Skip to main content

AVOCADO NA FAIDA ZAKE











Avocado likiwa linaandaliwa kwa kukamulia limao ili kuongeza ladha


Leo napenda niendeleze mada ya tunda la avocado pamoja na faida zake. Kabla ya kuongelea faida zake ningependa nielezee kwanza vitu ama virutubisho vinavyopatikana ndani ya tunda hilo. Vitu hivyo ni kama ifuatavyo;



MAJI: tunda hili lina kiasi kidogo cha maji tofauti na matunda mengine tuliyozoea kula.

MAFUTA: avocado lina kiwango kikubwa cha mafuta na ndani ya kiasi hicho cha mafuta kuna tindikali (acid) mbalimbali zinazosaidia kukinga na kutibu maradhi katika mwili.

PROTINI: tunda hili pia lina kiwango cha juu cha protini kutegemeana na aina ya tunda lenyewe. Ndani ya protini pia kuna tindikali (acid) aina ya amino.

VITAMINI "E": inadaiwa kuwa tunda hili lina kiwango kikubwa cha vitamini E kuliko ile inayopatikana kutoka kwenye mazao ya wanyama, hata mayai hayana kiwango kikubwa ukilinganisha na tunda la avocado.

VITAMINI "B6": Nayo inapatikana kwa wingi.

MADINI YA CHUMA (Iron): Pia yapo kwa wingi.



Baada ya kuvielezea baadhi ya virutubisho vinavyopatikana katika tunda hili, sasa tuangalie faida zinazotokana ama kwa kula au kutumia tunda la avocado au matumizi ya mmea wenyewe. Kwanza kabisa ningependa ujue kwamba majani ya mti wa avocado pamoja na magamba ya mti wake yakitengenezwa vizuri yanatumika kutibu maradhi ya kuharisha, kuondoa gesi tumboni, kutuliza kikohozi pamoja na matatizo ya ini na kusafisha njia ya mkojo. Dawa hii haishauriwi kutumiwa na akina mama wajawazito kwani inaweza kuwaletea matatizo yanayoweza kuharibu mimba. Aidha kwa wanawake ambao wameshindwa kuona siku zao kwa wakati, wanaweza kutumia mchanganyiko huo kwa nia njema ya kuwawezesha kuingia kwenye period.



Tunda la avocado ni chakula kizuri kwa watoto, pia lina madini ya potasiam (potassium) na vitamin B6 na E ambazo zinaweza kuleta nafuu kwa wale wenye matatizo ya stress, matatizo ya uzazi kama ugumba na uanithi. Tindikali aina ya oleic (oleic acid) iliyomo ndani ya tunda hili inasaidia kukinga dhidi ya magonjwa ya moyo, kiharusi na kansa. Aidha tunda hili linasaidia uyeyushaji wa chakula tumboni hasa kwa wale wenye matatizo ya vidonda vya tumbo, kwani tunda hili lina "fiber" ambayo ni muhimu kukinga kuta za utumbo. Watu wenye maradhi ya anaemia, diabetes, matatizo ya mfumo wa neva, matatizo ya artery wanashauriwa kula tunda hili mara kwa mara. Tunda la avocado limethibitishwa kupunguza kwa kiwango kikubwa cholesterol kutoka kwenye damu hasa kwa wale wenzangu na mimi ambao ni wanene.



Matumizi ya nje ya mwili kwa tunda hili husaidia kulainisha ngozi na kuondoa makwinyanzi, kung`arisha na kulainisha nywele na kuzifanya zionekane nadhifu, linasaidia ukuaji wa nywele na pia kuimarisha na kuzuia kukatika kwa nywele.

Comments

Popular posts from this blog

IJUE SAYANSI YA KUSIMAMA KWA UUME

Ukosefu  na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume, ni tatizo linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume duniani. Tatizo  la  ukosefu/upungufu  wa  nguvu  za  kiume ni  nini  ? Ukosefu  ama  upungufu  wa  nguvu za  kiume  ni  ile  hali  ya  mwanaume  kutokuwa  na  uwezo  wa kufanya  tendo  la  ndoa  kwa  ukamilifu HATUA  MBILI  MUHIMU  KATIKA  KUSIMAMA  KWA  UUME Ili  mwanaume   aweze  kufanya  tendo  la  ndoa  na  andelee  kufanya  tendo  la  ndoa, ni  lazima  uume wake  upitie  hatua  kuu  mbili  kama  ifuatavyo : Hatua  ya  kwanza , ni  lazima  uume  wake  uweze  kusimama  barabara  na...

TIBA YA ASILI YA KUACHA PUNYETO KWA WANAUME

Pilipili  Mbuzi Punyeto  ( kwa  wanaume  )  ni  kitendo   cha  mwanaume, kujifikisha  mwenyewe  kileleni  kwa  kujichua  uume  hadi  kumwaga  mbegu  za  kiume.  Uchunguzi  unaonyesha  katika  watu  wa  jinsia  ya  kiume  kumi  wenye  umri  wa  kuanzia  miaka  16  hadi  45, angalau  wanne  kati  yao  wamewahi  kupiga  punyeto  katika  kipindi  fulani  cha  maisha  yao, na  wawili  kati  yao  wanajihusisha  na  upigaji  punyeto. Uzoefu  unaonyesha, asilimia  kubwa  ya  wanaume  wanao  piga  punyeto  huanza  katika  umri  wa  kubalehe  ( miaka  14-16  ), wengine  huachana  na  tabia  hiyo  mara  baada  ...

FAIDA KUMI ZA MTI WA MKOMAMANGA

Mti   wa   Mkomamanga   ni   mti   wenye   faida   nyingi   sana   katika   afya   ya   mwanadamu. Mti   huu   una   virutubisho –afya     mbalimbali   ambavyo   ni   muhimu   katika   afya   ya   mwanadamu.   Virutubisho   hivyo   vinapatikana   kwenye   magome, majani, mbegu, maganda   ya   matunda, juisi   ya   matunda   pamoja   na kwenye   maua   ya   mti   wa   mkomamanga. Zifuatazo   ni   faida   muhimu   za   mti   wa   mkomamanga : 1.           Maganda   ya   tunda   la   mkomamanga   yakichemshwa    hutoa   juisi    ambayo   hutumika   kama   dawa   ya   kufunga   kuhara. 2.   ...