manga wala tangawizi. Kwani watu wengi utasikia wanakunywa chai ya tangawizi na soup iliyojazwa pili pili manga. Kumbe unaona vizuri wakati unapokunywa lakini huwa unayavimbisha matonsils kwani baada ya nusu saa utaona unaumwa kuliko mwanzo na homa kuja juu. Uzuri kuwa unakunywa maji ya moto moto. Vile vile kuchukuwa mdomo wako na kuweka kwenye goti na kuwa unalipuliza bila kutoka pumzi mara kwa mara na kama hufikii goti lako basi unaweza kuchukuwa kanga na kufanya mfano wa mpira na kuwa unapuliza kila utakapokuwa na wakati, hii pia inasaidia. Usiwe unazungumza sana isipokuwa kwa dharura kwani ujaribu utakavyoweza upepo usipite kwenye mdomo wako. Sio lazima unywe maji baridi ndio upate Tonsils mfano A/c linapofanya kazi upepo wa baridi unapita kwenye mdomo wako basi unapata Tonsils Au wakati unapolala na A/c linafanya ka

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na  kuwa  mgumu  kama  msumari. Na  hatua  ya  pili   ni  lazima, uume  wake  uendelee  kusimama  kwa  muda  mrefu  wakati  wa  tendo  la  ndoa.  Hatua  zote  mbili  zinapo  kamilika, ndipo  tunapo  pata  kitu  kinaitwa  STRONGER  AND  LONGER  ERECTION JINSI  HATUA  ZA  KUSIMAMA  KWA  UUME  ZINAVYO  TOKEA. 1. HATUA    YA  KWANZA: DAMU  KUTIRIRIKA  KWA