Skip to main content

Maajabu Ya Tunda la "Matongo Ga Mwarabu"Kutoka Tunduru mkoani Ruvuma.





Tunda  la  Matongo  Ga  Mwarabu
 
Ni miti mifupi sana inayojulikana na watu wa Tunduru kwaajili tiba nyingi toka enzi na enzi za wakazi wa Tunduru Ruvuma. Ni ngumu kupata jina lake kisayansi au katika kiswahili fasaha lakini kwa wakazi wa Tunduru ni Matunda yanayopendwa sana.
Zifuatazo ni faida za matunda haya:



1. Huongeza kumbukumbu- Mung'unya kama pipi matunda 2 hadi 4 kwa siku au kulingana na uhitaji wako.
2. Uvimbe- Sugulia mahali palipovimba asubuhi na jioni.
3. Kuumwa na nyuki, nge au manyigu- Loweka kwenye maji kisha paka mahali ulupong'atwa.
4. Nguvu za kiume- Mung'unya kama pipi matunda 7 masaa mawili kabla ya tendo.
5. Nguvu za kike na ashki- Fanya kama namba 4.
6. Mbu- Ili using'atwe na mbu loweka matunda kwenye maji kisha paka mwilini kama mafuta ya mgando.
7. Harufu mbaya sehemu za siri- Lowesha matunda kiasi kisha kunywa glasi moja au mbili na unawe sehemu za siri.
8. Homa- Loweka matunda kiasi kisha weka kwenye beseni ingiza miguu.
9. Jino- Jino linalouma weka tunda moja kwenye jino linalouma bila kumung'unya hadi utamu wa tunda utakapoisha.
10. BP- Mung'unya angalau matunda 8 kwa wiki.
NB- Matunda haya husitawi hasa nyakati za mvua. Yanapatikana pia Songea.
CREDIT :JAMII  FORUMS


Comments